Saturday 13 March 2010

LIGI KUU: Wikiendi hii, Chelsea awania kutwaa uongozi
Tottenham Hotspurs v Blackburn Rovers
Hii ni mechi ya kwanza kwa wikiendi hii na inchezwa mapema kupita zote.
Tottenham, walio nafasi muhimu sana ya 4 ambayo ni ya mwisho kufuzu kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI wapo nafasi hiyo wakiwa pointi sawa na Manchester City ila wamewazidi magoli, wanaikaribisha Blackburn Rovers Uwanjani White Hart Lane.
Blackburn wanaonekana wameshajinasua kutoka balaa la kushushwa Daraja lakini wana rekodi mbaya wakicheza ugenini na mechi ya mwisho kushinda ugenini ilikuwa Novemba mwaka jana.
Chelsea v West Ham
Chelsea wanawakaribisha jirani zao wa London West Ham Uwanjani Stamford Bridge na ushindi kwa Chelsea utawapa tena uongozi wa Ligi Kuu na kuwa pointi moja juu ya Manchester United.
Katika mechi ya mwisho ya Ligi, Chelsea walitandikwa na Manchester City 4-2.
Kwa West Ham, mambo ni mazito kwani wapo 3 tu juu ya Timu zile tatu za mwisho na wamefungwa mechi zao mbili za mwisho.
Burnley v Wolves
Hii ni mechi kubwa kwa Timu hizi kwani Burnley wapo nafasi ya 18, wakiwa moja ya Timu 3 zilizo nafasi ya hatari ya kushushwa Daraja, na Wolves wapo nafasi ya 17.
Burnley hawajashinda katika mechi 5 na Wolves wamefungwa mechi zao 3 za mwisho.
Hii ni mechi inayozikutanisha Timu iliyofunga magoli machache kwenye Ligi [Wolves, goli 21 katika mechi 28] na Timu iliyofungwa goli nyingi [Burnley, goli 61 katika mechi 29].
Bolton v Wigan
Ni pointi moja tu iliyo kati ya Timu hizi lakini Wigan wanaingia kwenye mechi hii wakiwa na furaha baada ya juzi kuitungua Liverpool 1-0 kwenye Ligi.
Nao Bolton wanatoka kwenye kipigo cha 4-0 walichopewa na Sunderland siku ya Jumanne kwenye Ligi Kuu.
Hull City v Arsenal
Arsenal ambao wako nafasi ya 3 wanasafiri hadi KC Stadium kucheza na Hull City ambao wako nafasi ya pili toka mwisho.
Kwa Arsenal, mechi hii ni muhimu kwani ushindi utawafanya waipite Man United ambao wanacheza Jumapili.
Stoke City v Aston Villa
Aston Villa wamecheza mechi 3 pungufu ya Timu zile zinazowania nafasi ya 4 kwa vile wamekuwa na mechi za Vikombe mbalimbali na ushindi kwao ni muhimu ili kuifukuzia nafasi hiyo ya 4.
Stoke wapo nafasi ya 11 na wamefungwa mechi moja tu mwaka huu.
Birmingham v Everton
Wakiwa kwao Uwanja wa Mtakatifu Andrew, Birmingham wanautafuta ushindi wao wa 3 mfululizo kwenye Ligi watakapocheza na Everton ambao wako pointi mbili nyuma ya Birmingham.
Manchester United v Fulham
Hii ni mechi inayochezwa Jumapili na inazikutanisha Timu ambazo mechi zao za mwisho zilikuwa ni za Ulaya wakati Man United walipoitwanga AC Milan 4-0 kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI na Fulham walipopigwa 3-1 na Juventus kwenye EUROPA LIGI.
Mechi ya mwisho ya Ligi kati ya Timu hizi, huku Man United ikiwa haina Difensi na kuwalazimu kuwachezesha Darrren Fletcher na Michael Carrick kama Masentahafu, Fulham walishinda 3-0.
Sunderland v Manchester City
Katika mechi yao ya mwisho, Sunderland waliifunga Bolton 4-0 huo ukiwa ushindi wao wa kwanza katika mechi 15 na kuwainua kuwa pointi 6 mbele ya zile Timu 3 za mkiani.
Man City wao wapo lile kundi linalogombea nafasi ya 4 na wamecheza mechi moja pungufu ya Timu ya 4 Tottenham huku wakiwa na pointi sawa.
Mechi ya mwisho, Man City walipata ushindi wa kishindo walipoichapa Chelsea 4-2 huko Stamford Bridge.

