Saturday 27 March 2010

Man United yarudi kileleni!!!
• Bolton 0 Man United 4
Wakiwa ugenini Reebok Stadium huku wakijua Wapinzani wao Chelsea wameirarua Aston Villa bao 7-1 na kukwea kileleni katika mechi iliyoanza mapema, Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu, Manchester United, wakicheza bila Mfungaji wao mkuu Wayne Rooney aliepumzishwa pamoja na Beki stadi Rio Ferdinand, nao waliirarua Bolton Wanderers kwa bao 4-0 na kurudi tena kileleni.
Baada ya mechi za leo, MSIMAMO LIGI KUU England huko juu ni kama ifuatavywo:
1. Man United mechi 32 pointi 72
2. Chelsea mechi 32 pointi 71
3. Arsenal mechi 32 pointi 68
4. Tottenham mechi 31 pointi 58
Hadi mapumziko Man United walikuwa mbele kwa bao la Jlloyd Samuel aliejifunga mwenyewe dakika ya 38 katika harakati za kuokoa krosi ya Ryan Giggs.
Kazi nzuri za Nani na Giggs zilizalisha bao 3 kipindi cha pili zilizofungwa na Dimitar Berbatov, mabao mawili na Darren Gibson, bao moja.
Vikosi vilivyoanza:
Bolton: Jaaskelainen, Ricketts, Cahill, Knight, Samuel, Muamba, Lee, Cohen, Wilshere, Elmander, Kevin Davies.
Akiba: Al Habsi, Taylor, Riga, Mark Davies, Klasnic, Andrew O'Brien, Weiss.
Man Utd: Van der Sar, Neville, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Fletcher, Scholes, Valencia, Giggs, Nani, Berbatov.
Akiba: Kuszczak, Park, Carrick, Rafael Da Silva, Macheda, Gibson, De Laet.
Refa: Martin Atkinson
LIGI KUU: Chelsea yaangusha kipondo Stamford Bridge!!!!
• Chelsea 7 Aston Villa 1
• Arsenal yakwama!!
Chelsea imeifumua Aston Villa bao 7-1 kwenye mechi ya Ligi Kuu Uwanjani Stamford Bridge na hivyo kutwaa uongozi wa Ligi wakiwa na pointi 71 kwa mechi 32 lakini Manchester United, wenye pointi 69 kwa mechi 31, wanacheza muda mfupi ujao na Bolton na ushindi kwao utawafanya waipiku Chelsea na kushika hatamu.
Hadi mapumziko Chelsea walikuwa mbele kwa bao 2-1.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Lampard, bao 4 mbili za penalti, Malouda 2 na Kalou bao moja.
Bao la Aston Villa lilifungwa na John Carew.
Chelsea na Aston Villa zitakutana tena Uwanjani Wembley kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA hapo Aprili 10.
Nao Arsenal wamenasa kwenye nafasi yao ya 3 baada ya kwenda sare 1-1 na Birmingham katika Uwanja wa Mtakatifu Andrew.
Arsenal sasa wamecheza mechi 32 na wana pointi 68.
Arsenal ndio waliopata bao kwanza dakika ya 81 kwa mzinga wa Samir Nasri lakini kwenye dakika za lala salama, dakika ya 92, patashika langoni kwa Arsenal ilimbabatiza Straika wa Birmingham Kevin Phillips na Kipa Manuel Almunia akazembea katika kuokoa na mpira kutinga wavuni.
MATOKEO: Jumamosi, Machi 27
Birmingham 1 v Arsenal 1
Chelsea 7 v Aston Villa 1
Hull City 2 v Fulham 0
Tottenham 2 v Portsmouth 0
West Ham 0 v Stoke City 1
Wolves 0 v Everton 0
Bondeni Viwanja Bomba
Afrika Kusini jana imetangaza kuwa Viwanja vyote 10 vitakavyochezewa mechi za Fainali za Kombe la Dunia kuanzia Juni 11 hadi Julai 11 vimekamilika baada ya FIFA kumaliza ukaguzi wao wa mwisho uliochukua siku10.
Mkuu wa Kamati ya Maandalizi ya Afrika Kusini Danny Jordan amesema: “Tumetimiza ahadi yetu ya kuwa na Viwanja bora kabla Mashindano kuanza na tena tumetimiza hili kabla ya muda wake!”
Kati ya Viwanja hivyo 10, sita ni Viwanja vipya kabisa na vinne ni vya zamani vilivyokarabatiwa.
Pompey wanaamini wameonewa!
Meneja wa Portsmouth Avram Grant anamini kuwa Ligi Kuu wamekosea kwa jinsi walivyokuwa wakiwatendea hasa uamuzi wa kuwazuia kutosajili Wachezaji uliofanywa Oktoba mwaka jana na ambao uliondolewa siku chache kabla ya dirisha la uhamisho kufungwa mwezi Januari.
Pompey wanakabiliwa na ukata mkubwa na wako chini ya Msimamizi maalum kuwanusuru wasifilisike na kufa na hilo limewafanya FA kuwakata pointi 9 hivyo kuwafanya wang’ang’anie mkiani mwa Ligi na kushuka Daraja ni, pengine, lazima kwao.
Tatizo hilo la kutosajili limeifanya Pompey iwe na uhaba wa Wachezaji na Grant, ambayo Timu yake inacheza na Tottenham leo kwenye Ligi Kuu, amedai: “Tuna Wachezaji 13 au 14 tu kwa mechi na Tottenham! Hili ni tatizo la uamuzi wao waliotufanyia Januari! Hatuwezi kushindana na Tottenham!”
Mbrazil Sandro kutua Spurs
Tottenham imethibitisha kumsajili Mchezaji wa Kimataifa wa Brazil Sandro, miaka 21, kutoka Klabu ya Internacional ya Marekani ya Kusini kwa dau la Pauni Milioni 6 na atajiunga na Tottenham mwanzoni mwa Msimu ujao.
Sandro, ambae ni Kiungo, ameichezea Timu ya Brazil ya Vijana Chini ya Miaka 21 mara 8 na kucheza mechi moja kwenye Kikosi cha kwanza cha Brazil ilipocheza na Chile Septemba mwaka jana katika mechi za mchujo za Kombe la Dunia.
Gerrard akiri kiwango chini msimu huu!!
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, amekiri Msimu huu kiwango chake kimekuwa chini ya kawaida yake na hilo limeifanya hata Liverpool kuyumba.
Liverpool tayari wapo nje ya UEFA CHAMPIONS LIGI, FA CUP na kwenye Ligi Kuu nafasi wanayoipigania ni kumaliza nafasi ya 4 na hivyo kucheza UEFA Msimu ujao lakini hata nafasi hiyo inategemea matokeo ya Timu nyingine na haipo mikononi mwao.
