Saturday 4 October 2008

Jumapili, 5 Oktoba 2008

[saa 9 na nusu mchana saa za bongo]

West Ham v Bolton

[saa 11 jioni]

Manchester City v Liverpool

Portsmouth v Stoke City

Tottenham v Hull City

Chelsea v Aston Villa

[saa 1 usiku]

Everton v Newcastle
BLACKBURN 0 MAN U 2

Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United wameshinda mabao 2-0 nyumbani kwa Blackburn Rovers Ewood Park.
Magoli ya Man U yalifungwa na Wes Brown kipindi cha kwanza kufuatia kona ya Wayne Rooney na Wes Brown akamalizia kwa kichwa.
Kipindi cha pili Man U walifunga goli la pili lililowekwa kimiani na Wayne Rooney baada ya kazi nzuri sana ya Ronaldo.
MATOKEO LIGI KUU: MECHI ZILIZOANZA SAA 11 JIONI [bongo taimu]

Sunderland 1 v Arsenal 1
Cesc Fabregas ameiokoa Arsenal toka kipigoni baada ya kusawazisha bao dakika za majeruhi kwa kichwa kufuatia kona.
Grant Leadbitter aliipatia Sunderland bao murua la kuongoza kwa shuti kali lililogonga posti ya juu na kudunda wavuni.

West Brom 1 v Fulham 0
Roman Bednar alifunga bao na kuwapa ushindi WBA wakiwa uwanja wao wa nyumbani.

Wigan 0 v Middlesbrough 1
Jeremie Aliadiere ameipa ushindi Middlesbrough wakiwa ugenini kwa bao zuri la dakika za mwisho kufuatia krosi ya Didier Digard ambayo Stewart Downing alipiga kichwa cha chini na Jeremie Aliadiere akaunganisha moja kwa moja.
Ferguson aomba radhi kwa Ince

Wakati leo Blackburn inayoongozwa na Meneja Paul Ince aliewahi kuchezea Manchester United inakutana na timu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amekiri alimkosea Paul Ince pale alipomwita 'big-time Charlie' akimaanisha ni mtu hovyo, mpenda mzaha na asie na maana.
Bosi huyo wa Manchester United alitoa maneno hayo mwaka 1998 alipokuwa akiwapa nasaha Wachezaji wa Man U kabla ya pambano lao na Liverpool ambayo siku hiyo mmoja wa Wachezaji wao alikuwa Paul Ince.
Paul Ince aliuzwa kwa Inter Milan na Sir Alex Ferguson lakini alipohama Inter Milan akaenda kwa Watani wa Jadi wa Manchester United Klabu ya Liverpool kitendo ambacho kiliwakera sana washabiki wa Man U.
Sir Alex Ferguson amekiri: 'Najuta kutoa kauli ile. Lilikuwa kosa.'
Paul Ince alichukizwa sana na kitendo cha kuuzwa na Sir Alex Ferguson na akasusa kuongea na Ferguson kwa miaka kadhaa ingawa siku hizi wanaongea kama kawaida.
Maneno ya Ferguson kumdhihaki Paul Ince yalirekodiwa na Wapiga Picha za TV waliokuwa wanatengeneza filamu kuhusu Klabu ya Manchester United.
Leo Sir Ferguson anakutana uso kwa uso na Paul Ince kama Meneja wa Klabu kwa mara ya kwanza na Ferguson ametamka kwamba hakuwa na tatizo na Ince kama Mchezaji kwani alikuwa Mchezaji mzuri sana ingawa Washabiki wa Man U wanamchukia kwa kuhamia Liverpool.
Nae Paul Ince anasema: 'Kwa sasa nikiwa na matatizo huwa nampigia Sir Alex Ferguson kuomba mawaidha. Yeye ni mtu mwenye kiwango bora! Nimecheza chini ya Mameneja wengi lakini hakuna hata mmoja anaempata Ferguson!

Friday 3 October 2008



MECHI ZA JUMAMOSI: Tathmini

Sunderland v Arsenal

Sunderland watakuwa uwanjani kwao Stadium of Light kuwakaribisha Arsenal ambao watakuwa kama mbogo waliojeruhiwa baada ya kufungwa na Hull City bao 2-1 wiki iliyokwisha.
Sunderland huenda wakawakosa Kiungo Liam Miller, Teemu Tainio, Phil Bardsley na Grant Leadbitter kwa kuwa ni majeruhi.
Arsenal, mbali ya majeruhi wa muda mrefu kina Tomas Rosicky, Amaury Bischoff na Eduardo, Wachezaji wote wako fiti.

TIMU:

Sunderland : Gordon, Fulop, Chimbonda, Ferdinand, Collins, McCartney, Diouf, Whitehead, Miller, Reid, Richardson, Malbranque, Henderson, Cisse, Murphy, Healy, Stokes, Chopra.

