Saturday 2 January 2010

KOMBE LA FA: Hakuna Timu ya Ligi Kuu iliyotolewa nishai na Timu za Madaraja ya chini!!!
Timu za Ligi Kuu leo zimepeta na kuingia Raundi ya 4 ya Kombe la FA baada ya kuzitoa Timu za Madaraja ya chini ispokuwa mechi za Portsmouth v Coventry na Nottingham Forest v Birmingham itabidi zirudiwe baada ya kumalizika suluhu.
Mechi ya Stoke City v York bado inaendelea kwa sababu ilichelewa kuanza na Stoke mpaka sasa yuko mbele bao 3-1.
Mechi ya Reading v Liverpool inaanza saa 2 na robo saa za bongo.
MATOKEO KAMILI: Jumamosi, 2 Januari 2010
Accrington v Gillingham [Imeahirishwa]
Aston Villa 3 v Blackburn 1
Blackpool 1 v Ipswich 2
Bolton 4 v Lincoln City 0
Brentford v Doncaster [Imeahirishwa]
Bristol City v Cardiff [Imeahirishwa]
Everton 3 v Carlisle 1
Fulham 1 v Swindon 0
Huddersfield 0 v West Brom 2
Leicester 2 v Swansea 1
MK Dons 1 v Burnsley 2
Middlesbrough 0 v Man City 1
Millwall 1v Derby 1
Nottingham Forest 0 v Birmingham 0
Plymouth 0 v Newcastle 0
Portsmouth 1 v Coventry 1
Preston 7 v Colchester 0
Reading v Liverpool [MECHI ITAANZA saa 2 na robo saa za bongo]
Scunthorpe 1v Barnsley 0
Sheffield Wednesday 1 v Crystal Palace 2
Southampton 1 v Luton 0
Stoke 3 v York 1 [MECHI INAENDELEA ILICHELEWA KUANZA]
Sunderland 3 v Barrow 0
Torquay 0 v Brighton 1
Tottenham 3 v Peterborough 0
Wigan 3 v Hull 1
RATIBA MECHI ZA Jumapili, 3 JanuarI 2010
Chelsea v Watford
Man U v Leeds United
Notts County v Forest Green
Sheffield United v QPR
Tranmere v Wolves
West Ham v Arsenal
KOMBE LA FA: Mechi 3 zaahirishwa kutokana na hali ya hewa mbaya!!!
Mechi 3 za Raundi ya 3 ya Kombe la FA zilizokuwa zichezwe leo zimeahirishwa kutokana na hali mbaya ya hewa inayofuatia baridi kali na kuganda barafu kwa Viwanja.
Mechi hizo sasa zimepangwa kuchezwa Januari 12.
Mechi zilizoahirishwa ni:
Accrington v Gillingham
Brentford v Doncaster
Bristol City v Cardiff
KOMBE LA FA: Man Utd v Leeds inakumbusha uhasama wa enzi!!!
Kihistoria Manchester United ikipambana na Leeds United ni mechi ya uhasama kwa Wachezaji wa pande hizo mbili pamoja na Mashabiki wa Timu hizo zinazotoka Miji ya Manchester na Leeds inayotenganishwa na Maili 40 tu.
Chimbuko la uhasama huo ni Vita ya Mawaridi iliyopiganwa Karne ya 15 lakini kimpira uhasama huu ulikuzwa miaka ya 1970 wakati Leeds United walikuwa na Genge la Mashabiki waliojiita Kruu wa Kazi [Service Crew] na Manchester United Genge lao liliitwa Jeshi Jekundu [Red Army].
Kwa miaka ya hivi karibuni uhasama huu umepungua kwa vile Leeds United wameporomoka kutoka Lig Kuu toka mwaka 2004waliposhushwa Daraja na Timu hizi hazijakutana tangu wakati huo.
Kwa sasa Leeds United wako Daraja la Ligi 1 ambalo ni Madaraja mawili chini ya Ligi Kuu, yaani baada ya Ligi Kuu lipo Daraja la Championship na kisha Ligi 1.
Leeds United kwa sasa ndio wanaoongoza msimamo wa Ligi 1.
Lakini kesho, saa 10 jioni saa za bongo, Leeds United watatua Old Trafford kuvaana na Manchester United kwenye Raundi ya 3 ya Kombe la FA, na uhasama unategemewa kuchomoza tena.
Kwa tahadhari, Polisi wa Jijini Manchester wameshawaomba Wamiliki wa Baa na Grosari kupunguza uuzaji wa pombe kabla ya mechi hiyo na pia kutowauzia pombe watu wanaoonekana tayari wako nyingi.
Pia Polisi imetoa onyo kuwa hakuna Shabiki atakaeruhusiwa kuingia Uwanjani ikiwa kalewa na mbali ya kuzuiwa upo uwezekano wa kupelekwa lupango.
Nae Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, amewatahadharisha Wachezaji wake kuepuka vitendo vinavyoweza kuchochea vurugu.
Ferguson ametamka: “Haina haja ya kukumbushia nini maana ya mechi na Leeds! Mechi hizo zimekuwa na uhasama wa kihistoria na ni lazima Wachezaji wa pande zote mbili wajichunge ili wasilipue vurugu! Leeds wanaleta Mashabiki wao 8,000 Old Trafford na itakuwa ni siku ya kazi ya ziada kwa Polisi!”
Ferguson alikumbushia uhasama uliokuwepo na kukumbusha jinsi alivyotaka kushambuliwa na Mashabiki wa Leeds wakati akitoka kutazama mechi Uwanja wa Leeds uitwao Elland Road na akiwa kwenye gari lake, wakati amesimama kwenye taa nyekundu, kundi la Mashabiki wa Leeds walimtambua na kupiga kelele: “Ferguson!’ na kuanza kumkimbilia lakini, bahati nzuri, sekunde hiyo hiyo, taa zikageuka njano, na yeye akapiga msele na kutoka nduki!
Wenger kubadili Timu FA Cup
Bosi wa Arsenal Arsene Wenger amesema atabadili Kikosi chake kitakachocheza na West Ham kwenye Kombe la FA hapo kesho na kuwapumzisha Mastaa wake kwa ajili ya mechi zijazo za Ligi Kuu dhidi ya Bolton Jumatano ijayo na Everton wikiendi ijayo.
Wenger ametamka: “Baadhi ya Wachezaji watapumzika. Tunataka kushinda lakini kwetu Ligi Kuu ni muhimu kuliko FA Cup!”
Arsenal haijatwaa Kikombe chochote tangu mwaka 2005.
Mbrazil Jo asimamishwa Everton kwa kwenda kula Xmas kwao!!!
Everton imemsimamisha kwa muda usiojulikana Mshambuliaji Jo kutoka Brazil ambae yuko hapo kwa mkopo akitokea Manchester City kwa sababu aliondoka Klabuni bila ruhusa na kwenda kula Sikukuu ya Xmas kwao Brazil.
Meneja wa Everton David Moyes amesema: “Tunampenda Jo lakini Klabu ina taratibu zake. Aliondoka bila ruhusa. Tumemsimamisha!”