Kinyang’anyiro pekee ambacho kipo mikononi mwao ni EUROPA LIGI ambako wako Robo Fainali na watacheza na Benfica ya Ureno mwezi Aprili.
Gerrard amekiri: “Fomu yangu msimu huu hainipi furaha! Sishtuki kwani najua ntabadilika!”
LIGI KUU: Wikiendi hii patamu!!!
RATIBA
Jumamosi, Machi 27
Birmingham v Arsenal
Bolton v Man United
Chelsea v Aston Villa
Hull City v Fulham
Tottenham v Portsmouth
West Ham v Stoke City
Wolves v Everton
Jumapili, Machi 28
Burnley v Blackburn
Liverpool v Sunderland
TATHMINI:
Bolton v Manchester United
Vinara wa Ligi Kuu Manchester United watasafiri hadi Bolton kuikwaa Bolton Wanderers huku wakiwania ushindi wao wa tano mfululizo kwenye Ligi Kuu na hivyo kuimarisha kiu yao ya kutwaa Ubingwa kwa mara ya 4 mfululizo.
Bolton hivi karibuni wamekuwa wakipata mafanikio ambayo yamewafanya waweke pengo la pointi 8 kati yao na zile Timu zilizo hatarini kuporomoka Daraja.
Birmingham v Arsenal
Ushindi wa Chelsea huko Portsmouth siku ya Jumatano umewafanya Arsenal warudishwe nyuma hadi nafasi ya 3 na hivyo ushindi huko ugenini Birmingham ni muhimu kwao.
Arsenal watakuwa bila ya Sentahafu waoThomas Vermaelen aliefungiwa.
Kwa Birmingham mechi hii ni muhimu hasa baada ya kupoteza mechi mbili zilizopita.
Chelsea v Aston Villa
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti bila shaka atakuwa akiomba ule wakati mgumu kwao uwe umepita na hivyo kuifunga Timu ngumu Aston Villa iliyo nafasi ya 7 na inayowania nafasi muhimu ya 4 ili kucheza UEFA msimu ujao.
Katika mechi ya kwanza ya Ligi kati ya Timu hizi mbili, Aston Villa ndio waliibuka kidedea.
Tottenham v Portsmouth
Timu hizi zitakutana huko Wembley Aprili 11 kwenye Nusu Fainali ya FA CUP lakini kwa sasa kinyang’anyiro ni kiu ya Tottenham kuidhibiti nafasi ya 4 waliyokuwa nayo ili wacheze UEFA msimu ujao huku Portsmouth walio mkiani wakipigana kufa na kupona kutoshuka Daraja ingawa hilo sasa ni kudra ya Mungu tu hasa baada ya kupokwa pointi 9 na Ligi Kuu.
===================================================================
MSIMAMO LIGI KUU England:
1. Man United mechi 31 pointi 69
2. Chelsea mechi 31 pointi 68
3. Arsenal mechi 31 pointi 67
4. Tottenham mechi 30 pointi 55
---------------------------------------------------------------------------------------------
5. Man City mechi 30 pointi 53
6. Liverpool mechi 31 mechi 51
7. Aston Villa mechi 30 pointi 51
8. Everton mechi 31 pointi 48
9. Birmingham mechi 31 pointi 44
10. Blackburn mechi 31 pointi 38
11. Fulham mechi 30 pointi 38
12. Stoke mechi 30 pointi 36
13. Sunderland mechi 31 pointi 35
14. Bolton mechi 31 pointi 32
15. Wolves mechi 31 pointi 31
16. Wigan mechi 31 pointi 31
17. West Ham mechi 31 pointi 27
-----------------------------------------------------------------------------------------------
18. Burnley mechi 31 pointi 24
19. Hull mechi 30 pointi 24
20. Portsmouth mechi 31 pointi 13
========================================================================
West Ham v Stoke City
Baada ya kipigo cha 3-1 walichopewa na Wolves siku ya Jumanne, mechi hii ina maana kubwa sana kwa West Ham na hasa Meneja wao Zol hasa kufuatia manung'uniko ya Mashabiki wa West Ham.
West Ham wako pointi 3 tu juu ya Timu 3 za mwisho na ushindi ni kitu cha lazima kwao lakini Stoke City nao, ingawa wana afueni kidogo, katika mechi zao 10 zilizopita wameshinda mara mbili tu na hivyo wanahitaji kubadilika.
Hull City v Fulham
Hii ni mechi ya pili kwa Meneja mpya wa Hull, Ian Dowie, ya kwanza iliisha kwa kuchapwa na Portsmouth dakika za lala salama kwa bao 3-2.
Lakini hii ni mechi ngumu kwa Hull kwani wanakutana na kigaga Fulham ambao ndio kwanza wanatoka kwenye huzuni ya kubwagwa nje ya Kombe la FA walipotwangwa bao 3-1 na Tottenham hapo Jumatano katika mechi ya marudio.
Wolves v Everton
Wolves wanaikaribisha Everton ambayo imeingia kwenye ile ‘Ligi ndogo’ ya kuwania nafasi ya 4 kwani sasa wako pointi 3 nyuma ya wagombea wengine wa nafasi hiyo ya 4, Liverpool na Aston Villa.
Mafanikio katika mechi za hivi karibuni zimewafanya Wolves wajikite kwenye nafasi za usalama na matokeo mazuri dhidi ya Everton yatawafanya wajenge zaidi uhai wao.
Burnley v Blackburn
Hii ni mechi ya kwanza siku ya Jumapili na ni ya kufa na kupona kwa Burnley walio nafasi ya 18 wakiwa moja ya Timu 3 zilizo nafasi za kushushwa Daraja.
Kwa Blackburn, walio kwenye usalama mkubwa ukilinganisha na Burnley, hii ni mechi itakayozidi kuwakikishia usalama endapo watashinda
Liverpool v Sunderland
Wengi watakumbuka kipigo cha Liverpool toka kwa Sundeland katika mechi ya kwanza ya Ligi hasa baada ya goli la ushindi la Sunderland kufungwa na Darren Bent kwa msaada mkubwa wa “Bichi Boli”.
Liverpool ndio kwanza wanatoka kwenye kipigo cha 2-1 toka kwa Mahasimu wao wakubwa Manchester United na hivyo kuwayumbisha kwenye azma yao ya kuinyakua nafasi ya 4 ya Ligi ili wacheze UEFA msimu ujao na hivyo matokeo mazuri katika mechi hii ni muhimu.
Sunderland watataka kuendeleza wimbi la kutofungwa katika mechi yao ya 6 mfululizo.