Friday 12 March 2010

EUROPA LIGI: Liverpool, Fulham zapigwa ugenini!!
Klabu za England, Liverpool na Fulham, jana zilipoteza mechi zao za kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za ugenini.
Liverpool ilifungwa 1-0 na Lille huko Ufaransa na Fulham ilitwangwa 3-1 na Juventus huko Italia.
Bao lililoiua Liverpool lilifungwa dakika ya 85 na Mchezaji wa Lille Eden Hazard.
Huko Italia, Juventus ilifunga bao zake 3 kipindi cha kwanza kupitia Nicola Legrottaglie, Jonathan Zebina na David Trezeguet.
Bao la Fulham lilifungwa na Dickson Etuhu.
Timu hizo zitarudiana wiki ijayo Machi 18.
Matokeo kamili:
Atletico Madrid 0 v Sporting Lisbon 0
Benfica 1 v Marseille 1
Hamburg 3 v Anderlecht 1
Juventus 3 v Fulham 1
Lille 1 v Liverpool 0
Panathinaikos 1 v Standard Liege 3
Rubin Kazan 1 v Wolfsburg 1
Valencia 1 v Werder Bremen 1
DROGBA NI BORA AFRIKA
Mchezaji kutoka Ivory Coast na anaechezea Klabu ya Chelsea, Didier Drogba, miaka 32, amechukua Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika na kuwapiku Michael Essien na Samuel Et’oo.
Drogba aliwahi kuchukua Tuzo hii mwaka 2006.
Algeria ilishinda Tuzo ya Timu Bora Afrika.
Magazeti Italia yalia: “NI FEDHEHA!”
Kufuatia vipigo vya nje ndani, 3-2 wakiwa kwao San Siro na 4-0 ndani ya Old Trafford , Magazeti ya Italia yameweka Mabango makubwa yakilalamika kuhusu kipigo cha 4-0 cha Jumatano cha AC Milan mikononi mwa Manchester United kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI huko Old Trafford.
Gazeti moja kubwa lilitamka: “Hapo zamani za kale, ilikuwepo Milan!” wakimaanisha enzi za AC Milan waliponyakua Ubingwa wa Ulaya mara 7.
Jingine lilisema: “Milan yaadhiriwa! Somo toka kwa Rooney! Si kushindwa ni kipondo!”
Gazeti moja liliandika kuwa kufungwa na Manchester United kunakubalika lakini jinsi walivyopigwa 4-0 bila ya Timu kuonyesha uchungu wowote ndilo linauma sana.
LIGI KUU England: RATIBA WIKIENDI HII:
[saa za bongo]
Jumamosi, Machi 13
[saa 9 dak 45 mchana]
Tottenham v Blackburn
[saa 12 jioni]
Birmingham v Everton
Bolton v wigan
Burnley v Wolves
Chelsea v West Ham
Stoke v Aston Villa
[saa 2 na nusu usiku]
Hull v Arsenal
Jumapili, Machi 14
[saa 10 na nusu jioni]
Man United v Fulham
[saa 1 usiku]
Sunderland v Man City
Jumatatu, Machi 15
[saa 5 usiku]
Liverpool v Portsmouth
Jumanne, Machi 16
[saa 4 dak 45 usiku]
Wigan v Aston Villa