Jo, miaka 22, ambae jina lake kamili ni Joao Alves de Assis Silva, alinunuliwa na Man City kutoka CSKA Moscow Julai 2008 kwa Pauni Milioni 18 lakini akakosa namba na ndipo akakopeshwa kwa Everton ambako nako pia mara nyingi huwekwa benchi la akiba.

Friday 1 January 2010

LIGI KUU England:TAKWIMU ZA FUNGA MWAKA
MSIMAMO LIGI KUU England: [Timu zimecheza mechi 20 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 45
2 Man Utd pointi 43
3 Arsenal pointi 41 [mechi 19]
4 Tottenham pointi 37
5 Man City pointi 35 [mechi 19]
6 Aston Villa pointi 35
7 Liverpool pointi 33
8 Birmingham pointi 32
9 Fulham pointi 27 [mechi 19]
10 Sunderland pointi 23
11 Everton pointi 22 [mechi 19]
12 Stoke City pointi 21 [mechi 19]
13 Blackburn pointi 21
14 Burnley pointi 20
15 Wolves pointi 19
16 Wigan pointi 19 [mechi 19]
17 West Ham pointi 18
18 Bolton pointi 18 [mechi 18]
19 Hull pointi 20 [mechi 18]
20 Portsmouth pointi 14
WAFUNGAJI BORA:
1 Jermaine Defoe [Spurs] 14
2 Didier Drogba [Chelsea]14
3 Wayne Rooney [Man U]14
4 Darren Bent [Sunderland]13
5 Fernando Torres [Liverpool] 12
6 Louis Saha [Everton] 10
7 Cesc Fabregas [Arsenal] 9
8 Carlos Tevez [Man City] 9
9 Gabriel Agbonlahor [Villa] 8
10 Carlton Cole [West Ham] 7
KADI NYEKUNDU NYINGI:
Javier Mascherano [Liverpool] 2
Wachezaji Pompey waingiwa hofu kuhusu Mishahara yao!!!
Mlinzi wa Portsmouth Steve Finnan ametoboa kuwa Wachezaji wa Timu hiyo wameingiwa na hofu kubwa kuhusu hali ya kifedha ya Klabu hiyo ambayo, kwa mara ya 3 sasa, wameshindwa kulipa Mishahara kwa wakati na safari hii wameahidiwa kulipwa siku ya Jumanne mara baada ya Sikukuu ya Mwaka mpya.
Portsmouth, ambao wako mkiani kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, pia wametakiwa kufilisiwa na Mamlaka ya Kodi ya Mapato kwa kuwa wana deni la kodi la Pauni Milioni 60.
Finnan amesema: “Wachezaji wana wasiwasi na si jambo zuri kwa Mashabiki!! Tuliwasikia juzi kwenye mechi na Arsenal wakiimba kulalamikia hali yetu!!”
Kesho Portsmouth wanacheza na Coventry kwenye Mtoano wa Raundi ya Tatu ya Kombe la FA na Finnan amewaahidi Washabiki kuwa wakiingia uwanjani matatizo yao yote watayaweka kando na kucheza kufa kupona.
McCarthy: Wakati wa kuondoka umefika!!!
Benni McCarthy, miaka 32, kutoka Afrika Kusini anaechezea Klabu ya Blackburn Rovers amekiri kuwa sasa umefika wakati wa yeye kutafuta Timu nyingine ili apate namba ya kudumu ili aweze kuchaguliwa kwenye Kikosi cha Bafana Bafana kitakachokuwa Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia mwezi Juni.
McCarthy ameanza mechi 6 tu Msimu huu wa Ligi hapo Blackburn.
McCarthy amesema: “Ningependa kubaki England, ni Ligi bora! Sina furaha na hali ya sasa, nataka nicheze kila mara ili nichukuliwe Bafana Bafana!”
McCarthy alijiunga na Blackburn mwaka 2006 akitokea FC Porto ya Ureno na amefunga goli 52 katika mechi 136 alizoichezea Blackburn.
Song aimba: Hakuna mtu anaweza kuifunga Arsenal!!!!
Kiungo kutoka Cameroun Alex Song anaechezea Arsenal ametamba kuwa hakuna Timu inayoweza kuifunga Arsenal.
Arsenal wako pointi 4 nyuma ya vinara wa Ligi Chelsea lakini wana mechi moja mkononi na wataicheza mechi hiyo Jumatano ijayo kwa kupambana na Bolton Wanderers.
Song ametamba: “Tukicheza kama tulivyoifunga Portsmouth 4-1 hapo juzi, hakuna mtu anaeweza kutufunga!!”
Portsmouth ndio Timu iliyo ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Song anategemewa kesho kucheza katika mechi ya Kombe la FA dhidi ya West Ham na kisha kusafiri ili kujiunga na Timu ya Taifa ya Cameroun inayojitayarisha kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazoanza Januari 10 huko Angola.
KWA WADAU WOTE:
TUNAWATAKIA KILA LA KHERI, FANAKA NA KILA KITU KWA MWAKA 2010!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
MUNGU AWABARIKI!
Amina.
===stormingfohadi
Ancelotti ambatiza Wenger “Mchawi mzuri”!!
Carlo Ancelotti amejibu mapigo kwa Arsene Wenger, ambae hapo juzi alidai Chelsea itaanguka kadri Msimu wa Ligi unavyoendelea, kwa kumbatiza “Mchawi mzuri”!
Uongozi wa Chelsea kwenye Ligi kuu mwezi Desemba ulipunguzwa kwa pointi 9 huku Arsenal wakishinda mechi 3 mfululizo, na, baada ya kuifunga Portsmouth 4-1 huko Fratton Park siku ya Jumatano, Arsene Wenger alitangaza kuwa Chelsea watapoteza pointi na kuporomoka chini kadri Msimu unavyoendelea na pia Ancelotti atatimuliwa Chelsea ifikapo mwishoni mwa Msimu.
Ancelotti aliicheka kauli ya Wenger na kutamka: “Kama alisema hayo basi yeye ni ‘mchawi mzuri”!”
Ancelotti akaongeza: “Tulikuwa na matatizo mwezi Desemba na hatukushinda na tulitoka sare na Everton, Birmingham na West Ham lakini hilo ni kawaida! Kila Timu ina kipindi chake kigumu!”
Hata hivyo, mpaka sasa mwaka 2010 ukianza, Chelsea ndio wanaongoza Ligi wakiwa na pointi 45, Manchester United ni wa pili na wana pointi 43 na Arsenal ni wa 3 wakiwa na pointi 41 huku wamecheza mechi moja pungufu.
Jumatano ijayo Arsenal watacheza na Bolton ikiwa ndio mechi yao pungufu.
Wakati huohuo, Meneja huyo wa Chelsea amesema hatishiki na uvumi mkubwa kuwa Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho, atarudishwa tena Chelsea kuchukua nafasi yake na Ancelotti amesema: “Itabidi asubiri kwani mie ndie Meneja wa Chelsea na ntabaki hapa! Yeye ni Meneja wa Inter Milan hivyo si mpinzani wangu!”
Baada ya kipigo cha 4-1, Pompey hawana Mishahara!!!