Arsenal : Almunia, Clichy, Toure, Gallas, Sagna, Nasri, Fabregas, Denilson, Walcott, Adebayor, Van Persie, Fabianski, Song, Djourou, Vela, Bendtner, Ramsey, Eboue, Silvestre.

REFA: Lee Mason (Lancashire)

West Brom v Fulham

West Brom wakiwa uwanjani kwao The Hawthorns watawakosa Kiungo Kim Do-Heon na Filipe Teixeira.
Nao Fulham huenda wakamkosa Bobby Zamora anaetatizwa na Flu wakati Andrew Johnson kafungiwa baada ya kula kadi nyekundu mechi iliyokwisha.

TIMU:

West Brom : Carson, Kiely, Zuiverloon, Hoefkens, Barnett, Donk, Olsson, Robinson, Morrison, Greening, Koren, Cech, Beattie, Moore, Miller, Valero, Bednar, MacDonald, Pele.

Fulham : Schwarzer; Pantsil, Hughes, Hangeland, Konchesky; Davies, Bullard, Murphy, Gera; Zamora, Seol, Zuberbuhler, Nevland, Dempsey, Andreasen, Kallio, Baird, Stoor, Gray.

REFA: Mark Halsey (Lancashire)

Wigan v Middlesbrough

Wigan watakuwa kwao JJB Stadium na Mchezaji pekee mwenye hatihati ya kutocheza ni Lee Cattermole wakati wapinzani wao Middlesbrough huenda wakacheza bila ya Beki Robert Huth.

TIMU:

Wigan : Kirkland, Melchiot, Boyce, Bramble, Figueroa, Valencia, Cattermole, Palacios, Kapo, Heskey, Zaki, Brown, Camara, De Ridder, Kilbane, Koumas, Kupisz, Scharner, Taylor, Pollitt, Kingson.

Middlesbrough : Turnbull, Jones, Hoyte, Wheater, Huth, Riggott, Taylor, Grounds, Digard, O'Neil, Aliadiere, Downing, Johnson, Shawky, Alves, Mido, Walker, Emnes, Craddock.

REFA: Martin Atkinson (Yorkshire)

Blackburn v Man Utd

Blackburn wakiwa kwao Ewood Park wanawakaribisha jirani zao Mabingwa Manchester United.
Klabu hizi ziko umbali wa kiasi ya maili 50 kati yao.
Hii ni mechi ambayo Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson anapambana na Mchezaji na Nahodha wake wa zamani ambae sasa ndie Meneja wa Blackburn Paul Ince.
Blackburn huenda wakawakosa kwa sababu ya maumivu Kipa Paul Robinson, Vince Grella na Benni McCarthy ingawa McCarthy ameshaanza mazoezi.
Kwa Manchester United, Wayne Rooney yuko kwenye hatihati baada ya kuumia enka juzi huko Denmark kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE walipocheza na Aalborg wakati Paul Scholes, Owen Hargreaves na Michael Carrick kuna uhakika hawawezi kucheza.

TIMU:

Blackburn : Brown, Robinson, Bunn, Nelsen, Samba, Ooijer, Warnock, Emerton, Olsson, Tugay, Derbyshire, Santa Cruz, Villanueva, Fowler, Andrews, Fowler, Grella, Treacy, Pedersen.

Man Utd : Van der Sar, Amos, Neville, Brown, Rafael, Ferdinand, Vidic, Evans, Evra, Ronaldo, O'Shea, Fletcher, Anderson, Giggs, Nani, Tevez, Berbatov, Rooney, Welbeck.

REFA: ALAN WILEY (Stafforshire)
SCHOLES NA FLETCHER WAONGEZA MIKATABA

Mabingwa wa LIGI KUU UINGEREZA NA ULAYA, Manchester United, leo wametangaza Wachezaji wao Paul Scholes na Darren Fletcher wameongeza mikataba yao.
Paul Scholes ameongeza hadi Juni 2010 na Darren Fletcher hadi Juni 2012.
Meneja wa Man U alipotangaza habari hizi alitamka: 'Scholes ni uthibitisho kwamba ukijitunza binafsi basi utadumu kwa muda mrefu kwenye klabu kubwa. Tizama Scholes yuko hapa tangu ana miaka 14 na sasa ana miaka 34! Nae Fletcher yuko hapa muda mrefu kama Giggs, Scholes na Wes Brown. Uvumilivu na uchezaji wake ni hazina kwetu!'
Wakitoa shukrani zao, Scholes alisema kwamba ni jambo kubwa kuongeza mkataba kwani ana nia kubwa ya kupata mafanikio zaidi ya msimu uliokwisha. Na Fletcher akaunga mkono kwa kutamka kuwa ukichezea klabu kubwa kama Man U hutaki kuhama na daima unataka kuchangia mafanikio.
Van der Sar arudi kuiokoa kwa muda Timu ya Uholanzi yenye majeruhi baada ya kustaafu.