Friday 26 March 2010

Bifu la Mancini v Moyes: Sasa Mancini ana kesi na FA!!
Roberto Mancini ameshitakiwa na FA kwa kosa la kutokuwa na mwenendo mzuri kufuatia kufarakana kwake na Meneja wa Everton David Moyes katika mechi ya Ligi Kuu hapo juzi kati ya Manchester City na Everton Uwanja wa City of Manchester ambayo Everton walishinda 2-0.
Bosi huyo wa Manchester City alimvaa Moyes aliekuwa ameushika mpira uliotoka nje ili kutoa nafasi Timu yake ibadili Mchezaji lakini Mancini akataka kumpora mpira huo na ikatokea mshikemshike ulioamuliwa na Mwamuzi wa Akiba howard Webb na Walinzi wa Uwanjani hapo.
Baada ya Mancini na Moyes kutenganishwa Refa wa mechi hiyo Peter Walton aliwatoa nje ya Uwanja wote Mancini na Moyes.
Ingawa David Moyes amepona mashitaka, FA imemwandikia barua kumkumbusha majukumu na mwenendo wake kama kiongozi.
Moyes amesema tukio hilo ni dogo na Mancini alimwomba radhi mara baada ya kutokea na yeye hana kinyongo chochote.
Mancini amepewa mpaka Aprili 6 kujibu mashitaka hayo na Kamisheni ya Sheria itakaa Aprili 19 kutoa uamuzi.
Nani asaini Mkataba wa Miaka 4 Man United
Winga wa Manchester United kutoka Ureno, Nani, miaka 23, amesaini Mkataba mpya wa miaka minne na Klabu yake.
Nani, ambae alijiunga Man United mwaka 2007 akitokea Sporting Lisbon, alikuwa amebakisha miaka miwili katika Mkataba wake wa sasa.
Meneja wa Man United, Sir Alex Ferguson, akithibitisha habari hizo, alisema: “Ameibuka kama kipaji na amepata maendeleo makubwa hapa!”
Mwenyewe Nani, ambae ameshachezea mechi 97 na kuifungia Man United mabao 12, ametamka: “Nimefurahia Mkataba mpya! Ni ndoto iliyotimia kuichezea Man United! Makocha wamenifundisha mengi na nacheza miongoni mwa Wachezaji bora duniani! Natazamia kubeba Vikombe vingi na Timu hii!”
Mourinho bubu!!
Kocha machachari na mwenye vituko vya hali ya juu wa Inter Milan, Jose Mourinho, ataendelea kutozungumza na Waandishi wa Habari kabla na baada ya mechi nyeti ya wikiendi hii ya Ligi Serie A watakapoumana na Timu ngumu AS Roma.
Uamuzi huo umethibitishwa na Klabu ya Inter Milan.
Mourinho aligoma kuongea na Waandishi mara baada ya kufungiwa mechi 3 kufuatia ishara ya mikono ya alama ya pingu aliyoitoa kwenye mechi na Sampdoria wakati Inter Milan ilipotoka sare 0-0 na Wachezaji wake wawili kupigwa Kadi Nyekundu kwenye mechi hiyo.
Tangu kifungo hicho cha mechi 3, mara pekee Mourinho alipoongea na Waandishi ni kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Mourinho, ambae hana uhusiano mzuri na Vyombo vya Habari vya Italia, amekuwa akiwapeleka Wachezaji kuongea na Waandishi mara baada ya mechi.
Siku ya Jumatano, Inter Milan ilipoitandika Livorno bao 3-0, Mchezaji Ivan Cordoba ndie alieongea na Waandishi.
Platini bado ataka ulaji UEFA
Rais wa UEFA, Nyota wa zamani wa Ufaransa, Michel Platini, atasimama tena kugombea kwa mara ya pili nafasi ya Urais wa UEFA mwakani nafasi hiyo itakapopigiwa kura.
Platini, miaka 54, alichukua wadhifa huo wa Rais wa UEFA mwaka 2007 kutoka kwa Lennart Johansson na anategemewa kutopata Mpinzani kwenye uchaguzi wa mwakani.
Wakati huohuo, Platini amesema Brazil, England na Spain ndizoTimu zinazotegemewa kushinda Kombe la Dunia ambazo Fainali zake zitachezwa Juni 11 hadi Julai 11 huko Afrika Kusini.
Brazil wameshawahi kuwa Mabingwa wa Dunia mara 5, England mara moja na Spain, ambao ndio Mabingwa wa Ulaya, hawajawahi kuwa Mabingwa wa Dunia.
Hata hivyo, Platini amezitaja Nchi nyingine, anazotegemea kuwa ngumu na tishio kwa Vigogo hao watatu aliowataja, ni Nchi za Argentina, Ufaransa, Uholanzi, Italy, Ivory Coat na Ureno.
Celtic ya Scotland yamtimua Meneja wake!!
Klabu Kongwe ya huko Scotland, Celtic, imemfukuza kazi Meneja wake Tony Mowbray kufuatia kipigo cha Timu hiyo cha 4-0 mikononi mwa St Mirren siku ya Jumatano.
Kipigo hicho cha 4-0 kimewafanya Celtic wawe pointi 10 nyuma ya Mahasimu wao wakubwa Rangers walio vinara wa Ligi Kuu Scotland.
Nahodha wa zamani wa Celtic Neill Lennon ambae amekuwa akifanya kazi Klabuni hapo kama Kocha amepewa wadhifa wa Meneja wa muda hadi hapo Klabu itakapompata mtu wa kudumu.
EURO 2012: Mashabiki wachukizwa mechi za England kuchezwa Ijumaa
Mashabiki wa England wamechukizwa na hatua ya FIFA kubadilisha Kalenda ya mechi za Kimataifa na kufanya moja ya siku ya mechi za Kimataifa kuwa Ijumaa ili kuwawezesha Wachezaji kurudi kwenye Klabu zao siku moja kabla.
David Taylor, Sekretari wa UEFA, amesema wao wamelazimika kuufuata uamuzi wa FIFA ambao aliuita ni wa kufurahisha Mameneja wa Klabu.
Ingawa FA, Chama cha Soka England, kimesema hakina pingamizi lolote kwa England kucheza Ijumaa, lakini Msemaji wa Chama cha Mashabiki wa England, Mark Perryman, amedai kwa Mashabiki wa England waishio London hilo halina ubaya lakini kwa wale walio nje ya London ni ngumu kwenda Wembley kwani Ijumaa ni siku ya kazi.
RATIBA ya Mechi za England:
IJUMAA, Septemba 3, 2010: England v Bulgaria
JUMANNE, Septemba 7, 2010 Switzerland v England
JUMANNE, Oktoba 12, 2010 England v Montenegro
JUMAMOSI, Machi 26, 2011 Wales v England
JUMAMOSI, Juni 4, 2011 England v Switzerland
IJUMAA, Septemba 2, 2011 Bulgaria v England
JUMANNE, Septemba 6, 2011 England v Wales
IJUMAA, Oktoba 7, 2011 Montenegro v England
LIGI KUU: RATIBA Mechi za Wikiendi hii
Jumamosi, Machi 27
Birmingham v Arsenal
Bolton v Man United
Chelsea v Aston Villa
Hull City v Fulham
Tottenham v Portsmouth
West Ham v Stoke City
Wolves v Everton
Jumapili, Machi 28
Burnley v Blackburn
Liverpool v Sunderland
Jumatatu, Machi 29
Man City v Wigan
FA CUP: NUSU FAINALI kuchezwa Wembley Stadium
Aprili 10: Chelsea v Aston Villa
Aprili 11: Tottenham v Portsmouth
[FAHAMU: Tottenham alimfunga Fulham 3-1 katika mechi ya Marudio Jumatano Machi 24]
Chelsea yakumbwa na Majeruhi kibao!!
Wamebakiwa na Masentahafu wawili tu!
Chelsea wanaowania Ubingwa wakiwa nyuma ya vinara wa Ligi Kuu Manchester United kwa pointi moja tu wamepata pigo kwenye mechi ya jana ya Ligi waliyowabamiza Portsmouth 5-0 baada ya Beki wao Rivardo Carvalho kuumia.
Carvalho, miaka 31, aliumia enka na huenda akafanyiwa opersheni ambayo itamweka nje kwa zaidi ya mwezi.
Kuumia kwa Carvalho kumeifanya Chelsea ibakiwe na Masentahafu wawili tu, Mbrazil Alex na Nahodha John Terry, kwani Mchezaji mwingine ambae hucheza Sentahafu, Branislav Ivanovic, aliumia Jumapili iliyopita walipotoka sare na Blackburn bao 1-1 na inasemekana atakuwa nje kwa muda mrefu.
Majeruhi wengine wa muda mrefu Klabuni Chelsea ni Beki wa kushoto Ashley Cole [enka], Michael Essien [goti] na Jose Bosingwa [enka].
Jumamosi hii inayokuja, Chelsea wapo kwenye Ligi Kuu na wanacheza na Aston Villa, kisha Jumamosi inayofuata, Aprili 3, wako Old Trafford kucheza na Manchester United kwenye Ligi Kuu na Aprili 10 wako Wembley kucheza Nusu Fainali ya Kombe la FA watakapoikwaa Aston Villa.
Scholes ataka ushindi mechi 7 ili kuwa Bingwa!!!
Paul Scholes ana imani kubwa yeye na wenzake Manchester United wana uwezo wa kushinda mechi zote 7 zilizobaki za Ligi Kuu na hivyo kutetea taji lao la Ubingwa kwa mara ya 4 mfululizo na hivyo kuweka rekodi kwa kuwa Timu ya kwanza kutwaa Ubingwa mfululizo mara 4.
Pia, mpaka sasa Manchester United na Liverpool ndizo zinafungana kwa kuchukua Ubingwa mara 18 zikiwa ndio zilizoutwaa mara nyingi.
Katika mechi hizo 7 zilizosalia zipo mechi na Chelsea, Manchester City na Tottenham lakini Scholes anasema: “Mechi na Chelsea ni kubwa na lazima tushinde! Tunao Wachezaji bora ambao washawahi kuwa kwenye hali hii hivyo wanajua wajibu wao!”
Scholes akaongeza: “Huwezi ukawatoa kwenye hesabu Arsenal hasa kwa mechi zao zilizobaki! Washacheza na Timu kubwa zote na watakuwa na imani watashinda mechi zao! Lakini sisi tunajua Ubingwa uko mikononi mwetu! Tukishinda mechi zetu zote ni Mabingwa!”
MSIMAMO LIGI KUU England KWA TIMU ZA JUU:
1. Man United mechi 31 pointi 69
2. Chelsea mechi 31 pointi 68
3. Arsenal mechi 31 pointi 67
4. Tottenham mechi 30 pointi 55
MECHI ZILIZOSALI KWA VIGOGO WATATU: Arsenal, Chelsea & Man United
ARSENAL
Machi 27=Birmingham v Arsenal
Aprili 3=Arsenal v Wolves
Aprili 10=Tottenham v Arsenal
Aprili 18=Wigan v Arsenal
Aprili 24=Arsenal v Man City
Mei 1=Blackburn v Arsenal
Mei 9=Arsenal v Fulham
CHELSEA
Machi 27=Chelsea v Aston Villa
Aprili 3=Man United v Chelsea
Aprili 13=Chelsea v Bolton
Aprili 17=Tottenham v Chelsea
Aprili 25=Chelsea v Stoke
Mei 1=Liverpool v Chelsea
Mei 9=Chelsea v Wigan
[FAHAMU=Aprili 10 Chelsea v Aston Villa (Nusu Fainali FA CUP, Wembley Stadium)
MAN UNITED
Machi 27=Bolton v Man United
Aprili 3=Man United v Chelsea
Aprili 11=Blackburn v Man United
Aprili 17=Man City v Man United
Aprili 25=Man United v Tottenham
Mei 1=Sunderland v Man United
Mei 9=Man United v Stoke