Thursday 11 March 2010

LEO EUROPA LIGI: Liverpool wapo Ufaransa, Fulham ni Italia!
Timu za England, Liverpool na Fulham, leo zipo ugenini kwenye mechi za kwanza za EUROPA LIGI ambayo marudio yake ni wiki ijayo.
Hii ni hatua ya Mtoano ya Timu 16 na Liverpool wako Ufaransa kucheza na Lille wakati Fulham wako Italia kupambana na vigogo wa huko Juventus.
Mechi nyingine yenye mvuto ni ile ya majirani wa Spain na Ureno kati ya Atletico Madrid v Sporting Lisbon.
RATIBA:
Atletico Madrid v Sporting Lisbon
Benfica v Marseille
Hamburg v Anderlecht
Juventus v Fulham
Lille v Liverpool
Panathinaikos v Standard Liege
Rubin Kazan v Wolfsburg
Valencia v Werder Bremen
Fergie ampa changamoto Rooney
• Beckham, Kocha AC Milan wakiri Rooney ni bora duniani!
• Beckham akana kuwa nae ni Kijani na Dhahabu!!
Sir Alex Ferguson amemtaka Wayne Rooney aivunje rekodi aliyoweka Cristiano Ronaldo ya kufunga goli 42 kwa msimu aliyoiweka mwaka 2007-08.
Mpaka sasa Rooney ana jumla ya mabao 30 lakini mwenyewe amesema yeye hajaweka lengo lolote ila anachotaka ni magoli tu.
Rooney akizungumza baada ya jana kuipiga AC Milan bao 4-0 huku bao mbili zikifungwa na yeye, alisema: “Ni matokeo mazuri kwetu! “
Nae David Beckham, aliewahi kuichezea Manchester United na kisha kuhamia Real Madrid na baadae LA Galaxy na sasa yuko kwa mkopo AC Milan, alikiri Rooney ni kiboko kwa kusema: “Bila shaka, yeye ni kipaji na ni bora duniani pamoja na Ronaldo na Messi!
Na Kocha wa AC Milan Leonardo amekubali Timu yake ilizidiwa kila kitu na Manchester United na kusema Man United walicheza kandanda la hali ya juu.
Wakati huo huo David Beckham amekanusha kuwa na yeye anawapinga Wamiliki wa Manchester United Familia ya Glazer baada ya kuonekana mwishoni mwa mechi hiyo ya Manchester United v AC Milan akivaa skafu ya Kijani na Dhahabu aliyorushiwa na shabiki mmoja anaeunga mkono upinzani dhidi ya kina Glazer.
Rangi hizo za Kijani na Dhahabu ni rangi za Klabu anzilishi ya Man United, Newton Heath, na zimechukuliwa kama ishara ya upinzani.
Beckham amesema: “Mimi ni Shabiki wa Manchester United. Nilirushiwa ile skafu nikaivaa shingoni. Hizo ni rangi za zamani za Man United. Mimi naisapoti Klabu.”
UEFA CHAMPIONS LIGI: Real waikosa Fainali kwao, watoswa na Lyon!
Man United 4 AC Milan 0
Wayne Rooney alichomeka bao 2, Park na Fletcher wakapiga moja moja na kuishindilia AC Milan misumari minne na kuiingiza Manchester United Robo Fainali lakini kilio kikubwa kilitokea Uwanja wa Bernabeau baada ya Real Madrid kutolewa nje ya UEFA CHAMPIONS LIGI huku Mei 22 Fainali ikitakiwa ichezwa Uwanja huo huo wa Bernabeau.
Alikuwa Mchezaji wa zamani wa Manchester United Cristiano Ronaldo aliewapa matumaini Real alipofunga goli dakika ya 5 na kufanya Timu hizo zifungane kwa bao 1-1 kwani Lyon walishinda 1-0 mechi ya kwanza.
Alieleta msiba mkubwa Hispania ni Miralem Pjanic aliposawazisha dakika ya 75 na hivyo kuipa Lyon ushindi wa jumla ya bao 2-1.
Mbali ya kutegemea kucheza Fainali Uwanja wa nyumbani hii ni mara ya 6 mfululizo Real Madrid wanabwagwa nje ya Mashindano haya kwenye hatua hii na hili ni pigo kubwa sana kwa Klabu iliyonunua Masupastaa kwa bei mbovu.

Wednesday 10 March 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Leo ni kimbembe Old Trafford na huko Bernabeau!!
• Ni Man U v AC Milan na Real v Lyon
Baada ya Manchester United kuishindilia AC Milan 3-2 wakiwa kwao San Siro na Real Madrid kupigwa kimoja na Lyon huko Ufaransa, leo ni mechi za marudiano na leo Real wako kwao Uwanja wa Bernabeau kuikaribisha Lyon na Man United wako nyumbani Old Trafford.
Kwa Real Madrid, licha ya kuwa kwao, hii ni mechi muhimu mno sana hasa kwa vile Fainali ya Kombe hili la UEFA CHAMPIONS LIGI msimu huu itachezwa hapo hapo Bernabeau mwezi Mei na hivyo kila Mshabiki wao anajua kuwa wanawajibika kuweko kwenye Fainali hiyo na ni lazima leo waifunge Lyon ili ndoto yao kucheza Fainali hiyo Bernabeau ikamilike.
Huko Old Trafford, kwa Mashabiki wa Manchester United ni kumwona tena kipenzi chao cha zamani lakini safari hii ni ‘adui’ na huyo ni David Beckham akiwa na Timu yake ya mkopo AC Milan.
Ili waibwage Manchester United, AC Milan lazima waifunge bao 2-0 au upatikane ushindi bora zaidi ya ule wa Man United wa 3-2 ukizingatia magoli ya ugenini.
Kwa ufupi, mechi za leo ni kimbembe!!
UEFA CHAMPIONS LIGI: Arsenal, Bayern zatinga Robo Fainali!!
• Arsenal 5 FC Porto 0
• Fiorentina 3 Bayern Munich 2

Mabao matatu ya Niklas Bendtner na moja moja la Nasri na Eboue yameiangamiza FC Porto kwa bao 5-0 na hivyo kuupindua ushindi wa FC Porto wa bao 2-1 katika mechi ya kwanza na kuipeleka Arsenal Robo Fainali kwa jumla ya bao 6-2.
Mabao ya Arsenal yalifungwa dakika ya 10 na ya 25 na Bendtner.