Kipa wa Manchester United Edwin van der Sar ambae alitangaza kustaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Uholanzi mara baada ya mashindano ya EURO 2008 mwezi Julai atarudi tena kuichezea Timu hiyo kwa mechi mbili tu wiki ijayo kwenye mapambano ya mtoano wa kuwania nafasi za kuingia FAINALI KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI 2010.
Kocha wa Uholanzi Bert van Marwijk na msaidizi wake Frank de Boer imebidi wamuombe Edwin van der Sar arudi kibaruani toka kwenye kustaafu kufuatia kuumia kwa Makipa wote wawili wa Timu ya Taifa.

Makipa hao majeruhi ni Maarten Stekelenburg wa Ajax na yule wa Feyenoord Henk Timmer.
Kocha Bert van Marwijk amemtaja Van der Sar kwenye kikosi cha Wachezaji 22 kitakachocheza mechi za KUNDI LA 9 na Iceland mjini Rotterdam, Uholanzi tarehe 11 Oktoba na ugenini zidi ya Norway siku nne baadae.
Van der Sar ameshaidakia Uholanzi mara128.
TIMU YA MARSEILLE YATEMBEZA KOFIA KIWANJA CHA NDEGE ILI WAPATE PESA ZA MAFUTA NDEGE IWARUDISHE KWAO!

Viongozi na Wachezaji wa Klabu ya Ufaransa Marseille walijkuta waking'uta mifuko yao ili kuchangishana pesa ili walipie mafuta ya ndege iliyokuwa iwarudishe kwao Marseille kutoka Madrid walikofungwa na Atletico Madrid mabao 2-1 kwenye mechi ya UEFA CHAMPION LEAGUE Jumatano usiku.
Mkasa huu uliwakuta baada ya ndege yao kunyimwa mafuta na Kampuni ya Mafuta CLH kwa madai hawakuruhusiwa na Exxon Kampuni ya Mafuta yenye mkataba na wamiliki wa ndege hiyo wa kuwajazia mafuta popote ndege zao zilipo duniani. CLH walidai Exxon haikutuma ombi lolote la mafuta kwao na wakagoma kutoa mafuta kwa mkopo wakidai pesa taslimu.
Ndipo kofia ikazungushwa kuchangishana EURO 3,000 za mafuta.
Kocha wa Marseille Eric Gerets alidhihaki mkasa huo kwa kusema: 'Ilibidi nitoe pesa zangu zote mfukoni na nikashindwa kununua hata sigara hapo uwanjani! Ingekuwa tumeshinda nisingejali! Lakini tumefungwa, tumekwama, sigara nimekosa, pesa sina!'
Mchezaji Etxeberria asaini mkataba kuchezea Athletic Bilbao bure!!!!

Joseba Etxeberria amesaini nyongeza ya mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Klabu ya Spain Athletic Bilbao iliyoko La Liga huko Spain bure bila ya kulipwa hata senti mmoja ikiwa pamoja na kutopokea mshahara hadi mkataba utakapoisha mwishoni mwa msimu ujao.
Mchezaji huyo wa wa zamani wa Kimataifa wa Spain ambae ni Kiungo mwenye umri wa miaka 31 alijiunga na Athletic Madrid akiwa na miaka 17 na hajahama tangu wakati huo. Mkataba wake wa kawaida wenye malipo kama ilivyo desturi uliisha mwishoni mwa msimu uliopita.
Ili kutimiza ndoto yake ya kustaafu akiwa Klabu moja tu na kuweka rekodi ya kucheza mechi 500 baada ya kuwa na Atletic Bilbao ndio maana Joseba Etxeberria amekubali kucheza bure kwa mwaka mmoja.
Mchezaji huyu alikuwa kwenye kikosi cha Spain cha Kombe la Dunia mwaka 1998 na ameshachezea Spain kwenye Fainali za Mataifa ya Ulaya mara mbili.
Rais wa Klabu hiyo Atletic Madrid Fernando Garcia Macua amesema: "Sisi kama Klabu hatuna jinsi ya kumshkuru!! Hiki ni kitendo cha upendo na uzalendo wa hali ya juu!!'
Nae mdau mmoja alinena: 'Kitendo hiki kinawaaibisha wale Mastaa wote wa sasa wenye uroho wa mabilioni ya pesa na hawana msaada kwa yeyote!!'
UEFA CUP: EVERTON WATUPWA NJE, TOTTENHAM, ASTON VILLA NA PORTSMOUTH WASONGA MBELE!

Jana Timu kadhaa za Uingereza zilijitupa uwanjani katika mechi za marudiano za kuamua timu zipi zinaingia raundi ya makundi kugombea Kombe la UEFA.
Matokeo ni kama ifuatavyo:

Wisla Krakow 1-1 Tottenham

Tottenham wasonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya kushinda mechi ya kwanza 2-1.

Standard Liege 2-1 Everton

Everton wametupwa nje kwa jumla ya mabao 4-3. Mechi ya kwanza walitoka suluhu 2-2.