Thursday 25 March 2010

Bifu la Mancini v Moyes!!!
Mameneja wa Manchester City, Roberto Mancini, na wa Everton, David Moyes, huenda wakakabiliana na Pilato wa FA baada ya kufarakana wakati wa mechi ya Ligi Kuu hapo jana Uwanjani City of Manchester, mechi ambayo Everton waliinyuka Man City 2-0.
Sakata hilo lilitokea mpira ulipotoka nje ya uwanja na Moyes kuushika huku akigonja kubadilisha Mchezaji na ndipo Mancini akamvaa na kutaka kumpora mpira na ndipo mshikemshike ukaanza na kulazimu Refa wa Akiba Howard Webb na Walinzi kuwatenganisha.
Mameneja hao wawili wakatolewa nje ya Uwanja na Refa.
Alipohojiwa baada ya mechi, Mancini alijaribu kulipoza tukio hilo na kusema ameshaongea na kuomba radhi kwa mwenzake Moyes na mambo yote yamekwisha.
Nae Moyes amedai tukio hilo ni dogo na ameshangazwa mno kutolewa nje na Refa.
Katika mechi hiyo mabao ya Everton yalifungwa na Tim Cahill na Mikel Arteta.
Pompey 0 Chelsea 5
Jana, kwenye Ligi Kuu, Chelsea iliiwasha Timu taabani Portsmouth mabao 5-0 na kuipiku Arsenal kwenye nafasi ya pili.
Manchester United wanaongoza wakiwa na pointi 69, Chelsea wa pili pointi 68 na Arsenal ni wa tatu wakiwa na pointi 67. Kila Timu imecheza mechi 31 na kubakiza mechi 7.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Drogba, bao mbili, Malouda, bao mbili, na Lampard moja.
Katika mechi nyingine za jana za Ligi Kuu matokeo ni:
Man City 0 Everton 2
Blackburn 2 v Birmingham 1
Aston Villa 1 v Sunderland 1
Beckenbauer: Rooney ni hatari!!!
Rais wa Bayern Munich ambae alikuwa Supastaa wa Ujerumani zamani, Franz Beckenbauer, amekiri Wayne Rooney ndie hatari kubwa kwao katika kiu yao ya kutwaa Ubingwa wa Ulaya.
Beckenbauer amesema Rooney anaifanyia kazi nzuri Timu yake Manchester United na kufunga goli 33 katika msimu si kitu kidogo kwa Soka la siku hizi.
Veterani huyo amesema: “Ni Mchezaji hatari! Sisi Bayern tunamwogopa na tunamgwaya kucheza nae kwenye Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI!”
Msimu huu,Manchester United na Bayern Munich zitakutana Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na mechi hizo ni kumbukumbu kwa wengi Fainali ya mwaka 1999 ya UEFA CHAMPIONS LIGI Man United walipoibwaga Bayern Munich 2-1 kwa goli mbili za dakika za majeruhi zilizofungwa na Teddy Sheringham na Ole Gunnar Solskjaer.
Man United na Bayern Munich zitacheza mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONS LIGI huko Ujerumani Machi 30 na marudiano ni Old Trafford Aprili 7.
Vilevile, Beckenbauer amesema Rooney anao uwezo wa kuiletea ushindi England huko Afrika Kusini katika Fainali za Kombe la Dunia.
Nae Meneja wa zamani wa Bayern Munich Jurgen Klinsmann amesema: “Rooney ni mkali msimu huu. Ametulia, anajiamini na akiendelea hivi basi atachaguliwa Mchezaji Bora Ulaya!”
Pompey waruhusiwa kuuza Wachezaji
Portsmouth wamepewa kibali maalum na Ligi Kuu kuuza Wachezaji wao nje ya dirisha la uhamisho ili kupoza ukata unaoikabili Klabu hiyo.
Klabu hiyo ambayo tayari imeshakatwa pointi 9 na ipo mkiani kwenye wa msimamo wa Ligi na hilo, bila shaka, litawashusha Daraja,wameruhusiwa kuuza Wachezaji lakini hawaruhusiwi kuchezea Timu za kwanza za Klabu za Ligi Kuu.
Hata hivyo Msimamizi maalum wa Klabu hiyo Andrew Andronikou amesema: "Ingawa kuuza Wachezaji ni moja ya mikakati lakini kwa sasa hatulazimiki kufanya hivyo kwani kufika kwetu Nusu Fainali Kombe la FA kumetupa pesa za kujiendesha.”
Pompey waliomba kuuza Wachezaji mwezi Februari lakini waligomewa na Ligi Kuu.
Klabu hiyo imepewa masharti ya kuuza Wachezaji nayo ni:
-Wachezaji hawaruhusiwi kuchezea Timu za kwanza za Ligi Kuu hadi msimu umalizike.
-Wanaweza kuingia mkataba na Klabu nyingine kwa sasa ili Mchezaji ahamie huko mwishoni mwa msimu.
-Mauzo ya Mchezaji yeyote lazima yaidhinishwe na FIFA.
Kawaida kuna madirisha mawili ya uhamisho, moja ni Januari 1 hadi 31 na la pili ni Juni 1 hadi Agosti 31.
Mwezi Januari Portsmouth waliuza Wachezaji watatu.