Kipindi cha pili Nasri alifunga bao ya dakika 63 na Eboue dakika ya 66 na Bendtner akamalizia kwa penalti dakika ya 90.
Huko Italia, licha ya Bayern Munich kupigwa 3-2 na Fiorentina imetinga Robo Fainali kwa mabao ya ugenini.
Bayern Munich ilishinda mechi ya kwanza 2-1 na hivyo kuyafanya jumla ya magoli baada ya mechi mbili kuwa 4-4 na hivyo sheria ya goli la ugenini kutumika.
UEFA CHAMPIONS LIGI: Mechi za marudiano
RATIBA:
Jumatano, 10 Machi 2010
Man United v AC Milan
Real Madrid v Lyon
MATOKEO MECHI ZA KWANZA:

AC Milan 2 v Man United 3
Lyon 1 v Real Madrid 0

Tuesday 9 March 2010

England yanaswa kwenye mkanda wa siri!!
Zimeibuka habari kuwa kuna mkanda wa siri umenaswa ukiwa na rekodi ya mazungumzo kati ya Makocha wa England na Wachezaji wao wakiwa hotelini kabla ya mechi ya kirafiki na Misri Jumatano iliyopita.
Mkanda huo uliorekodiwa haujulikana kama ulinaswa kupitia simu au vinasa sauti na umekuwa ukipelekwa kwa Vyombo vingi vya Habari ili ununuliwe.
Lakini Wanasheria wa Timu ya England wamevionya kuwa kuutumia mkanda huo uliorekodiwa kinyume cha sheria ni makosa.
England hivi karibuni iligubikwa na kashfa iliyomhusu John Terry ambae ilimfanya avuliwe Unahodha wa England.
Gerrard huenda akalikwaa rungu la FA!!
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, huenda akajikuta yuko matatani na FA baada ya kunaswa kwenye video akimtukana Refa Andre Marriner na pia kutoa ishara ya V katika mechi ya jana Liverpool waliyofungwa 1-0 na Wigan.
Vitendo hivyo vya Gerrard vilitokea dakika ya 81 baada ya kulambwa Kadi ya Njano na Refa Marriner alipomkwatua kwa nyuma Mchezaji wa Wigan James McCarthy.
Refa Marriner hakuviona vitendo vya Gerrard lakini FA huenda wakaamua kumshitaki Gerrard kwa uhuni.
Rooney afanya mazoezi
Supastaa Straika wa Manchester United Wayne Rooney ameipa nguvu Timu yake baada ya kuonekana akifanya mazoezi na wenzake kwenye Kambi ya mazoezi ya Carrington na huenda akacheza kesho kwenye mechi ya marudiano na AC Milan ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Man United iliifunga AC Milan 3-2 huko San Sirro.
Rooney aliikosa mechi ya Ligi Kuu ya Jumamosi Man United walipoifunga Wolves 1-0 na ilitangazwa ana matatizo ya goti.
Katika mazoezi hayo ya huko Carrington ambacho ndicho kituo cha mazoezi cha Manchester United, Veterani Ryan Giggs alionekana pia akifanya mazoezi.
Giggs alivunjika mkono kwenye mechi ya Ligi Kuu na Aston Villa mwezi uliokwisha.
UEFA CHAMPIONS LIGI: Mechi za marudiano
RATIBA:
Jumanne, 9 Machi 2010
Arsenal v FC Porto
Fiorentina v Bayern Munich
Jumatano, 10 Machi 2010
Man United v AC Milan
Real Madrid v Lyon
Jumanne, 16 Machi 2010
Chelsea v Inter Milan
Sevilla v CSKA Moscow
Jumatano, 17 Machi 2010
Barcelona v VfB Stuttgart
Bordeaux v Olympiakos
MATOKEO MECHI ZA KWANZA:
AC Milan 2 v Man United 3
Lyon 1 v Real Madrid 0
Bayern Munich 2 v Fiorentina 1
FC Porto 2 v Arsenal 1
Olympiakos 0 v Bordeaux 1
VfB Stuttgart 1 v Barcelona 1
CSKA Moscow 1 v Sevilla 1
Inter Milan 2 v Chelsea 1
TATHMINI:
Arsenal v FC Porto
Cesc Fabregas, Nahodha wa Arsenal, ataikosa mechi muhimu ya marudiano na FC Porto ambayo Arsenal wanatakiwa washinde 1-0 ili wasonge mbele, kwa vile ni majeruhi.
Katika mechi ya kwanza, FC Porto ilishinda 2-1.
Mbali ya kumkosa Fabregas, Arsenal pia itamkosa Difenda William Gallas lakini
nafasi ya Gallas inategemewa kuzibwa na Sol Campbell na akikosekana yupo Mikel Sylvestre.
Nao FC Porto wamesema wao hawatui Uwanja wa Emirates ili kucheza kwa kujihami kulinda ushindi wao wa mechi ya kwanza wa 2-1 bali watashambulia tu kama staili yao ilivyo kila siku.
Chapombe Adriano!!
Mkurugenzi wa Klabu ya Flamengo Marcos Braz amesema Adriano amekumbwa na matatizo binafsi na ameanza tena kunywa pombe kwa wingi na mfululizo.
Braz amelalama: “Akianza kunywa, haachi! Alilishinda tatizo hili lakini limerudi tena kwa sababu ya presha ya matatizo binafsi!”
Braz amezipinga habari za Magazeti ya Brazil kuwa Adriano anatumia madawa ya kulevya.
Mwaka jana Adriano aliikimbia Inter Milan na kurudi kwao Brazil akidai kuwa hana furaha na ni mpweke huko Italia.
Adriano yupo kwenye Kikosi cha Brazil na anategemewa pia kuwemo kwenye Kikosi hicho kwa Fainali za Kombe la Dunia.
Ameshaichezea Brazil mara 48 na kufunga magoli 27.
LIGI KUU: Liverpool yakong’otwa!
Kwenye mechi pekee ya Ligi Kuu hapo jana, Wigan imeifunga Liverpool bao 1-0 Uwanjani DW na hivyo kuitia kiwewe cha kuikosa nafasi ya 4 itakayowawezesha kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI msimu ujao.
Bao la ushindi la Wigan lilifungwa dakika ya 35 na Mshambuliaji Hugo Rodallega.
Baada ya mechi, Kocha wa Liverpool Rafa Benitez aliwalaumu Wachezaji wake kwa kutocheza vizuri na kupoteza pasi nyingi. Lawama hizo pia zilimlenga Straika wake Dirk Kuyt kwa kufanya kosa lililozaa goli lililowakata ngebe Liverpool.
Katika msimamo wa ligi, Liverpool wapo nafasi ya 6 wakiwa wamecheza mechi 29 na wana pointi 48 na mbele yao wapo Tottenham na Manchester City wote wakiwa na pointi 49 lakini Man City wamecheza mechi moja pungufu.
Nyuma ya Liverpool wapo Aston Villa waliocheza mechi 26 tu na wana pointi 45.