Mara baada ya kutandikwa bao 4-1 na Arsenal kwenye Ligi Kuu Uwanjani kwao Fratton Park mbele ya Mashabiki wao waliokuwa wakiimba ‘Fukuza Bodi” na “Pesa zetu ziko wapi?’, sasa Wachezaji wa Portsmouth watakosa Mishahara yao ya Desemba hii ikiwa ni mara ya 3 kwa Timu hiyo kukosa kulipwa Mishahara yao kwa wakati.
Portsmouth pia wameshindiliwa msumari wa moto pale Mamlaka ya Kodi ya Mapato kutaka Klabu hiyo ifilisiwe kwa kushindwa kulipa Kodi inayokadiriwa kuwa ni Pauni Milioni 60.
Portsmouth pia imefungiwa na FA kutosajili Mchezaji yeyote hadi itakapolipa madeni ya kutokukamilisha malipo ya ununuzi wa Wachezaji.
Portsmouth ndio Klabu ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi Kuu na hivi karibuni ilimtimua Meneja wake na kumteua Avram Grant kushika nafasi hiyo.
Klabu ya Portsmouth imetoa taarifa kuwapoza Wadau wake kuwa itawalipa Wachezaji na Wafanyakazi wake ifikapo Januari 5 na uchelewesho huo umetokana tu na matatizo ya kiutawala na sio fedha.
Pia, wamesisitiza kuwa Mmiliki wa Klabu hiyo, Ali al-Faraj kutoka Saudi Arabia, sasa anaandaa mfumo mpya wa utawala wa kifedha ili kufuta matatizo ya uendeshaji.

Thursday 31 December 2009

MECHI YA LIGI KUU ENGLAND JANA YAWEKA HISTORIA: Hakuna hata Mchezaji mmoja wa England aliecheza!!!
  • Waingereza waja juu!!!!
Meneja wa Blackburn Rovers Sam Allardyce ameitabiria Timu ya Taifa ya England kuwa katika hali ngumu hapo baadae baada ya mechi ya Ligi Kuu hapo jana kati ya Portsmouth na Arsenal kuweka historia ya kuwa mechi ya kwanza kabisa katika Ligi hiyo kuchezwa huku hamna hata Mchezaji mmoja Raia wa England aliecheza.
Allardyce alisema: “Kwa Timu ya Taifa, hilo linasikitisha sana! Ligi Kuu na FA lazima walitazame hilo!”
Rais wa FIFA Sepp Blatter amekuwa akipiga kampeni ya kuanzisha Sheria inayoitwa “6 jumlisha 5”, ikimaanisha Timu lazima ziwe na Wachezaji watano Raia wa Nchi yenye Ligi yake au waliolelewa na Klabu za Nchi hiyo katika mechi moja lakini hilo limekuwa likipingana na Sheria za Haki na Uhuru wa Binadamu zilizowekwa na Jumuia ya Nchi za Ulaya.
Katika mechi hiyo iliyochezwa jana Jumatano Desemba 30 ambayo Arsenal iliifunga Portsmouth 4-1, Wachezaji 22 walioanza mechi hiyo walikuwa wanatoka Nchi 15 [hamna hata mmoja toka England] huku Ufaransa ikitoa Wachezaji 7.
Kulikuwa na Wachezaji wawili kutoka Algeria, na mmoja mmoja kutoka Bosnia, Ireland, Israel, Iceland, Afrika Kusini, Scotland, Ujerumani, Spain, Belgium, Wales, Cameroun, Croatia na Urusi.
Katika Wachezaji wa Akiba kulikuwa na wanne kutoka England na wawili kati yao, Craig Esmond wa Arsenal aliingizwa badala ya Mfaransa Samir Nasri, na, Portsmouth wakamuingiza Michael Brown badala ya Richard Hughes kutoka Scotland.
Historia hiyo iliwekwa hapo jana ikiwa ni miaka 10 baada ya Chelsea kuweka historia ya kuichezesha Timu bila Mchezaji hata mmoja toka England katika mechi yao na Southampton iliyochezwa Desemba 26, 1999.
Meneja wa Sunderland Steve Bruce aliunga mkono katika kuponda hali hiyo lakini alisema: “Hatutoi Wachezaji wazuri Chipukizi na ndio maana tunahaha dunia nzima kusaka Wachezaji wenye vipaji! Kila Meneja wa Klabu za England angependa kuwa na Wachezaji wa England lakini hamna vipaji!”
Nae Nahodha wa zamani wa Manchester United, Roy Keane, ambae ni Raia wa Ireland na kwa sasa ni Meneja wa Ipswich Town, alisema: “Hilo, pengine, litamuumiza kichwa Fabio Capello, Meneja wa England lakini kwangu halinikoseshi usingizi!!!”
KOMBE LA FA: Ni wikiendi ya FA, Ligi Kuu ni likizo!!!
Wikiendi hii ni mechi za Raundi ya Tatu ya Mitoano ya Kombe la FA tu na Timu za Ligi Kuu zimeingizwa rasmi na kupangiwa mechi kwenye Kombe hilo.
Timu nyingi za Ligi Kuu zinapambana na Timu za Madaraja ya chini lakini kuna baadhi ya mechi zinazozikutanisha Timu za Ligi Kuu zenyewe kama vile mechi ya Aston Villa v Blackburn, Wigan v Hull na West Ham v Arsenal.
Hivyo, wikiendi hii hamna mechi za Ligi Kuu ila Jumanne ijayo itakuwepo mechi moja ya Stoke v Fulham na Jumatano pia itakuwepo moja ya Arsenal v Bolton.
Wikiendi ya Januari 9 mechi za Ligi Kuu zitachezwa kama kawaida.
RATIBA: MECHI ZA FA CUP RAUNDI YA TATU
Jumamosi, 2 Januari 2010 [saa za bongo]
[saa 9 na nusu mchana]
Bristol City v Cardiff
[saa 12 jioni]
Accrington v Gillingham
Aston Villa v Blackburn
Blackpool v Ipswich
Bolton v Lincoln City
Brentford v Doncaster
Everton v Carlisle
Fulham v Swindon
Huddersfield v West Brom
Leicester v Swansea
MK Dons v Burnsley
Middlesbrough v Man City
Millwall v Derby
Nottingham Forest v Birmingham
Plymouth v Newcastle
Portsmouth v Coventry
Preston v Colchester
Scunthorpe v Barnsley
Sheffield Wednesday v Crystal Palace
Southampton v Luton
Stoke v York
Sunderland v Barrow
Torquay v Brighton
Tottenham v Peterborough
Wigan v Hull
[saa 2 na robo usiku]
Reading v Liverpool
Jumapili, 3 JanuarI 2010
[saa 10 jioni]
Man U v Leeds United
[saa 12 jioni]
Chelsea v Watford
Notts County v Forest Green
Sheffield United v QPR
[saa 1 na robo usiku]
West Ham v Arsenal
[saa 2 na robo usiku]
Tranmere v Wolves
Tembo kutua Bongo Jumamosi
Timu ya Taifa ya Cote D’ivoire, maarufu kama Tembo, watatua Dar es Salaam Jumamosi ili kupiga kambi ya mazoezi kwa matayarisho ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazoanza kuchezwa huko Angola Januari 10.