Man City 2-1 Omonia Nicosia

Man City wanasonga mbele kwa kushinda mechi zote mbili kwa mabao 2-1 kila moja.

Aston Villa 1-1 Litex Lovech

Aston Villa walishinda mechi ya kwanza kwa mabao 3-1 hivyo wameingia raundi nyingine kwa jumla ya mabao 4-2.

Guimaraes 2-2 Portsmouth

Portsmouth walishinda mechi ya kwanza kwa mabao 2-0 lakini kwenye mechi hii ya marudiano walipigwa 2-0 hadi dakika 90 zilipokwisha na kufanya timu ziwe sare kwa jumla ya magoli 2-2.
Ndipo muda wa nyongeza ukachezwa na Portsmouth wakamudu kurudisha kwa mabao yaliyofungwa na Mshambuliaji wao ‘ngongoti’ Peter Crouch na kufanya mechi iwe sare ya 2-2 lakini Portsmouth wamesonga mbele kwa jumla ya mabao 4-2.

Thursday 2 October 2008


LIGI KUU: MECHI ZA WIKIENDI

Jumamosi, 4 Oktoba 2008

[saa 11 jioni saa za bongo]

Sunderland v Arsenal

West Brom v Fulham

Wigan v Middlesbtough

Blackburn v Man United [saa 1 na nusu usiku, bongo taimu]

Jumapili, 5 Oktoba 2008

[saa 9 na nusu mchana saa za bongo]

West Ham v Bolton

[saa 11 jioni]

Manchester City v Liverpool

Portsmouth v Stoke City

Tottenham v Hull City

Chelsea v Aston Villa

[saa 1 usiku]

Everton v Newcastle
CHELSEA WABANWA MBAVU RUMANIA

Wapigiwa wimbo wa Taifa wa Man United walipoingia uwanjani!!

Chelsea wameponea chupuchupu kufungwa huko Rumania walipokutana na timu mpya kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE CFR Cluj na kulazimisha kutoka sare ya 0-0 kwenye mechi ya KUNDI A.
Ili kuwatia kiwewe Chelsea, wakati timu zikiingia uwanjani kwenda kukaguliwa, zilikaribishwa kwa ‘WIMBO WA TAIFA WA MANCHESTER UNITED’ uitwao ‘GLORY, GLORY MAN UNITED’ huku Washabiki wakilifungua bango kubwa lililoandikwa: ‘WARIDI NI JEKUNDU, CHELSEA NI BLUU, BIBI YANGU MZAA MAMA ANAPIGA PENALTI VIZURI KUPITA NYIE!’ wakiwadhihaki Chelsea waliposhindwa kwa penalti na Man United kwenye Fainali ya mashindano haya msimu uliopita.
Chelsea walipata pigo kwenye mechi hii baada ya Mshambuliaji wao wanaemtegemea Didier Drogba kuumia na kutolewa nje ya uwanja kwenye dakika ya 57.
CFR Cluj: Stancioiu, Tony, Souza, Cadu, Pereira, Culio, Muresan, Dani, Dubarbier, Yssouf Kone, Trica (Didi 88). AKIBA: Nuno Claro, Panin, Hugo Alcantara, Deac, Emmanuel Kone, Ruiz.
KADI: Pereira, Dani.
Chelsea: Cech, Bosingwa, Alex, Terry, Bridge, Mikel, Kalou (Anelka 46), Ballack, Lampard, Malouda (Di Santo 74), Drogba (Belletti 57). AKIBA: Hilario, Ivanovic, Ferreira, Stoch.
KADI: Alex, Anelka.
WATAZAMAJI: 22,000.
REFA: Florian Meyer (Germany).

LIVERPOOL WAENDELEZA USHINDI

Robbie Keane jana amefunga goli lake la kwanza kwa Liverpool tangu ahamie hapo kutoka Tottenham na kuiwezesha timu yake kushinda kwa mabao 3-1 kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI KUNDI D waliyocheza na PSV Eindhoven ya Holland Uwanja wa Anfield huko Liverpool.
Dirk Kuyt aliipatia Liverpool bao lakuongoza dakika ya 4 tu ya mchezo baada ya shuti la Fernando Torres kutemwa na Kipa Andreas Isaksson. Kabla ya haftaimu Robbie Keane akafunga bao la pili.
Nahodha Steven Gerrard akapachika bao la 3 kwa Liverpool katika dakika ya 74 na hilo likiwa goli lake la 100 kuifungia Liverpool.
PSV Eindhoven wakapata bao lao moja dakika nne baadae mfungaji akiwa Danny Koevermans.
Liverpool: Reina, Arbeloa, Skrtel, Carragher, Aurelio, Kuyt, Gerrard (Babel 81), Alonso, Riera (Benayoun 68), Torres, Keane (Leiva Lucas 75). AKIBA: Cavalieri, Dossena, Agger, Mascherano.
MAGOLI: Kuyt 5, Keane 34, Gerrard 76.
PSV: Isaksson, Kromkamp, Simons, Marcellis, Salcido, Brechet (Pieters 46), Mendez (Dzsudzsak 76), Culina, Bakkal, Amrabat, Wuytens (Koevermans 60). AKIBA: Cassio, Rodriguez, Zonneveld, Nijland.
KADI: Marcellis.
GOLIs: Koevermans 78.
WATAZAMAJJI: 41,097
REFA: Felix Brych (Germany).
MATOKEO KAMILI:

KUNDI A
Bordeaux 1-3 Roma
CFR Cluj 0-0 Chelsea

KUNDI B
Anorthosis Famagusta 3-1 Panathinaikos
Inter Milan 1-1 Werder Bremen

KUNDI C
Shakhtar Donetsk 1-2 Barcelona
Sporting 2-0 Basle

KUNDI D
Atletico Madrid 2-1 Marseille
Liverpool 3-1 PSV

MECHI ZINAZOFUATA:

Jumanne, 21 Oktoba 2008

KUNDI E

Man U v Celtic

Villarreal v AaB,

KUNDI F

Bayern Munich v Fiorentina,

Steaua Bucuresti v Lyon,

KUNDI G

FC Porto v Dynamo Kiev,

Fenerbahce v Arsenal,

KUNDI H

Juventus v Real Madrid,

Zenit St Petersburg v BATE Borisov

Jumatano, 22 Oktoba 2008

KUNDI A

Bordeaux v CFR Cluj-Napoca,

Chelsea v Roma,

KUNDI B

Inter Milan v Anorthosis Famagusta,

Panathinaikos v Werder Bremen,

KUNDI C

Basle v Barcelona,

Shakhtar Donetsk v Sporting,

KUNDI D

Atletico Madrid v Liverpool

PSV v Marseille,

Wednesday 1 October 2008

BAADA YA USHINDI WA JANA:

Wenger asherehekea ushindi!!!

Meneja wa Arsenal Arsena Wenger, baada ya mstuko wa kupigwa na 'vibonde' Hull City Jumamosi uliomfanya aweweseke hadi kukosea kutaja timu iliyomfunga na kuiita West Brom na kuahidi shoka litatembea kwa Wachezaji kwenye mechi ya jana, alikuwa mtu mwenye furaha kubwa jana baada ya ushindi wa mabao 4-0.

Wenger hakutimiza ahadi yake ya shoka ingawa hakumchezesha Eboue na badala yake Samir Nasri alianza na dakika ya 64 Eboue akambadilisha Nasri.

Wenger alinena kwa furaha: 'Sikufanya mabadiliko kwani sikutaka nionekane natoa adhabu kwa Wachezaji. Ni bora uipe timu nafasi ijirekebishe makosa!'

Sir Alex Ferguson akumbwa na majeruhi!!!

Ingawa Mabingwa wa Ulaya, Manchester United, wamefurahia ushindi wa mabao 3-0 ugenini huko Aalborg, Denmark walipoitwanga Aab Aalborg, ushindi huo pengine umekuja kwa gharama kubwa kutokana na kuumia kwa Wachezaji muhimu sana kwa timu.

Paul Scholes aliumia goti dakika ya 16 tu ya mchezo na akatolewa kwa machela na nafasi kuchukuliwa na Ryan Giggs. Mwishoni mwa mechi Scholes alionekana akitembelea kwa magongo. Ferguson alisema huenda Scholes akawa nje ya uwanja kwa wiki hadi 8.

Pigo la pili lilikuwa kuumia enka kwa Wayne Rooney ingawa taarifa zilisema kutolewa kwake uwanjani ilikuwa ni tahadhari tu na maumivu yake si ya kutisha kama ya Scholes. Nafasi ya Rooney kwenye mechi hiyo ilichukuliwa na Carlos Tevez.

Pigo la tatu ni kuumia kwa Beki chipukizi Rafael kutoka Brazil ambae alikuwa akianza mechi kubwa kwa mara ya kwanza na nafasi yake kushikwa na Wes Brown.

Nae Dimitar Berbatov aliefungua akaunti yake ya kufunga magoli kwa Man U hapo jana alipofunga bao 2 amemkosha Ferguson aliemsifia sana: 'Berbatov amefunga magoli mawili maridadi sana! Magoli hayo ya mwanzo kuifungia Man U yatampa morali kubwa!'