Wednesday 24 March 2010

MECHI ZA LEO JUMATANO Machi 24:
FA CUP
Tottenham v Fulham [Marudio ya Robo Fainali baada ya kutoka sare 0-0]
LIGI KUU
Portsmouth v Chelsea
Man City v Everton
Blackburn v Birmingham
Aston Villa v Sunderland
=======================================================================
MSIMAMO LIGI KUU England:
1. Man United mechi 31 pointi 69
2. Arsenal mechi 31 pointi 67
3. Chelsea mechi 30 pointi 65
4. Tottenham mechi 30 pointi 55
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
5. Man City mechi 29 pointi 53
6. Liverpool mechi 31 mechi 51
7. Aston Villa mechi 29 pointi 50
8. Everton mechi 30 pointi 45
9. Birmingham mechi 30 pointi 44
10. Fulham mechi 30 pointi 38
11. Stoke mechi 30 pointi 36
12. Blackburn mechi 30 pointi 35
13. Sunderland mechi 30 pointi 34
14. Bolton mechi 31 pointi 32
15. Wolves mechi 31 pointi 31
16. Wigan mechi 31 pointi 31
17. West Ham mechi 31 pointi 27
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
18. Burnley mechi 31 pointi 24
19. Hull mechi 30 pointi 24
20. Portsmouth mechi 30 pointi 13
======================================================================
Wachezaji Pompey waokoa ajira za Wafanyakazi!!
Imebainika Wachezaji wa Klabu taabani Portsmouth, ambayo iko mkiani Ligi Kuu, imekatwa pointi 9 na Ligi Kuu na yenye ukata mkubwa wa fedha, wamejichangisha ili kuokoa ajira za Wafanyakazi wanne waliokuwa hatarini kutimuliwa muda wowote ule ili kuungana na wengine 85 waliopunguzwa hivi karibuni.
Lakini Wachezaji wa Timu hiyo, wakiongozwa na Nahodha Kipa David James, wameamua kuchanga Pauni 1500 kila mtu ili kuwanusuru Wafanyakazi hao wanne ambao ni Msimamizi wa Matengenezo wa Uwanja, Mchua Musuli na wengine wawili.
Meneja wa Portsmouth, Avram Grant, akithibitisha taarifa hizo, amesema: “Wachezaji, mimi mwenyewe na wengine, wametoa mchango wao kwa moyo mkunjufu. Hawa Wafanyakazi wanne wako hapa kabla yetu na watakuwa hapa hata tukiondoka!”
Mmoja wa Wafanyakazi hao, Tug Wilson, ambae ndie Msimamizi wa Uwanja, amenena: “Siku hizi tunasikia mengi mabaya kuhusu Wachezaji lakini kitendo cha Wachezaji hawa ni utu na ni kitu cha kushangaza!”
Avram Grant ameongeza: “Tug yuko hapa miaka mingi, ana kazi ngumu kuanzia asubuhi hadi usiku na mshahara mdogo. Nina furaha atabaki. Ikifika wakati Klabu inakosa utu wake basi imekwisha!”
Arsenal haina ubavu kuwa Mabingwa, adai Arshavin!!!
Andrey Arshavin, Fowadi wa Arsenal kutoka Urusi, ana hofu kwamba Arsenal haina ubavu kwa Kikosi kilichopo kuweza kubeba Makombe msimu huu.
Msimu huu, Arsenal bado wapo kwenye kinyang’anyiro cha Ligi Kuu England ambako wako nafasi ya pili nyuma ya Manchester United na pia wamo Robo Fainali UEFA CHAMPIONS LIGI watakapowavaa Mabingwa Watetezi Barcelona.
Lakini Kikosi hicho cha Arsene Wenger kinakabiliwa na matatizo makubwa ya ukosefu wa Kikosi kikubwa na hasa wanapokuwepo majeruhi wengi.
Arshavin amesema: “Maoni yangu ni kuwa tunahitaji Wachezaji wengine wengi. Mwishoni mwa Msimu uliokwisha tuliuza Wachezaji wawili na kununua mmoja tu. Sasa tumewapoteza Mastaa Van Persie, Kieran Gibbs na Aaron Ramsey ambao wameumia!”
Arshavin ameendelea kudai bila ya Wachezaji wengi ni rahisi sana kwa wapinzani wao kuwasoma na kujua mbinu na mikakati yao na hivyo wanapata uwezo wa kuwakaba kirahisi na kuwashambulia.
West Ham 1 Wolves 3
Wolves wamepiga hatua kubwa ili kujinasua mkiani walipowafunga West Ham katika mechi pekee ya Ligi Kuu Jumanne usiku kwa mabao 3-1 Uwanjani Upton Park.
Mabao ya Wolves yalifungwa na Kevin Doyle, Ronald Zubar na Mathew Jarvis.
Bao pekee la West Ham lilipachikwa na Guillermo Franco.
Ushindi huo umeipandisha Wolves nafasi moja na wako nafasi ya 15 wakiwa na pointi 31 kwa mechi 31.
West Ham wamebaki nafasi ya 17 wakiwa na pointi 27 kwa mechi 31 na wako juu ya Timu za 18 na 19, Burnley na Hullm City, kwa pointi 3 tu.
Portsmouth wako nafasi ya mwisho, nafasi ya 20, na wana pointi 13 tu baada ya kunyang’anywa pointi 9 na Ligi Kuu.
Timu zitakazoshika nafasi za 18, 19 na 20 mwishoni mwa msimu ndizo hushushwa Daraja.