Tembo watacheza na Timu ya Taifa ya Bongo, Taifa Stars, Uwanja wa Taifa Jumatatu usiku.
Kikosi hicho cha Ivory Coast kitawasili kikiwa na Watu 50.
Viingilio kwenye mechi hiyo ni kuanzia Shilingi 50,000/= hadi 5,000/=.
Tembo hao watakuwa na Mastaa wao kina Didier Drogba, Solomon Kalou, Yaya Toure, Aruna Dindane, Habib Kolo Toure na wengineo.
USHINDI WA 5-0 KWA WIGAN: Fergie aisifia Timu yake:
• Timu yote ilicheza murua!
• Rooney alikuwa kiboko!
Sir Alex Ferguson amesema alikuwa kwenye Xmas mbaya baada ya kufungwa mechi mbili dhidi ya Fulham 3-0 na Villa 1-0 lakini, baada ya kuikung’uta Wigan 5-0 hapo jana, yuko tayari kusherehekea bethdei yake akitimiza miaka 68 leo na pia mkesha wa Mwaka mpya.
Meneja huyo wa Manchester United anaamini Timu yake iko kwenye nafasi nzuri kuiandama Chelsea inayoongoza Ligi kwa vile tu wako pointi mbili nyuma yao.
Ferguson akizungumzia mechi ya jana alisema: “Wachezaji walijua ni lazima kufunga magoli kwani mwishoni mwa Ligi nani anajua pengine tofauti ya magoli itakuwa muhimu!”
Kero kubwa kwa Wigan hapo jana ilikuwa ni Winga wa Man U Antonio Valencia ambae Man U walimnunua kutoka Wigan mwanzoni mwa Msimu huu kwa Pauni Milioni 16. Valencia alifunga bao moja na kutengeneza matatu hapo jana.
Ferguson amesema: “Kwetu, muhimu ni kuwa Valencia alifunga goli moja na hilo ni goli lake la 6. Atafunga mengine zaidi msimu huu!!”
Kuhusu Rooney, ambae alifunga bao lake la 14 katika mechi 19 za Ligi, Ferguson amemsifu na kumwita ni kiboko.
Akizungumzia mechi ijayo ya Jumapili watakapocheza na Leeds United kwenye Kombe la FA, Ferguson amesema Kikosi tofauti kitacheza kikiwa na Chipukizi huku akidokeza Nahodha wake Gary Neville yuko fiti, Jonny Evans sasa yuko mazoezini na Ro Ferdinand tayari ameanza mazoezi.
Man United 5 Wigan 0
Manchester United, wakiwa nyumbani Old Trafford, wameibamiza Wigan mabao 5-0 katika mechi ya Ligi Kuu England na kujichimbia nafasi ya pili kwenye Ligi hiyo wakiwa na pointi 43 kwa mechi 20 huku vinara Chelsea wakiwa na pointi 45 kwa mechi 20.
Katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa Ligi, Man U waliibamiza Wigan 5-0 Uwanja wa DW, nyumbani kwa Wigan, na mabao yote kwenye mechi hiyo yalifungwa kipindi cha pili.
Lakini katika mechi ya leo, hadi mapumziko Man U walikuwa mbele kwa mabao 3-0 Wafungaji wakiwa Wayne Rooney, dakika ya 28, Carrick, dakika ya 31 na Rafael dakika ya 44.
Kipindi cha pili Berbatov akapiga bao la 4 dakika ya 49 na Valencia akapachika la 5 dakika ya 74.
VIKOSI:
Man Utd: Kuszczak, Rafael Da Silva, Brown, Vidic, Evra, Valencia, Carrick, Fletcher, Park, Berbatov, Rooney.
AKIBA: Amos, Neville, Owen, Anderson, Welbeck, Fabio Da Silva, Obertan.
Wigan: Kirkland, Melchiot, Boyce, Bramble, Figueroa, Gomez, Thomas, Cho, Scharner, N'Zogbia, Rodallega.
AKIBA: Pollitt, Edman, Amaya, Scotland, Koumas, Sinclair, McCarthy.
REFA: Lee Mason
Portsmouth 1 Arsenal 4
Timu iliyo mkiani kwenye Ligi Kuu, Portsmouth, leo uwanjani kwao Fratton Park wamezidi kupigiliwa misumari huko chini baada ya kupata kichapo cha mabao 4-1 toka kwa Arsenal kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Kwa ushindi huu, Arsenal wamefikisha pointi 41 kwa mechi 19 na wako nafasi ya 3 wakiwa nyuma ya Man U walio nafasi ya pili wakiwa na pointi 43 kwa mechi 20.
Hadi mapumziko Arsenal ilikuwa mbele kwa bao 2 Wafungaji wakiwa Eduardo, dakika ya 27 na Nasri dakika ya 42.
Kipindi cha pili Arsenal wakaongeza bao 2 kupitia Ramsey na Song.
Bao la Portsmouth lilifungwa na Nadir Belhadj.
VIKOSI:
Portsmouth: Begovic, Finnan, Kaboul, Ben-Haim, Hreidarsson, Yebda, Mokoena, Hughes, Belhadj, Boateng, Piquionne.
AKIBA: Ashdown, Diop, Brown, Utaka, Vanden Borre, Kanu, Wilson.
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Traore, Ramsey, Song Billong, Diaby, Nasri, Eduardo, Arshavin.
AKIBA: Fabianski, Rosicky, Vela, Silvestre, Wilshere, Merida, Eastmond.

Wednesday 30 December 2009

Meneja Bolton apigwa Shoka!!
Bolton Wanderers imethibitisha kuwa Meneja wao Gary Megson amefukuzwa kazi.
Megson alichukua Umeneja hapo Bolton Oktoba 2007 na katika msimu wake wa kwanza aliinusuru Klabu hiyo kushushwa Daraja na msimu uliokwisha aliinyanyua Timu na kumaliza nafasi ya 13 kwenye Ligi.
Lakini msimu huu, Timu hiyo imekuwa ikiyumba na katika mechi ya jana, wakiwa nyumbani, waliupoteza uongozi wa bao 2-0 na kuwaruhusu Hull City kupata sare ya 2-2.
Kimsimamo, Bolton wako nafasi ya 18 na wana pointi 18 kwenye Ligi ikiwa ni nafasi ya kushushwa Daraja ingawa wamecheza mechi chache (mechi 18) ukilinganisha na Timu nyingi zilizocheza mechi 20.
Wadau wengi wa Bolton wamekuwa hawampendi Megson na hata jana mara baada ya mechi na Hull kumalizika mwenyewe Megson alikiri Mashabiki wa Bolton hawamtaki.
Bolton imetangaza kuwa Timu itasimamiwa na Meneja Msaidizi Chris Evans ambae atasaidiwa na Kocha wa Timu ya Kwanza Steve Wegley.
Fergie: Ubingwa ni mbio za mtu 2!!!
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson anategemea kinyang’anyiro cha Ubingwa wa Ligi Kuu ni kupiganiwa na Timu mbili tu ambazo ni Man U na Chelsea huku Timu nyingine zinazoweka ngumu wakati huu kupukutika kadri Ligi inavyosonga mbele.