MECHI ZA LEO:
Jumatano, 1 Oktoba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]

KUNDI A

CFR Cluj-Napoca v Chelsea

Bordeaux v Roma

KUNDI B

Anorthosis Famagusta v Panathinaikos

Inter Milan v Werder Bremen

KUNDI C

Shakhtar Donetsk v Barcelona

Sporting Lisbon v Basle

KUNDI D

Atletico Madrid v Marseille

Liverpool v PSV
TATHMINI:
Chelsea baada ya kupata ushindi mnono nyumbani Stamford Bridge walipowafunga Bordeaux bao 4-0 sasa watakuwa nchini Romania kupambana na timu mpya kwenye mashindano haya CFR Cluj-Napoca iliyofanya maajabu kwenye mechi ya kwanza ilipoifunga timu yenye uzoefu na ngumu Roma ya Italia nyumbani kwake.
Nao Liverpool baada ya kushinda ugenini kwa bao 2-1 zidi ya Marseille sasa itakuwa nyumbani Anfield kupigana kuendeleza wimbi la ushindi watakapocheza na PSV Eindhoven ya Uholanzi iliyofungwa nyumbani na Atletico Madrid.
Mechi nyingine tamu ni ile ya KUNDI B wakati INTER MILAN, Timu ya Kocha Jose Mourinho, itakapoikaribisha timu ngumu toka Ujerumani Werder Bremen.
Juzi, Inter Milan ilifungwa na watani wao AC MILAN kwenye mechi ya Ligi ya Italia SERIE A kwa bao 1-0 kwa bao la Ronaldinho na hicho kikawa kipigo cha kwanza kwa Jose Mourinho tangu atue Italia.
Katika mechi hiyo nae Mchezaji mwenye sifa mbaya duniani Marco Materazzi wa INTER MILAN alikula kadi nyekundu ingawa alikuwa hachezi kwani alikuwa mchezaji wa akiba kwenye benchi na alituhumiwa kumtukana Refa.
AaLBORG 0 MAN U 3

Dimitar Berbatov jana alifungua akaunti yake ya magoli kwa Man U alipopachika mabao mawili katika kipindi cha pili kwenye mechi ya michuano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE iliyochezwa Denmark zidi ya wenyeji Aab Aalborg ambayo Man U walishinda kwa mabao 3-0.

Bao la kwanza la Man U lilifungwa na Wayne Rooney kwenye dakika ya 22 baada ya pasi tamu ya Ryan Giggs alieingizwa dakika chache kabla baada ya Paul Scholes kuumia goti.

AaB Aalborg: Zaza, Bogelund, Olfers, Beauchamp (Caca 38), Pedersen, Augustinussen, Risgaard, Curth, Johansson, Enevoldsen, Saganowski. AKIBA: Stenild, Due, Braemer, Sorensen, Kristensen, Ronnie Schwartz Nielsen.
KADI: Johansson, Zaza.
Man Utd: Van der Sar, Rafael Da Silva (Brown 66), Ferdinand, Vidic, Evra, Ronaldo, Scholes (Giggs 16), O'Shea, Nani, Berbatov, Rooney (Tevez 59). AKIBA: Amos, Anderson, Park, Evans.
KADI: Rafael Da Silva.
MAGOLI: Rooney 22, Berbatov 55, 79.
WATAZAMAJI: 10,346
REFA: Olegario Benquerenca (Portugal
).

ARSENAL 4 FC PORTO 0

Arsenal wakiwa nyumbani Emirates Stadium walianza mechi hii kwa kukoswakoswa pale FC Porto, Mabingwa wa Ureno, pale Mchezaji wao Cristian Rodriguez alipopiga kichwa kilichogonga mwamba na kufuatiwa na shuti la Lisandro lililoondolewa kwenye mstari wa goli likiwa tayari kutinga wavuni.

Arsenal wakazinduka na kupachika mabao mawili kupitia kwa Van Persie dakika ya 31 na Adebayor dakika ya 40 hivyo kwenda haftaimu wakiwa mbele kwa mabao 2 kwa 0.

Kipindi cha pili wafungaji haohao wakaongeza mabao mengine mawili wakati Van Persie alipopachika dakika ya 48 na Adebayor akafunga penalti dakika ya 71.

Arsenal: Almunia, Sagna, Toure, Gallas, Clichy, Walcott (Vela 71), Fabregas, Denilson, Nasri (Eboue 64), Van Persie (Bendtner 64), Adebayor. AKIBA: Fabianski, Ramsey, Silvestre, Djourou.
KADI: Clichy.
MAGOLI: Van Persie 31, Adebayor 40, Van Persie 48, Adebayor 71 pen.
FC Porto: Helton, Sapunaru, Bruno Alves, Rolando, Benitez, Guarin, Costa, Fernando (Lucho Gonzalez 46), Raul Meireles (Hulk 64), Rodriguez (Candeias 79), Lopez. AKIBA: Nuno, Pedro Emanuel, Stepanov, Lino.
KADI: Costa.
Att: 59,623
REFA: Herbert Fandel (Germany).


MATOKEO KAMILI:

KUNDI E

Aalborg 0 v Man U 3

Villarreal 1 v Celtic 0

KUNDI F

Bayern Munich 1 v Lyon 1

Fiorentina 0 v Steau Bucharest 0

KUNDI G

Arsenal 4 v Porto 0

Fenrbahce 0 v Dynamo Kiev 0

KUNDI H

Bate 2 v Juventus 2

Zenit St Petersburg 1 v Real Madrid 2

Tuesday 30 September 2008


KIPIGO CHA HULL CITY CHAMTIA KIWEWE WENGER!