Tuesday 23 March 2010

Rufaa ya Vermaelen yatupwa!!
Leo FA imetupilia mbali rufaa ya Arsenal kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Beki wao Thomas Vermaelen siku ya Jumamosi kwenye mechi ya Ligi Kuu waliyowafunga West Ham 2-0 na hivyo haruhusiwi kucheza mechi ya Ligi ya Jumamosi ijayo Arsenal atakapokuwa ugenini kucheza na Birmignham.
Refa Martin Atkinson alimtoa Vermaelen alipomchezea Guillermo Franco faulo alipokuwa akienda kufunga na hivyo kufungiwa mechi moja.
Itabidi Wakongwe Sol Campbell na Mikel Silvestre wazibe mapengo ya Vermaelen na Gallas, ambae ni majeruhi, kwa mechi hiyo ya Jumamosi.
LIGI KUU Leo: West Ham v Wolves
Uwanjani Upton Park, leo usiku West Ham watawaalika wenzao Wolves katika mechi ya Ligi Kuu inayozikutanisha Timu iliyo nafasi ya 16, Wolves, na ile iliyo nafasi ya 17, West Ham, huku Wolves ana pointi 28 na West Ham wana pointi 27.
Hii ni mechi muhimu mno kwa Timu zote mbili hasa ukizingatia wao wako juu tu ya Timu 3 za mwisho, Burnley, Hull City na Portsmouth, ambazo ndizo ziko eneo la hatari la kushushwa Daraja na Timu za Burnley na Hull zina pointi 24 kila mmoja.
Arsenal wakata rufaa kupinga Kadi ya Vermaelen
Arsenal wamekata rufaa kwa FA kupinga Kadi Nyekundu aliyopewa Beki wao Thomas Vermaelen siku ya Jumamosi kwenye mechi ya Ligi Kuu waliyowafunga West Ham 2-0.
Refa Martin Atkinson alimtoa Vermaelen alipomchezea Guillermo Franco faulo alipokuwa akienda kufunga na hivyo kufungiwa mechi moja na anatakiwa aikose mechi ya Ligi ya Jumamosi inayokuja ambayo Arsenal wanasafiri kwenda kupambana na Birmingham.
Vermaelen na William Gallas ndio Masentahafu wa Arsenal msimu huu lakini Gallas amezikosa mechi kadhaa hivi karibuni baada ya kuumia na hivyo itabidi Wakongwe Sol Campbell na Mikel Silvestre wazibe mapengo ya Vermaelen na Gallas.
Rufaa hiyo ya Veermaelen inategemewa kusikilizwa leo.
Al Fayed aishambulia FIFA!!
Mmiliki wa Fulham, Mohamed Al Fayed, ameishambulia vikali FIFA kwa kukataa kutumia teknolojia ya kisasa katika Soka.
Kwa muda mrefu sasa Wadau wengi wa Soka wamekuwa wakiitaka FIFA itumie marudio ya mikanda ya video na elektroniki kwenye mistari ya magoli ili kuwasaidia Marefa kutoa uamuzi sahihi katika mechi lakini FIFA imegoma kufanya mapinduzi hayo kwa kudai utamu wa mpira unatokana na uamuzi na makosa ya Binadamu.
Al Fayed amefoka: “Nimepigia kelele hili kwa muda mrefu sasa! FIFA hawaelewi! Wao haiwaumizi, hawalipi chochote! Hawahisi chochote! Nani kawachagua? Sijui! Pengine kura za Afrika, nyingine Kathmandu [Nepal]! Kama ningekuwa na uwezo ningewafukuza wote!”
Al Fayed, Baba Mzazi wa Dodi aliefariki kwenye ajali ya gari pamoja na Princess Diana huko Paris mwaka 1997, ameapa kutayarisha mechi maalum kwenye Uwanja wa Klabu yake Fulham, Uwanja wa Craven Cottage, huku akitumia zana zote za kisasa kuwasaidia Marefa ili kuwadhihirishia FIFA na Rais wake Sepp Blatter kuwa kutumia teknolojia ya kisasa kunawezekana kabisa.
Nahodha Newcastle yuko Hospitali baada ya kupigwa mazoezini!
Nahodha wa Newcastle, Steven Taylor, amelazwa Hospitali ili kupata matibabu baada ya kuumizwa mazoezini kutokana na kupigana na Mchezaji mwenzake Andy Carroll.
Inadaiwa Taylor, ambae ndio kwanza amerudi mazoezini baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu, amevunjika taya na huenda akazikosa mechi zote za Newcastle za Ligi Daraja la Championship zilizobaki msimu huu.
Newcastle ndio vinara wa Ligi hiyo na wanategemewa kurudi tena Ligi Kuu baada ya kuporomoka msimu uliopita.
Habari za ugomvi huo hazijathibitishwa na Klabu ya Newcastle.