Ferguson amesema: “Kwa sasa haionekani hivyo lakini historia inatuambia ni Timu mbili tu ndizo zitakuwa wababe wa kugombea taji!! Chelsea ni hatari kubwa kwa sababu wana uzoefu mkubwa!”
Ferguson alitamka mwanzoni mwa msimu kuwa Chelsea ndie atakuwa mshindani wao mkubwa, na, licha ya upinzani mkubwa unaoonyeshwa na Timu mbalimbali kwa sasa, Ferguson bado anaamini Chelsea ndio tishio.
Ferguson amesisitiza: “Mwanzoni mwa msimu niliwaona Chelsea ndio tishio kubwa na bado sijabadili mawazo!”
Ukichukulia majeruhi yaliyowakumba Manchester United, na sasa Kipa Edwin van der Sar kwenda likizo ya muda usiojulikana kumuuguza mkewe ambae ni mgojwa sana, Man U kuwa nyuma ya vinara Chelsea kwa pointi chache kwenye Ligi ni kitu kinachowatia imani kubwa Wadau wa Mabingwa hao Watetezi.
Vilevile, kuweza kufunga mabao 40 katika mechi 19 za Ligi ni kitu cha mvuto hasa ukizingatia pengo la Mfungaji wao bora msimu uliopita, Cristiano Ronaldo, alietimkia Real Madrid.
Ferguson ametamka: “Watu wamechukulia kumpoteza Ronaldo kama pigo kubwa! Wamehisi hatuwezi kuwa wazuri kama alivyokuwepo! Ronaldo ni Mchezaji Bora sana! Lakini sisi tumebadilika na ukweli ni kuwa msimu uliokwisha baada ya mechi 19 tulikuwa na pointi 41, msimu huu kwa mechi 19 tuna pointi 40!!”
Kigoli cha ‘babu’ chaipa ushindi Liverpool, Bolton v Hull ngoma ngumu!!!
Kigoli cha dakika za majeruhi, dakika ya 93, lilolifumaniwa na Fernando Torres limewapa ushindi Liverpool wa bao 1-0 huko Villa Park dhidi ya Wenyeji Aston Villa ambao hiki ni kipigo chao cha pili mfululizo kwenye Ligi Kuu baada ya kudundwa 3-0 na Arsenal mechi iliyopita.
Kwa ushindi huo, Liverpool sasa imeipiku Birmingham na kuchukua nafasi ya 7 kwenye msimamo wa Ligi.
Katika mechi nyingine ya Ligi Kuu iliyochezwa jana, Bolton na Hull City zilitoka sare 2-2.
Hull City walikuwa nyuma 2-0 kwa mabao ya Ivan Klasnic dakika ya 20 na dakika ya 61 Kevin Davies alifunga kwa kichwa bao la pili lakini mabao mawili ya Stephen Hunt yaliiwezesha Hull kupata droo.
MECHI ZA LIGI LEO: Jumatano, 30 Desemba 2009
[saa za bongo]
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v Arsenal
[saa 5 usiku]
Man U v Wigan

Tuesday 29 December 2009

LEO NI:
• Aston Villa v Liverpool
• Bolton v Hull City
Leo usiku kutakuwa na mechi mbili za Ligi Kuu England kati ya Aston Villa v Liverpool na nyingine ni Bolton v Hull.
Kwa Mashabiki wengi mechi yenye mvuto zaidi ni ile kati ya Villa v Liverpool itakayochezwa Villa Park kwa sababu tu Villa Msimu huu imechachamaa kuwania kumaliza Ligi ikiwa kwenye Timu Bora nne ili wafuzu kucheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE Msimu ujao na Liverpool awali iliota kutwaa Ubingwa Msimu huu lakini baada ya mwendo mbovu, ikiwemo kufungwa mechi 7 za Ligi na sare nyingi, sasa wako nafasi ya 8 kwenye Ligi na, bila shaka, wanaombea tu kumaliza wakiwa kwenye Timu Bora nne.
Villa katika mechi yake ya mwisho ilitandikwa mabao 3-0 na Arsenal Uwanjani Emirates na leo itashuka kwao ikitaka kufuta matokeo hayo mabaya.
Liverpool walishinda mechi yao ya mwisho kwa bao 2-0 dhidi ya Wolves walipokuwa nyumbani Anfield.
Katika mechi ya leo, Villa watamkosa Winga wao machachari Ashley Young ambae ana adhabu ya kufungiwa mechi moja baada ya kupata jumla ya Kadi 5 za Njano.
Liverpool watamkosa Kiungo wao mahiri kutoka Argentina Javier Mascherano ambae ana adhabu ya kufungiwa mechi.
Refa katika mechi hiyo ni Peter Walton.
Van der Sar kapewa likizo, Nani kuuzwa?
Edwin van der Sar amepewa likizo ya dharura na Manchester United baada ya mkewe kuugua ghafla huko kwao Uholanzi na inasemekana hali yake si nzuri.
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amemruhusu Van der Sar kumuuguza mkewe hadi hali yake itakapotengamaa.
Van der Sar hajaichezea Man U tangu November 21 walipoifunga Everton 3-0 kwenye Ligi Kuu alipoumia goti.
Inategemewa Makipa Tomasz Kuszczak au Ben Foster ndio watakaokaa golini kwenye mechi ya kesho ya Ligi Kuu na Wigan huko Old Trafford.
Lakini katika siku za hivi kribuni Tomasz Kuszczak ndio amekuwa akidaka kila mechi.
Wakati huohuo, kuna uvumi mkubwa kuwa huenda Winga wa Man U Nani akatimkia Spain au Italy mwezi Januari dirisha la uhamisho likifunguliwa na inasemekana pia huenda akarudi kwao Ureno na kuchezea Benfica ili Man U wamchukue Nyota Chipukizi toka Argentina Angel di Maria toka Klabu hiyo.
Wakala wa Nani, Jorge Mendez, amedokeza kuwa yupo mbioni kushughulikia suala la Nani.
Kuwafunga “Vibonde” wawili, Mancini aota Ubingwa Man City!!
Roberto Mancini, Meneja mpya wa Manchester City, ambaye alianza himaya yake kwa kuwafunga ‘Vibonde’ Stoke City 2-0 Desemba 26 na kisha jana kuibwaga Wolves 3-0, ameanza majigambo na kudai Timu yake ni nzuri sana kuliko alivyofikiria mwanzo na wana uwezo wa kutwaa Ubingwa wa England.
Awali, alipoingia tu Man City wiki moja iliyopita, Mancini alitangaza lengo lake ni kumaliza miongoni mwa Timu Bora nne Msimu huu na kisha kutwaa Ubingwa Msimu ujao.
Mancini ametamba: “Tumebakiza mechi 19 za Ligi na uwezo tunao wa kuwa Mabingwa! Tuna Timu nzuri!”
Mancini aliongeza kwa kusema wiki yake ya kwanza hapo Man City imekuwa nzuri ingawa ana listi ya majeruhi kibao wakiwemo Wachezaji kina Stephen Ireland, Roque Santa Cruz, Joleon Lescott, Wayne Bridge, Shaun Wright-Phillips na Nedum Onuoha.