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameweweseka na kipigo toka kwa timu mpya LIGI KUU Hull City walichokipata Emirates Stadium ambayo ni ngome ya Arsenal walipobandikwa bao 2-1 Jumamosi iliopita kwenye mechi ya LIGI KUU.
Wenger alipohojiwa baada ya mechi alihuzunika sana na kuweweseka kiasi cha kutojua ni timu gani iliyomfunga na akawa anaitaja ni West Bromwich Albion badala ya Hull City. Pengine hali hiyo ilijitokeza kwa sababu siku hiyo ya kipigo ilikuwa ni siku yake kuadhimisha miaka 12 tangu atue Arsenal.

Wenger sasa ameahidi shoka litaanguka kwa baadhi ya Wachezaji kwenye mechi ya leo wanayocheza hapohapo kwao Emirates Stadium leo saa 3 dakika 45 usiku, saa za bongo, watakapocheza na timu mahiri na ngumu ya Ureno FC Porto katika mechi ya KUNDI G ya mashindano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Katika mechi za kwanza za Kundi hili FC Porto iliifunga timu machachari ya Uturuki Fenerbahce bao 3-1 walipocheza Ureno. Arsenal walitoka chupuchupu huko Ukraine walipochomoa bao dakika za mwisho na kutoka sare ya 1-1 na waliokuwa wenyeji wao Dynamo Kiev.

Arsene Wenger ameahidi mabadiliko kwenye kikosi na inatumainiwa Samir Nasri na Mikael Silvestre wanaweza kuanza kwani wote sasa wamepona maumivu yao.

LEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
Jumanne, 30 Septemba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]
KUNDI E: Aalborg v Man U******* Villarreal v Celtic
KUNDI F: Bayern Munich v Lyon******* Fiorentina v Steau Bucharest
KUNDI G: Arsenal v Porto******* Fenrbahce v Dynamo Kiev
KUNDI H: Bate v Juventus******* Zenit St Petersburg v Real Madrid
REFA WA MAN U v BOLTON AOMBA RADHI KWA PENALTI TATA!

Refa Rob Styles aliechezesha mechi ya LIGI KUU Jumamosi huko Old Trafford kati ya wenyeji Man U na Bolton na kuipa Man U penalti baada ya kuhisi Ronaldo kafanyiwa madhambi [tizama picha] na Beki wa Bolton JLoyd Samuel ameomba radhi kwa Bolton kwa kutoa penalti hiyo kimakosa.

Kulikuwa na hisia baada ya kosa hilo Refa huyo atanyimwa kuchezesha LIGI KUU wikiendi inayokuja lakini Bodi ya Marefa imethibitisha kupitia Bosi wake Keith Hackett kuwa amepangiwa kuchezesha mechi kati ya Tottenham na Hull City. Imekuwa desturi Refa anaefanya kosa kubwa huwa hapangiwi mechi za LIGI KUU wikiendi inayofuata.

Mara baada ya mechi, Sir Alex Ferguson wa Man U alitania kuhusu penalti hiyo kwa kusema: 'Nilishangaa maana niliona mchezaji wao kacheza mpira! Lakini huyu Refa Rob Styles msimu uliopita alitunyima penalti 4 au 5 za wazi! Naona sasa anatulipa! Sasa tunamdai penalti 4!!'

Baada ya kuambiwa kuhusu Refa Rob Styles kuomba radhi, Sir Alex Ferguson aliunga mkono kwa kusema: 'Anastahili sifa kwa kuwa na ujasiri wa kukubali kosa. Ameungama na imeonyesha utu wake. Hili ni jambo bora sana kwa soka yetu.'
Baada ya mechi hiyo ya Jumamosi Meneja wa Bolton Greg Megson alilalamika vikali na kumtaka Refa Rob Styles aombe radhi.
Nae Nahodha wa Bolton Kevin Nolan amekaririwa akisema hata Wachezaji wa Man U hasa Ronaldo aliekuwa bado kalala kwenye nyasi baada ya 'rafu' hiyo alisikika akisema: 'Sitaki penalti!' wakati Darren Fletcher na Gary Neville walimwambia mara baada ya tukio hilo la rafu tata na kabla penalti kupigwa kwamba ile haikuwa penalti.
Penalti hiyo tata iliwapa Man U bao la kwanza kwenye dakika ya 60 na Rooney akaingizwa toka benchi na kufunga bao la pili.

Aab Aalborg v Manchester United: Timu zinazoongozwa na Mameneja toka Scotland

Leo katika mechi ya KUNDI E ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE Mabingwa watetezi Manchester United wako nchini Denmark kwenye mji mdogo uitwao Aalborg kupambana na timu ndogo lakini ndio Mabingwa wa Denmark Aab Aalborg.