Monday 8 March 2010

FIFA yaipiga buti teknolojia!!!
Dunia ya Soka itaendelea kuutegemea uamuzi wa Binadamu pekee ili kuamua kama mpira umevuka mstari wa goli au la na hivyo ni goli au siyo badala ya kutegemea teknolojia ya kisasa inayotumia mikanda ya video na elktroniki nyingine kutoa uamuzi wa papo kwa papo na sahihi.
Bodi ya Kimataifa ya Vyama vya Soka [IFAB=International Football Association Board] imepiga kura na kutupilia mbali mapendekezo mawili ambayo yangeondoa kumtegemea Refa tu kutoa uamuzi katika hali za utatanishi kwenye mechi.
Jerome Valcke, Katibu Mkuu wa FIFA, ametamka: “Huu ni mwisho wa kufikiria kutumia teknolojia!”
FIFA imekuwa kwenye shinikizo kubwa la kukubali kutumia teknolojia ya kisasa ili kuondoa makosa makubwa yanayofanywa na Marefa katika mechi kubwa.
Dunia itakumbuka hivi majuzi Republic of Ireland ilivyopokwa kuingia Fainali za Kombe la Dunia pale Thierry Henry wa Ufaransa alipokontroli mpira kwa mkono bila Refa kuona na kumpasia William Gallas alieisawazishia Ufaransa bao na kuiingiza Fainali za Kombe la Dunia.
Valcke amesema uamuzi wa kumwongezea mamlaka Refa wa Akiba [Refa wa nne] ambae huwepo pembeni kwenye kila mechi na pia kuwepo kwa Marefa wengine wasaidizi wawili mmoja nyuma ya kila goli, utafanywa kwenye Kikao maalum cha IFAB mwezi Mei.
IFAB ilianzishwa mwaka 1886 na ndio inayojulikana kama “Mlinzi wa Sheria za Soka” na Wanachama wake ni Vyama vya Soka vya England, Scotland, Wales na Ireland ya Kaskazini na kila mmoja huwa ana kura moja.
FIFA, katika mikutano ya IFAB, ina kura 4 na ni lazima zipatikane asilimia 75 ya kura zote ili uamuzi kufikiwa.
Nchi za England, Scotland, Wales na Ireland ya Kaskazini ndizo zinazotambulika kama kiini cha kuanzishwa Soka duniani.
Nae Jonathan Ford, Kiongozi wa FA ya Wales, amesema utata kwenye Soka ndio unafanya Soka kuvutia na hivyo kuanzisha mijadala na malumbano kuhusu matukio mbalimbali yenye utata kwenye mechi ni sehemu ya Soka inayovutia na kuchangamsha.
Ford amesema: “Makosa ya Marefa ni ya kibinadamu! Na hilo huchangamsha Soka na kuwafanya watu wawe na cha kuzungumza kwenye Mabaa miaka nenda rudi!”
FA CUP: Nusu Fainali yapangwa!
Droo ya Nusu Fainali ya Kombe la FA imefanyika na Mabingwa Watetezi wa Kombe hilo Chelsea wamepangwa kucheza na Aston Villa.
Katika Robo Fainali, Chelsea waliitoa Stoke City 2-0 na Aston Villa waliibwaga Reading 4-2.
Mechi nyingine ya Nusu Fainali ni mshindi kati ya Tottenham na Fulham, waliotoka sare 0-0 juzi na watarudiana Machi 24, kukutana na Portsmouth ambao ndio walikuwa Mabingwa mwaka 2008.
Portsmouth waliifunga Birmingham 2-0 kwenye Robo Fainali.
Mechi za Nusu Fainali zitachezwa Uwanja wa Wembley Jijini London kwenye wikiendi ya Aprili 10 na 11.