Vilevile, atawakosa Kolo Toure na Emmanuel Adebayor kwa mwezi Januari watakaposafiri kwenda kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola.
LIGI KUU England: Chelsea kileleni!!!
• Goli la kujifunga wenyewe laipa ushindi Chelsea!!!
• Man City ushindi wa pili kwa Mancini!!!!
Kwenye mechi za jana za Ligi Kuu, Chelsea wakiwa ngomeni kwao Stamford Bridge walikuwa nyuma kwa bao 1-0 hadi mapumziko lakini kipindi cha pili wakapata mabao mawili moja likiwa la kujifunga wenyewe na kuilaza Timu ngumu Fulham 2-1.
Fulham walipata bao lao kupitia Gera dakika ya 4 na Drogba akaisawzishia Chelsea dakika ya 73.
Lakini dakika ya 75, Chris Smalling wa Fulham akajifunga mwenyewe na kuipa Chelsea ushindi wasiostahili.
Kwa ushindi huo, Chelsea wako mbele kwenye Ligi wakiwa na pointi 45 kwa mechi 20 wakifuatiwa na Manchester United, wanaocheza kesho na Wigan, wakiwa na pointi 40 kwa mechi 19. Timu ya 3 ni Arsenal, pia wanacheza kesho na ugenini na Portsmouth, na wana pointi 38 kwa mechi 18.
Nao Manchester City, wakicheza mechi yao ya pili chini ya Meneja mpya Roberto Mancini, wameshinda mechi yao ya pili baada ya kuikung’uta Wolves 3-0 ugenini.
Mabao ya Man City yalifungwa na Tevez, dakika ya 33 na 86, na Garrido dakika ya 69.
Tottenham Hotspurs, baada ya kuwafunga West Ham 2-0, sasa wameikwaa nafasi ya 4 kwenye Ligi wakiwa na pointi 37 kwa mechi 20.
MSIMAMO kileleni mwa LIGI KUU England: [Timu zimecheza mechi 20 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 45
2 Man Utd pointi 40 [mechi 19]
3 Arsenal pointi 38 [mechi 18]
4 Tottenham pointi 37
5 Aston Villa pointi 35 [mechi 19]
6 Man City pointi 35 [mechi 19]
7 Birmingham pointi 32
8 Liverpool pointi 30 [mechi 19]
9 Fulham pointi 27 [mechi 19]
10 Sunderland pointi 23
MECHI ZA LIGI KUU LEO: Jumanne, 29 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Hull

Monday 28 December 2009

MATOKEO ZA LIGI KUU England: Jumatatu, 28 Desemba 2009
Tottenham 2 v West Ham 0
Blackburn 2 v Sunderland 2
Chelsea 2 v Fulham 1
Everton 2 v Burnley 0
Stoke 0 v Birmingham 1
MECHI INAYOFUATA [saa 4 dak 45 usiku saa za bongo]
Wolves v Man City
MECHI ZA LIGI KUU ZIJAZO:
[saa za bongo]
Jumanne, 29 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Hull
Jumatano, 30 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v Arsenal
[saa 5 usiku]
Man U v Wigan
MECHI MFULULIZO ENGLAND!!
Wiki yote hii kutakuwa na uhondo mfululizo wa mechi za Ligi Kuu England kisha Jumamosi tarehe 2 Januari 2010 Timu za Ligi Kuu England zitajimwaga kwa mara ya kwanza ndani ya viwanja mbalimbali kugombea Kombe la FA hiyo ikiwa ni Raundi ya 3 ya Kombe hilo maarufu.
Hivyo, kwa sababu ya Kombe hilo la FA, wikiendi ijayo kutakuwa hamna mapambano ya Ligi Kuu na mechi za Ligi zitachezwa Jumanne tarehe 5 Januari na Jumatano tarehe 6 Januari na kisha kuendelea kama kawaida wikiendi ya tarehe 9 Januari.
Vilevile, Jumanne Januari 5 kutakuwa na mechi ya Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Carling kati ya Blackburn na Aston Villa na Jumatano Januari 6 ni Nusu Fainali ya pili ya Kombe la Carling kati ya Mahasimu Manchester City na Manchester United.
Mechi hizo za Nusu Fainali za Kombe la Carling zinachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na marudiano yake ni Januari 19 na 20.
Ratiba kamili kuanzia kesho ni:
Jumanne, 29 Decemba 2009
LIGI KUU England
Aston Villa v Liverpool
Bolton v Hull
Jumatano, 30 Decemba 2009
LIGI KUU England
Man Utd v Wigan
Portsmouth v Arsenal
Jumamosi, 2 Januari 2010
KOMBE LA FA
Accrington Stanley v Gillingham
Aston Villa v Blackburn
Blackpool v Ipswich
Bolton v Lincoln City
Brentford v Doncaster
Bristol City v Cardiff
Everton v Carlisle
Fulham v Swindon
Huddersfield v West Brom
Leicester v Swansea
Middlesbrough v Man City
Millwall v Derby
MK Dons v Burnley
Nottm Forest v Birmingham
Plymouth v Newcastle
Portsmouth v Coventry
Preston v Colchester
Reading v Liverpool
Scunthorpe v Barnsley
Sheff Wed v Crystal Palace
Southampton v Luton
Stoke v York
Sunderland v Barrow
Torquay v Brighton
Tottenham v Peterborough
Wigan v Hull
Jumanne, 5 Januari 2010
KOMBE LA CARLING, NUSU FAINALI, MECHI YA KWANZA
Blackburn v Aston Villa
LIGI KUU England
Stoke v Fulham
Jumatano, 6 Januari 2010
KOMBE LA CARLING, NUSU FAINALI, MECHI YA KWANZA
Man City v Man U
LIGI KUU England
Arsenal v Bolton
Jumamosi, 9 Januari 2010
LIGI KUU England
Arsenal v Everton
Birmingham v Man U
Burnley v Stoke
Fulham v Portsmouth
Hull v Chelsea
Sunderland v Bolton
Wigan vAston Villa
Jumapili, 10 Januari 2010
LIGI KUU England
Liverpool v Tottenham
West Ham v Wolves
Jumatatu, 11 Januari 2010
LIGI KUU England
Man City v Blackburn
Tottenham 2 West Ham 0
Kwenye mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa leo White Hart Lane nyumbani kwa Tottenham Hotspurs na kumalizika punde tu, wenyeji walimudu kuifunga West Ham mabao 2-0 na kujikita nafasi ya 4 kwenye msimamo wa Ligi huku wakiwa na pointi 37.
Luka Modric ambae hajaichezea Tottenham tangu mwezi Agosti alipovunjika mguu aliifungia Timu yake bao la kwanza baada ya kupokea pasi nzuri toka kwa Winga Aaron Lennon kwenye dakika ya 11.
Hadi mapumziko Tottenham 1 West Ham 0.
Kipindi cha pili dakika ya 81, Jermaine Defoe alipachika bao la pili kufuatia kaunta ataki murua ya Tottenham.
VIKOSI:
Tottenham: Gomes, Corluka, Dawson, King, Assou-Ekotto, Lennon, Palacios, Huddlestone, Modric, Crouch, Defoe.