Monday 22 March 2010

Pompey na balaa jingine!!!
• Yashindiliwa Faini Pauni Milioni 1!!!
Wasimamizi wa LIGI KUU England wameipiga Klabu ya Portsmouth Faini ya Pauni Milioni 1 kwa kukiuka sheria na taratibu mbalimbali za Ligi Kuu zikiwemo kuchelewesha mishahara ya Wachezaji, kutokulipa Ada za Uhamisho na kadhalika.
Portsmouth ipo kwenye ukata mkubwa na imenusurika kufilisiwa baada ya kuamuliwa iwekwe chini ya Msimamizi maalum na hilo pia, ingawa ni kuiokoa Klabu isife, ni kinyume cha taratibu za Ligi Kuu na limesababisha ikatwe pointi 9.
Portsmouth wapo mkiani mwa msimamo wa Ligi Kuu na wapo hatarini kushushwa Daraja kwani wapo pointi 11 nyuma ya Timu iliyo juu yao huku wakiwa wamebakiwa na mechi 8.
Faini hiyo ya Pauni Milioni 1 inategemewa kuchukuliwa toka mapato yao ya kutoka Makampuni ya TV.
RATIBA ZA MASHINDANO YA KLABU ULAYA
UEFA CHAMPIONS LIGI
[saa za bongo]
ROBO FAINALI
Jumanne, Machi 30
[saa 3 dak 45 usiku]
Bayern Munich v Manchester United
Lyon v Bordeaux
Jumatano, Machi 31
[saa 3 dak 45 usiku]
Arsenal v Barcelona
Inter Milan v CSKA Moscow
Jumanne, Aprili 6
[saa 3 dak 45 usiku]
Barcelona v Arsenal
CSKA Moscow v Inter Milan
Jumatano, Aprili 7
[saa 3 dak 45 usiku]
Manchester United v Bayern Munich
Bordeaux v Lyon
NUSU FAINALI
Jumatano, Aprili 21
[saa 3 dak 45 usiku]
Bayern Munich/Man United v Lyon/Bordeaux
Inter Milan/CSKA Moscow v Arsenal/Barcelona
Jumatano, Aprili 28
[saa 3 dak 45]
Lyon/Bordeaux v Bayern Munich/Man United
Arsenal/Barcelona v Inter Milan/CSKA Moscow
FAINALI
Jumamosi, Mei 22
[saa 3 dak 45 usiku]
EUROPA LIGI:
ROBO FAINALI
Alhamisi, Aprili 1
[saa 4 dak 5 usiku]
Benfica v Liverpool
Fulham v Wolfsburg
Hamburg v Standard Liege
Valencia v Atletico Madrid
Alhamisi, Aprili 8
Atletico Madrid v Valencia
Liverpool v Benfica
Standard Liege v Hamburg
Wolfsburg v Fulham
NUSU FAINALI
Alhamisi, Aprili 22
Hamburg/Standard Liege v Fulham/Wolfsburg
Valencia/Atletico Madrid v Benfica/Liverpool
Alhamisi, Aprili 29
Fulham/Wolfsburg v Hamburg/Standard Liege
Benfica/Liverpool v Valencia/Atletico Madrid
FAINALI
Jumatano, Mei 12
WAFUNGAJI BORA LIGI KUU:
1. Rooney 26 [Man United]
2. Drogba 22 [Chelsea]
3. Bent 20 [Sunderland]
4. Defoe 17 [Tottenham]
5. Tevez 16 [Man City]
6. Torres 16 [Liverpool]
7. Fabregas 15 [Arsenal]
8. Saha 13 [Everton]
9. Lampard 12 [Chelsea]
10. Agbolanhor 11 [Aston Villa]
11. Berbatov 10 [Man United]
12. Adebayor 9 [Man City]
13. Arshavin 9 [Arsenal]
14. Carlton Cole 9 [West Ham]
15. Jerome 9 [Birmingham]
KWA UFUPI TU:
-Wenger kuhusu Van Persie:
Arsene Wenger ana matumaini kidogo kuwa Staa wake Robin van Persie huenda akaonekana tena uwanjani msimu huu baada ya kupata nafuu vizuri enka yake aliyofanyiwa operesheni baada ya kuumizwa Novemba mwaka jana akiichezea Nchi yake Uholanzi ilipokutana na Italia.
Wenger amesema hata akirudi tena mazoezini bado anahitaji si chini ya wiki 3 ili kuwa fiti na hiyo itamchukua hadi Mei.
Msimu wa Ligi unakwisha Mei 9.
-Allardyce na Fergie:
Sam Allardyce, Meneja wa Blackburn Rovers ambayo jana ilitoka sare 1-1 na Vigogo Chelsea, amesema sare hiyo si kwa ajili ya rafiki yake Sir Alex Ferguson wa Manchester United bali ni kwa ajili yao ili kujihakikishia usalama wao wa kutoshuka Daraja.
-Owen Hargreaves kupona:
Owen Hargreaves wa Manchester United huenda akarudi kwenye Kikosi cha kwanza mwezi ujao baada ya kucheza dakika 45 za kwanza za Kikosi cha Pili cha Man United kilichoifunga Burnley 2-0.
Sir Alex Ferguson amesema amefurahi mno kumwona Hargreaves uwanjani baada kuwa nje kwa Miezi 18 akiuguza magoti aliyofanyiwa operesheni.
-Robert Mancini:
Roberto Mancini, Meneja wa Manchester City kutoka Italia, anategemea Mchezaji wake Wayne Bridge atabadilisha uamuzi na kuichezea England baada ya kuisusa kutokana na kashfa ya John Terry kutembea na gelfrendi wake wa zamani.
Mancini anataka Bridge abadilishe uamuzi hasa kwa vile yeye anaamini sana kuwa England ina uwezo wa kunyakua Kombe la Dunia.
England ipo chini ya Mtaliana mwingine Fabio Capello ambae ameacha mlango wazi kwa Bridge kujiunga na England hasa baada ya Beki wa kutumainiwa Ashley Cole kuwa majeruhi wa muda mrefu na atakosekana kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
-Rafa alia na penalti ya Man United:
Rafa Benitez wa Liverpool amedai Refa Howard Webb hakustahili kuwapa penalti Manchester United katika ushindi wao wa bao 2-1 hapo jana kwa vile Valencia alijiangusha.
Mikanda ya Video ilionyesha wazi Kiungo wa Liverpool Mascherano akimvuta jezi Valencia ingawa kitendo hicho kilianzia nje ya boksi na kuendelea hadi ndani ya penalti.
Wayne Rooney alipiga penalti hiyo lakini Kipa Reina aliokoa na mpira kurudi tena kwa Rooney aliefunga bao la kusawazisha.
Wakati huo huo, Sir Alex Ferguson amedai Mascherano alistahili kupewa Kadi Nyekundu na si Njano kama aliyopewa kwa faulo hiyo kwa Valencia kwa vile alikuwa mtu wa mwisho na alimzuia Valencia asiende kufunga.
Chelsea walia lakini wajipa matumaini!!
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amesisitiza wao bado wana matumaini ya kuwa Mabingwa licha ya jana kupoteza pointi walipotoka suluhu na Blackburn Rovers bao 1-1 na sasa kushikilia nafasi ya 3 wakiwa na pointi 65 kwa mechi 30, Arsenal wakiwa wa pili kwa pointi 67 kwa mechi 31 na Manchester United wakiongoza wakiwa na pointi 69 kwa mechi 31.
Tangu wiki ya pili ya msimu huu kuanza, hii ni mara ya kwanza kwa Chelsea kuwa nje ya Timu mbili za juu na dalili za kupwaya kwao zipo kwenye takwimu kwani wameshinda mechi mbili tu kati ya 8 za ugenini na vilevile wamepata pointi 5 tu katika mechi zao 5 za mwisho za Ligi.
Wiki iliyokwisha Chelsea walitupwa nje ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE baada ya kufungwa na Inter Milan na matumaini yao yaliyobaki kupata Vikombe msimu huu ni kwenye Kombe la FA Ligi Kuu tu.
RATIBA LIGI KUU:[saa za bongo]

Jumanne, Machi 23
West Ham v Wolves [saa 5 usiku]
Jumatano, Machi 24

[saa 4 dak 45]
Aston Villa v Sunderland
Man City v Everton
Portsmouth v Chelsea
[saa 5 usiku]
Blackburn v Birmingham
Chelsea wakwama Ewood Park!!
• Wapo nafasi ya 3!!
Leo katika mechi ya Ligi Kuu, nia ya Chelsea kupata pointi 3 na hivyo kuikaribia Manchester United ilitupwa nje na Timu ngumu Blackburn Rovers waliokuwa nyumbani Ewood Park na kulazimisha sare ya bao 1-1.
Sare hii ya Chelsea imezinufaisha sana Manchester United na Arsenal ambazo sasa zipo juu ya Chelsea huku Man United, ambae jana alimtandika Liverpool 2-1, akiongoza Ligi kwa kuwa na pointi 69 kwa mechi 31 na wa pili ni Arsenal akiwa na pointi 67 kwa mechi 31 na Chelsea ni wa 3 akiwa na pointi 65 kwa mechi 30.
Chelsea walikuwa ndio wa kwanza kupata bao kupitia Didier Drogba baada ya pande tamu la Nicholas Anelka.
Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili El-Hadji Diouf aliisawazishia Blackburn baada ya krosi ya Michel Salgado.
Fulham 1 Man City 2
Huko Craven Cottage, Fulham wakiwa wametoka kwenye furaha ya kuitwanga Juventus 4-1 hapo juzi kwenye EUROPA LIGI, jana Jumapili wamepigwa bao 2-1 na Manchester City kwenye mechi ya LIGI KUU.
Mabao ya Man City yalifungwa na Roque Santa Cruz na Carlos Tevez.
Bao la Fulham lilifungwa kwa penalti na Danny Murphy baada ya Gareth Barry kuunawa mpira.