Sunday 7 March 2010

LIGI KUU: Everton 5 Hull 1
Everton wakiwa nyumbani Goodison Park wameishindilia Hull City bao 5-1 na hivyo kuzidi kuingiza kwenye balaa Hull ambayo inaelea mkiani kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Mabao ya Everton yalifungwa na Mikel Arteta bao mbili, Leighton Barnes na Landon Donovan bao moja moja na moja Hull City walijifunga wenyewe baada ya mpira kumbabatiza Richard Garcia.
FA CUP: Chelsea 2 Stoke City 0
Frank Lampard na John Terry wameifungia Chelsea bao moja kila mmoja na kuifikisha Timu yao Nusu Fainali ya Kombe la FA na hivyo kuungana na Portsmouth na Aston Villa.
Timu ya 4 itakayoingia Nusu Fainali ni ama Tottenham au Fulham ambazo jana zilitoka 0-0 na zitarudiana White Hart Lane Machi 24.
KWA UFUPI TU:
Allardyce ampaka Rafa!
Bosi wa Blackburn Sam Allardyce amejibu mapigo kwa Bosi wa
Liverpool Rafa Benitez katika vita yao ya maneno iliyoanza muda mrefu na kupamba moto baada ya Liverpool kuifunga Blackburn bao 2-1 kwenye mechi ya Ligi Kuu wikiendi iliyokwisha.
Tangu Benitez atue England mwaka 2004 amekuwa hana uhusiano mzuri na Allardyce na kila Timu zinazoongozwa na Mameneja hao zikikutana malumbano makali hutokea kati yao.
Mara baada ya mechi ya wikiendi iliyopita, Benitez alidai Blackburn walikuwa wakitumia miguvu na pasi ndefu tu.
Allardyce amejibu: “Yeye anajua Timu yake ilicheza mpira mbovu na ni bahati tu walishinda! Anajaribu kunilaumu mimi ili akwepe lawama za ubovu wa Liverpool!”
Kuszczak: “Nipeni namba au naondoka!”
Kipa wa akiba wa Manchester United Tomasz Kuszczak ambae yuko msimu wake wa nne Klabuni hapo ametaka awe anapewa namba au ataondoka mwishoni mwa msimu huu.
Kuszczak, miaka 27, ni Kipa nambari mbili nyuma ya Edwin van der Sar, miaka39, ambae ameongeza mkataba wake na Manchester United hadi mwishoni mwa msimu wa 2011.
FA CUP: Vila iko Nusu Fainali
Aston Villa leo wakiwa ugenini wamefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la FA licha ya kuwa bao 2-0 hadi haftaimu lakini walibadilika kipindi cha pili na kufunga bao 4 na hivyo kuwabwaga Reading 4-2.
Alikuwa ni John Carew aliekuwa shujaa baada ya kuifungia Villa bao 3.
Bao jingine la Villa lilipachikwa na Ashley Young.
England si wazuri kuchukua Kombe la Dunia
Mkongwe wa England, Geoff Hurst, aliefunga goli 3 mguuni kwake katika Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1966 dhidi ya Ujerumani na kuipa England Kombe hilo kwa ushindi wa bao 4-2, amedai Kikosi cha sasa cha England si kizuri kiasi cha kuwa na uwezo wa kuwa Mabingwa wa Dunia.
Hurst amedai Timu hiyo ina kasoro nyingi zikiwemo za kukosa Mafowadi wazuri ukimtoa Wayne Rooney na kukosa Difensi imara baada ya kuumia Mafulbeki Glen Johnson na Ashley Cole pamoja na kuwa na wasiwasi wa kumkosa Rio Ferdinand anaeandamwa na kuumia mara kwa mara.
Hurst amesema England itafika Nusu Fainali tu kwa Kikosi chao kilichopo na kama ingekuwa Fernando Torres anachezea England pamoja na Rooney alikuwa ana uhakika Timu hiyo ingekuwa kiboko.