AKIBA: Alnwick, Hutton, Bale, Jenas, Keane, Bassong, Kranjcar.
West Ham: Green, Faubert, Tomkins, Upson, Ilunga, Collison, Behrami, Kovac, Parker, Diamanti, Franco.
AKIBA: Stech, Jimenez, Spector, Da Costa, Nouble, Payne, Stanislas.
REFA: Chris Foy
Mechi za LIGI KUU England zinazofuata na zitakazoanza muda si mrefu ni:
Blackburn v Sunderland
Chelsea v Fulham
Everton v Burnley
Stoke v Birmingham
[saa 4 dak 45 usiku]
Wolves v Man City
Ancelotti akiri Chelsea taabani!!!
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amekubali kuwa Timu yake Chelsea kwa sasa ipo hoi bin taabani kufuatia matokeo yasiyoridhisha katika mechi za hivi karibuni na kudorora kwao kumefuatia mara baada ya kuikung’uta Arsenal 3-0 kwenye Ligi Kuu mwezi uliopita.
Tangu ushindi huo wa kishindo Chelsea wameshinda mechi moja tu katika 5 walizocheza na sasa wapinzani wao Manchester United na Arsenal wameikaribia mno kwenye msimamo wa Ligi.
Chelsea bado wanaongoza Ligi Kuu wakiwa na pointi 42 wakifuatiwa na Man Uwenye pointi 40 na Arsenal pointi 38.
Ancelotti amekiri kupwaya kwao na amesema: “Ni kweli tumepoteza mwelekeo lakini bado tuna uwezo wa kutwaa Ubingwa! Ni mbio ndefu na sasa tuko Nusu tu!”
Leo jioni Chelsea watakuwa nyumbani Stamford Bridge kuikwaa Timu ngumu Fulham kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Rooney apona kuzivaa hasira za Fergie!!!
Wayne Rooney amepona kukumbana na hasira za Meneja wake Sir Alex Ferguson hapo jana baada ya kufanya kosa kubwa lililoisaidia Hull City kupata bao la kusawazisha kwenye mechi ya Ligi Kuu ambayo hatimaye Manchester United walishinda mabao 3-1.
Rooney ndie aliewafungia Man U bao la kwanza dakika za majeruhi za kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili Rooney alifanya kosa kubwa pale pasi yake aliyotaka kumrudishia Kipa wake Kuszczak kunaswa na Craig Fagan aliemtilia pasi mwenzake Altidore lakini aliangushwa na Beki wa Man U Rafael kwenye boksi na ndipo Fagan akasawazisha kwa penalti.
Rooney amesema: “Goli lao la kusawazisha ni kosa langu! Meneja wangu asingefurahishwa lakini bahati tumeshinda!”
Baada ya kosa lake, Rooney alicheza kufa na kupona na kusababisha bao la pili pale krosi yake ilipombabaisha Beki wa Hull Andy Dawson na kujifunga mwenyewe.
Kisha Rooney akatengeneza bao la 3 na kumpa pasi Berbatov aliepachika bao hilo.
Ferguson alimsifia Rooney kwa kusema: “Ni mpiganaji! Alifanya kosa moja lakini yeye ni mshindi! Alijisahihisha na kuutengeneza ushindi wetu!”
Kwa goli lake la jana sasa Rooney ana magoli 13 kwenye Ligi Kuu na amefungana na Defoe pamoja na Drogba katika Ufungaji goli nyingi.

Sunday 27 December 2009

Man U yaidunda Hull na kurudi nafasi ya 2!!!
Kwa mara ya kwanza katika mechi karibu 5, Manchester United leo walishuka ugenini uwanja wa KC kupambana na Hull City kwenye mechi ya Ligi Kuu huku wakiwa na Difensi ambayo inatambulika na si ile ya kuungaunga iliyowafanya wachapwe na Villa na Fulham.

Leo Beki ilichezwa na Rafael pembeni kulia, Evra pembeni kushoto na Dabo Sentahafu ilichezwa na Wes Brown na Nemanja Vidic.
Carrick na Fletcher ambao ndio walikuwa wakicheza kama Masentahafu katika mechi za hivi karibuni, kwenye mechi hii walirudi kwenye nafasi zao za kawaida za Kiungo.
Na Kikosi hicho kilichokuwa na uwiano hakikuwaangusha Washabiki wa Man U kwani waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 na hivyo kuipiku Arsenal na kutinga nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi huku Chelsea bado wakiongoza wakiwa na pointi 42, Man U 40, Arsenal 38 na Aston Villa 35. 
Wayne Rooney alifunga bao la kwanza Kipindi cha Kwanza kwenye dakika za majeruhi baada ya kazi nzuri kwenye wingi ya kulia ya Darren Fletcher alietia krosi iliyoguswa na Giggs na kumkuta Rooney alieidokoa hadi wavuni.
Kipindi cha pili Hull walisawazisha kwa penalti iliyofungwa na Craig Fagan dakika ya 14 baada ya pasi ya Rooney kunaswa na Fagan aliempasia Jozy Altidore ambae aliangushwa na Rafael wa Man U na Refa Alan Wiley kuamua ni penalti.
Katika dakika ya 28 ya Kipindi hicho cha Pili, Man U walifunga bao la pili baada ya Giggs kumpenyezea Rooney aliepiga krosi ili imfikie Park [alieingizwa badala ya Valencia] lakini Beki wa Hull Andy Dawson akajifunga mwenyewe.
Dimitar Berbatov akaweka wavuni bao dakika ya 82 baada ya pande tamu kutoka kwa Wayne Rooney.
VIKOSI:
Hull: Myhill, Mendy, Gardner, Zayatte, Dawson, Garcia, Boateng, Olofinjana, Hunt, Altidore, Fagan.
AKIBA: Duke, Barmby, Geovanni, Kilbane, Ghilas, Vennegoor of Hesselink, Cairney.
Man Utd: Kuszczak, Rafael Da Silva, Vidic, Brown, Evra, Valencia, Carrick, Fletcher, Giggs, Berbatov, Rooney.
AKIBA: Foster, Owen, Park, Welbeck, Fabio Da Silva, Obertan, De Laet.
REFA: Alan Wiley
MECHI ZINAZOKUJA ZA LIGI KUU England: [saa za bongo]
Jumatatu, 28 Desemba 2009
[saa 9 dak 45 mchana]
Tottenham v West Ham
[saa 12 jioni]
Blackburn v Sunderland
Chelsea v Fulham
Everton v Burnley
Stoke v Birmingham
[saa 4 dak 45 usiku]
Wolves v Man City
Jumanne, 29 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Hull
Jumatano, 30 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v Arsenal
[saa 5 usiku]
Man U v Wigan
Fabregas aipa ushindi Arsenal lakini...........!!!!!!!
Nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas ambae leo ndie alieipa ushindi Timu yake baada ya kuingizwa Kipindi cha Pili na kufunga bao 2 zilizoipa ushindi Arsenal wa bao 3-0 dhidi ya Aston Villa kwenye Ligi Kuu Uwanjani Emirates alilazimika kutolewa huku zikiwa zimebaki dakika 6 mpira kumalizika baada ya kujitonesha sehemu aliyoumia hivi karibuni na ambayo ndio iliyomfanya asianze mechi hii tangu mwanzo.