Sunday 21 March 2010

Man United yaikata ngebe Liverpool!!
Leo katika Uwanja wa Old Trafford Manchester United wameupiga stopu uteja kwa Liverpool na kuwatandika Mahasimu wao hao bao 2-1 na kutwaa uongozi wa Ligi Kuu kutoka kwa Arsenal walioushika tangu jana.
Sasa Man United ana pointi 69 akifuatiwa na Arsenal mwenye pointi 67 na Chelsea ni wa 3 akiwa na pointi 64 huku ana mechi mbili mkononi.
Liverpool ndio walioanza vyema mechi hii baada ya Fernando Torres kuwapa bao kwa kichwa dakika ya 5 tu baada ya krosi ya Kuyt.
Man United walisawazisha dakika ya 12 kwa bao la Wayne Rooney aliefunga baada ya penalti yake kuokolewa na Kipa Reina na mpira kumrudia Rooney ambae hakufanya kosa kwa mara ya pili.
Penalti hiyo ya Rooney ilisababishwa na Mascherano kumchezea rafu Valencia na Refa kuamuru penalti.
Hadi mapumziko mabao yalikuwa 1-1.
Ndipo kwenye dakika ya 60 Ji-Sung Park alipofunga kwa kichwa cha kudaivu baada ya krosi ya Darren Fletcher.
Vikosi vilivyoanza:
Man Utd: Van der Sar, Neville, Ferdinand, Vidic, Evra, Valencia, Fletcher, Carrick, Park, Rooney, Nani.
AKIBA: Kuszczak, Berbatov, Giggs, Scholes, Rafael Da Silva, Jonathan Evans, Obertan.
Liverpool: Reina, Johnson, Carragher, Agger, Insua, Mascherano, Lucas, Kuyt, Gerrard, Maxi, Torres.
AKIBA: Cavalieri, Aquilani, Benayoun, Kyrgiakos, Babel, Ngog, Kelly.
REFA: Howard Webb
Wenger atabiri Ubingwa baada ya kuipiga West Ham 2-0!!
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Timu yake inao ubavu na ubora wa kutwaa Ubingwa Ligi Kuu na ametamka hivyo mara tu baada ya kuwafunga vibonde West Ham bao 2-0 hapo jana huku wakicheza Mtu 10 tu baada ya Beki wao Thomas Vermaelen kulambwa Kadi Nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Arsenal iongoze Ligi kwa vile tu Chelsea na Manchester United hazikucheza Jumamosi na mechi zao zipo Jumapili.
Katika ushindi huo, mabao ya Arsenal yalifungwa na Denilson na Cesc Fabregas kwa penalti.
Wakati Vermaelen anatolewa, West Ham walipewa penalti iliyopigwa na Alessandro Diamanti na kuokolewa na Kipa wa Arsenal Manuel Almunia.
Wenger ametamba: “Tuna nafasi nzuri msimu huu!”
Kimahesabu na kitabuni, Arsenal wamesaliwa na mechi ‘mchekechea’ ukilinganisha na Wapinzani wao Chelsea na Man United ambao wana mechi kati yao wenyewe wakati Arsenal ameshamaliza mechi zote na Vigogo Chelsea, Man United na Liverpool.
BIGI MECHI: Man United v Liverpool
Jumapili, Machi 21 Uwanja: Old Trafford Saa: 10 na Nusu jioni, saa za bongo
• Liverpool imeshinda Mechi 3 mfululizo, Vidic alambwa Kadi Nyekundu Mechi zote hizo 3!!!
Timu hizi zilikutana mara ya mwisho Mwezi Oktoba mwaka jana na Liverpool walishinda 2-0 na hiyo ikiwa ni mara ya 3 mfululizo kwa Liverpool kuifunga Manchester United.
Msimu uliokwisha, Liverpool walishinda mechi zote mbili za Ligi kwa 2-1 huko Anfield na 4-1 uwanjani Old Trafford.
Katika mechi zote hizo 3 ambazo Manchester United walifungwa, Beki wao Nemanja Vidic amekuwa akitolewa kwa Kadi Nyekundu na hivyo kulainisha ushindi kwa Liverpool.
Mbali ya kuikandya FA kwa maamuzi yake yanayoikandamiza Man United hasa kwenye masuala ya nidhamu ikizingatiwa kufungiwa kwa Mchezaji wake Rio Ferdinand mechi 4 wakati Steven Gerrard na Javier Mascherano wa Liverpool hawaadhibiwi chochote kwa makosa yaliyofanana na ya Rio, Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, ametamka: “Tunajua wao Liverpool siku zote bahati huanguka kwao! Kwa hilo wanafanya vizuri! Labda siku moja bahati itakuwa yetu!”
Akizungumzia kutolewa kwa Kadi Nyekundu Beki wake Nemanja Vidic katika mechi 3 mfululizo na Liverpool ambazo Liverpool walishinda mechi zote hizo 3, Ferguson alisema: “Zile Kadi 2 Nyekundu alizopata Anfield ni sababu ya shinikizo la kelele za Mashabiki na Wachezaji wa Liverpool! Nimeziangalia tena zote! Sio sahihi hata kidogo!”
Katika mechi ya Jumapili, Liverpool wana listi ndogo ya majeruhi akiwemo Difenda Martin Skrtel pekee ingawa Albert Riera hatakuwepo kutokana na suala lake la nidhamu ndani ya Klabu.
Man United wana listi ndefu ya majeruhi wakiwemo Ritchie De Laet, Wes Brown, Rafael da Silva, Michael Owen, Anderson, John O’Shea na Owen Hargreaves.
Ryan Giggs, aliekuwa akiuguza mkono uliovunjika, huenda akacheza.
VIKOSI VINATEGEMEWA KUWA:
Manchester United (4-4-2): Van der Sar; Neville, Ferdinand, Vidic, Evra; Valencia, Carrick, Scholes, Nani; Berbatov, Rooney.
Liverpool (4-5-1): Reina; Johnson, Carragher, Agger, Insua; Maxi, Aquilani, Mascherano, Babel; Gerrard, Torres.
Refa: Howard Webb. [Amechezesha Mechi 21 Kadi Nyekundu 3 Njano 77]
TAKWIMU YA MECHI: Zimetolewa Kadi Nyekundu 6 katika Mechi 6 za mwisho za Ligi kati ya Timu hizi.
Powered By Blogger