Tangu itwae Kombe la Dunia mwaka 1966, England imefika Nusu Fainali ya Kombe hilo mwaka 1990 na kutolewa Robo Fainali mwaka 2002 na 2006.
FIFA: Uhamisho Wachezaji Duniani kudhibitiwa
FIFA imesema itaanzisha njia mpya ya kudhibiti uhamisho wa Kimataifa wa Wachezaji ili kuondoa kasoro nyingi zikiwemo zile za Wachezaji kumilikiwa na Kampuni badala ya Klabu wanazochezea na ununuzi wa Wachezaji hao unaohusishwa kuhodhi pesa kinyume cha sheria.
Utaratibu mpya wa FIFA utatumia njia za elektroniki na unaitwa ‘Transfer Matching System’ [TMS] na hivyo kuondoa utaratibu wa sasa wa kutumia faksi na makaratasi ili kuhamisha Wachezaji na hivyo kuondoa dosari nyingi.
Meneja Mkuu wa TMS, Mark Goddard, amesema: “Mpaka sasa mtindo uliokuwa ukitumiwa ni wa makaratasi kama ilivyokuwa miaka 100 nyuma! Ilikuwa ngumu kufuatilia Wachezaji gani wamehamishwa. Kulikuwa na uhamisho feki, kulikuwa na uuzwaji wa Wachezaji ambao hawapo ili mradi Watu mafisadi wahamishe pesa zao toka Nchi moja hadi nyingine kinyume cha sheria!”
Katika mfumo wa TMS uanaotumia mtandao, ili kukamilisha uhamisho wa Mchezaji inabidi Klabu zinazouza na kununua Mchezaji ziingize kwenye mtandao taarifa zote zinazotakiwa kuhusiana na Mchezaji anaehamishwa zikiwemo ada ya uhamisho, mshahara wa Mchezaji huyo, Wakala wake au Mwanasheria wake na muda wa mkataba wake.
Pia, ada ya uhamisho ni lazima itoke Benki moja kwenda nyingine.
Goddard amesema: “Huu ni mradi mkubwa wa FIFA. Haujabadilisha sheria za uhamisho bali unadhibiti uhamisho na kuondoa kasoro na dosari nyingi.”
Moja ya kasoro hizo ni ile ya Wachezaji kumilikiwa na ‘Watu baki” badala ya Klabu. Mtindo huo ni kitu cha kawaida huko Marekani ya Kusini ambako baadhi ya Wachezaji humilikiwa na Makampuni, Mawakala na hata Mifuko ya Pensheni.
Mfano maarufu ni umiliki wa Mchezaji Carlos Tevez aliechukuliwa na West Ham kutoka Corinthians lakini ikabainika baadae kuwa Corinthians haikuwa ikimmiliki.
West Ham ilipigwa faini ya Pauni Milioni 5.5 Aprili 2007 kwa kukiuka sheria za Ligi Kuu zinazokataza Mchezaji kumilikiwa na Kampuni binafsi badala ya Klabu.
Vilevile, mtindo huu wa TMS utaondoa kesi za madai zinazohusiana na kutolipwa au kutokamilishwa ada ya uhamisho wa Mchezaji kwa vile vitu vyote vitakuwa wazi mtandaoni.
Goddard ameongeza kuwa mtindo huo mpya unarahisisha mno uhamisho wa Mchezaji na akatoa mfano wa Mchezaji mmoja aliehama Klabu moja kutoka England na kwenda Scotland na uhamisho wote ikiwemo kupata kibali cha Kimataifa vilichukua dakika 7 tu na Mchezaji huyo akafanikiwa kuichezea Klabu yake mpya siku hiyo hiyo.
Owen nje msimu wote, Hargreaves kurudi dimbani!!
Mshambuliaji wa Manchester United Michael Owen hatacheza tena msimu huu baada ya kuumia musuli za mguu katika Fainali ya Kombe la Carling walipoifunga Aston Villa 2-1.
Owen, miaka 30, ndie aliifungia Man United bao la kwanza katika Fainali hiyo na ikabidi atoke Kipindi cha Kwanza baada ya kuumia.