Taarifa zinasema kuna hatari Fabregas akawa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja baada ya kujiumiza tena musuli ule ule wa mguu uliomfanya akose mechi hivi karibuni.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amethibitisha habari za kuumia Nahodha wake ingawa amesema bado hawajajua atakuwa nje kwa muda gani. 
Wenger vilivile alidokeza kuwa mwezi Januari wanaweza kuingia sokoni dirisha la uhamisho litakapofunguka kununua Mshambuliaji mmoja ili kuziba pengo la Robin van Persie ambae atakuwa nje mpaka Aprili au Mei kuuguza enka yake.
Mitutu ikiongozwa na Fabregas yaiua Villa!!
Katika mechi ya Ligi Kuu leo Arsenal wakiwa nyumbani Uwanjani Emirates wameipiga Aston Villa mabao 3-0 na mabao mawili ya kwanza yakifungwa na Nahodha wao Cesc Fabregas alieanza mechi hii akiwa benchi na kuingizwa mara baada ya Kipindi cha Pili kuanza.
Fabregas alifunga bao la kwanza kwa frikiki murua kwenye dakika ya 65 na kuongeza bao la pili baada ya pasi tamu ya Theo Walcott dakika ya 80.
Abou Diaby akaongeza bao la 3 dakika ya 90.
Kwa ushindi huo, Arsenal sasa wako nafasi ya pili na wamecheza mechi 18 na wana pointi 38 na wako nyuma ya Chelsea wanaoongoza kwa kuwa na pointi 42 kwa mechi 19.
Mabingwa Watetezi Manchester United, wanaocheza na Hull City muda si mrefu kuanzia sasa, wako nafasi ya 3 wakiwa wamecheza mechi 18 na wana pointi 37.
Aston Villa wako nafasi ya 4, wamecheza mechi 19 na wana pointi 35.
VIKOSI:
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Traore, Song Billong, Denilson, Nasri, Diaby, Eduardo, Arshavin.
AKIBA: Fabianski, Fabregas, Vela, Walcott, Ramsey, Silvestre, Eboue.
Aston Villa: Friedel, Luke Young, Dunne, Cuellar, Warnock, Ashley Young, Petrov, Milner, Downing, Agbonlahor, Heskey.
AKIBA: Guzan, Sidwell, Carew, Delph, Reo-Coker, Beye, Collins.
DAVID JAMES ataka kuhamia Spurs!
Kipa wa Portsmouth David James, miaka 39, ambae pia hudakia Timu ya England, ameonyesha dhamira yake ya kuungana tena na aliekuwa Meneja wa Portsmouth ambae sasa yupo Tottenham, Harry Redknapp, ili fufue matumaini yake ya kuitwa Kikosi cha England kitachokwenda Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwakani.
James amesema: “Ni bora kuchezea Spurs, huko nafasi yangu ya kuchezea England itaongezeka! Harry ni Kocha bora na ndio maana Spurs wana mafanikio!”
Huko Tottenham, Kipa wao wa akiba, Carlo Cudicini, yupo nje baada ya kuumia kwenye ajali ya pikipiki na hilo litamfanya James awe Kipa Msaidizi chini ya Kipa kutoka Brazil Heurelho Gomes ambae siku za nyuma alionekana kupwaya.
Hata hivyo, Meneja wa sasa wa Portsmouth, Avram Grant, hayuko tayari kumwachia David James kuondoka ingawa anaweza kulazimika kumwachia kwa vile Portsmouth ina matatizo makubwa ya fedha.
LIVERPOOL yashinda kwa “msaada wa Refa!”
Jana Liverpool iliweza kuwafunga Wolves 2-0 kwenye Ligi Kuu baada ya Wolves kucheza mtu 10 mara baada ya Refa Andre Marriner kumtoa Stepen Ward kwa Kadi Nyekundu baada ya kumpa kadi ya pili ya Njano katika mazingira ya utatanisha.
Refa Marriner kwanza alimpa Kadi ya Njano Berra kwa rafu ambayo Ward alimchezea Lucas Leiva wa Liverpool lakini baada ya Wachezaji wa Liverpool kulalamika, Refa huyo aliongea na Msaidizi wake na ndipo alipompa Kadi ya Pili ya Njano Ward na kisha kumwonyesha Nyekundu na kumtoa.
Uamuzi huo uliwapa mwanya Liverpool waliofunga bao la kwanza kupitia Steven Gerrard na la pili akafunga Yossi Benayoun.
WOLVES walalamikia Refa kuibeba Liverpool!!!
Bosi wa Wolves Mick McCarthy amepinga vikali kutolewa Mchezaji wake Stephen Ward na Refa Andre Marriner ambae alimpa Kadi 2 za Njano na kisha Nyekundu na hivyo kuwapa mwanya Liverpool kupata bao 2 baada ya Wolves kubaki mtu 10.
Refa Marriner kwanza alimpa Kadi ya Njano Berra kwa rafu ambayo Ward alimchezea Lucas Leiva wa Liverpool lakini baada ya Wachezaji wa Liverpool kulalamika, Refa huyo aliongea na Msaidizi wake na ndipo alipompa Kadi ya Pili ya Njano Ward na kisha kumwonyesha Nyekundu na kumtoa.
McCarthy amedai: “Nimeona marudiao ya video! Sidhani alistahili kutolewa nje! Refa hakupata msaada wowote toka kwa Mwamuzi wa akiba Phil Dowd! Na pale alipompa KadI Berra na kulalamikiwa na Wachezaji wa Liverpool alilazimika kumpa Kadi Ward!! Hayo ni makosa kwa Refa kukubalisha presha ya Wachezaji!”
MANCINI aanza kibarua kwa ushindi!!
Meneja mpya wa Manchester CityRoberto Mancini ameanza kibarua kwa mguu mzuri baada ya kuwafunga Stoke City 2-0 hapo jana kwenye Ligi Kuu lakini amekiri kuwa Timu yake inabidi iongeze juhudi na kukaza uzi.
Mancini amembadili Meneja Mark Hughes Jumamosi iliyopita na mechi ya jana ilikuwa ndio mechi yake ya kwanza ambapo Martin Petrov na Carlos Tevez ndio waliomfungia mabao ya ushindi yaliyopatikana kipindi cha kwanza.
Wenger haitaki mipira ya kurusha!!
Arsene Wenger wa Arsenal amependekeza kuwa badala ya mipira kurushwa ikitoka pembeni mwa uwanja ziwe zinapigwa frikiki ili kuharakisha mchezo.
Mfaransa huyo pia amedai kuwa baadhi ya Timu kwenye Ligi kuu hunufaiki zaidi kwa vile tu wanao Wachezaji wenye nguvu ya kurusha mipira mbali na akatoa mfano wa Mchezaji wa Stoke City Rory Delap ambae akirusha mpira ni kama kaupiga kwa mguu na mara nyingi huipa ushindi Stoke kwa mipira ya kurusha.
Wenger amedai: “ Sheria ibadilishwe! Soka ni mpira wa miguu na si mikono!”
Powered By Blogger