Sasa imefahamika maumivu hayo yatalazimika kufanyiwa opersheni na hilo litamweka nje hadi msimu unakwisha.
Nae majeruhi wa muda mrefu Owen Hargreaves ataonekana uwanjani siku ya Alhamisi akicheza mechi ya Timu ya Pili ya Manchester United itakapopambana na Kikosi cha pili cha Manchester City.
Hargreaves hajacheza tangu Septemba 2008 na alifanyiwa operesheni kwenye magoti yake mawili huko Marekani.
LA LIGA: Real watwaa uongozi!!
Baada ya Barcelona kutoka sare ya 2-2 na Almeria hapo jana, Real Madrid waliokuwa nyuma kwa bao 2-0 walipocheza na Sevilla, waliibuka na kupata ushindi wa mabao 3-2 na hivyo kutwaa uongozi wa La Liga.
Sevilla walipata bao la kwanza baada ya Xabi Alonso kujifunga mwenyewe na Dragutinovic kufunga la pili kwa frikiki.
Lakini Real wakajitutumua na kufunga kupitia Ronaldo, Ramos na Van de Vaart na hivyo kufungana pointi 62 na Barcelona lakini Real wana magoli bora.
Goli la 100 la Scholes laipaisha Man United kileleni!!
• Wolves 0 Man United 1
• Arsenal 3 Burnley 1
• West Ham 1 Bolton 2
Kiungo Veterani Paul Scholes jana alifunga goli lake la 100 katika mechi za Ligi Kuu na kuifanya Manchester United iongoze Ligi walipopata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Wolves Uwanjani Molineux.
Bao hilo la Scholes lilifungwa dakika ya 73 na kuifanya Man United iwe na pointi 63, Chelsea na Arsenal zina pointi 61 kila mmoja lakini Chelsea ana tofauti ya magoli bora.
Hata hivyo Chelsea wikiendi hii hawana mechi ya Ligi Kuu kwani wanacheza Robo Fainali ya FA Cup leo na Stoke.
Jana Manchester United ilicheza bila ya mtambo wao wa magoli Wayne Rooney aliepumzishwa kwa vile anasumbuliwa na maumivu ya goti.
Awali Arsenal waliifunga Burnley bao 3-1 uwanjani Emirates na kuwafanya bado wawe tishio kwenye Ubingwa wa Ligi Kuu.
Arsenal ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 11 kupitia Fabregas.
Kipindi cha pili, dakika ya 50, David Nugent alisawazisha kwa Burnley baada ya kumvika kanzu Kipa Manuel Almunia.
Winga Theo Walcott alipachika bao la pili kwa Arsenal na Mchezaji alieingia toka benchi Andrey Arshavin akaweka bao la 3 dakika za majeruhi.
Katika mechi nyingine ya Ligi Kuu, Bolton iliweza kujinasua kidogo toka chini baada ya kupata ushindi wa ugenini walipoifunga West Ham bao 2-1.
Bolton walicheza dakika 18 za mwisho wakiwa mtu 10 baada ya Kiungo wao Tamir Cohen kupewa Kadi 2 za Njano na hivyo kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Bolton walipata bao la kwanza dakika ya 11 mfungaji akiwa Kevin Davies na bao la pili lilifungwa na Jack Wilshere, ambae yupo Bolton kwa mkopo kutoka Arsenal.
FA CUP: Fulham 0 Tottenham 0
Katika mechi ya Kombe la FA ya Robo Fainali huko Craven Cottage, Fulham na Tottenham zilitoka sare ya kutofungana na itabidi zirudiane huko White Hart Lane ili kupata Timu moja itakayoenda Nusu Fainali.
Leo kuna mechi mbili za Robo Fainali kati ya Chelsea v Stoke na Reading v Aston Villa.
Powered By Blogger