Mechi hii itakayoanza saa 3 dakika 45 usiku, saa za bongo, itachezwa kwenye Uwanja uitwao Energi Nord Arena wenye uwezo wa kuchukua Watazamaji 10,000 tu.

Aab Aalborg ilitoka sare kwenye mechi ya kwanza ya Kundi hili ilipocheza ugenini na Celtic huko Scotland. Kipa wa Aab Alborg Karim Zaza toka Morocco alikuwa shujaa alipookoa penalti kwenye mechi hiyo.

Aab Aalborg inaongozwa na Meneja ambae kama Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson ni mtu wa Scotland. Bruce Rioch, mwenye umri wa miaka 61, ni Mchezaji wa zamani wa Aston Villa na ameshawahi kuwa Meneja wa timu za LIGI KUU Middlesbrough na Arsenal.

Bruce Rioch ndie aliemsaini Dennis Berkamp na mwaka 1996 akiwa Meneja wa Arsenal waliwahi kuwafunga Man U kwa bao la Bergkamp.

Kikosi cha Aab Aalborg kina vijana wengi wa Timu ya Taifa ya Denmark ya umri wa chini ya miaka 21 ingawa kuna Wachezaji kadhaa toka nje ya nchi kama Kipa Karim Zaza [Morocco], Marek Saganowski (Poland), Andreas Johansson (Sweden) na Michael Beauchamp (Australia).

Wengi wanahisi hii ni mechi kati ya Klabu ndogo na maskini zidi ya Klabu kubwa na tajiri. Hebu linganisha: Uwanja wa Aalborg, Energi Nord Arena, una uwezo wa kuchukua Watazamaji 10,000 tu wakati Old Trafford wa Man U unapakia watu zaidi ya 76,000! Dau lililolipwa kumnunua Dimitar Berbatov toka Tottenham kuja Man U la Pauni Milioni 30 ni bajeti ya kuiendesha Aab Alborg kwa miaka 7!

Juu ya yote hayo, Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema: 'Timu za Denmark ni wapiganaji! Hatuwadharau hivyo ntashusha kikosi changu kamili.'

Monday 29 September 2008






MENEJA MPYA WA NEWCASTLE KUANZA KAZI AKIWA AMEKAA KWA WATAZAMAJI!

Joe Kinnear ambae ameteuliwa wiki iliyopita kuwa Meneja wa Muda wa Newcastle hadi mwisho wa mwezi wa Oktoba inapotegemewa Klabu huenda ikapata mmiliki mpya ataanza kazi yake kwa kukaa na Watazamaji badala ya benchi la Timu yake baada ya FA , Chama cha Soka Uingereza, kufafanua kuwa Meneja huyo bado hajatumikia adhabu aliyopewa mwaka 2004 ya kufungiwa mechi mbili na hivyo kutokukaa benchi la timu.

Joe Kinnear alipewa adhabu hiyo mwaka 2004 alipokuwa Meneja wa Nottingham Forest baada ya mechi waliyofungwa na Gillingham alipomwita Refa wa mechi hiyo 'ze comedy' yaani Msanii Mwigizaji na Mchekeshaji!

Wakati huo Kinnear alijitetea kuwa aliuliza: 'Huyu Refa anafanya shughuli gani na nikaambiwa ni Mwigizaji/Mchekeshaji basi nikaamua kumwita jina la 'COCO' yule Mchekeshaji maarufu!'

Tangu wakati huo mwaka 2004 Joe Kinnear alikuwa nje ya soka hadi wiki iliyopita.

Hivyo FA imetamka kifungo chake kimeanza kwa mechi ya Jumamosi walipofungwa 2-1 na Blackburn na mechi ya pili atakayoikosa ni ya tarehe 5 Oktoba 2008 watakapocheza na Everton.


RATIBA YA KOMBE la UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Kesho na Jumatano viwanja mbalimbali Ulaya vitawaka moto kwa kuzikutanisha Klabu mahiri Ulaya katika mechi za Makundi ya kugombea Kombe la Klabu Bingwa Ulaya-UEFA CHAMPIONS LEAGUE .
Mabingwa watetezi Manchester United walioko Kundi E watakuwa ugenini nchini Denmark kupambana na Aalborg. Katika mechi ya kwanza ya Kundi hili Man U walitoka suluhu na Villarreal huko Old Trafford.
Arsenal watakuwa nyumbani Emirates Stadium kupambana na FC Porto ya Ureno huku wakiomba dua safari hii wapate ushindi baada ya kunusurika kwenye mechi ya kwanza waliposawazisha bao dakika za mwisho walipocheza ugenini na Dynamo Kiev.
Chelsea baada ya kupata ushindi mnono nyumbani Stamford Bridge walipowafunga Bordeaux bao 4-0 sasa watakuwa nchini Romania kupambana na timu mpya kwenye mashindano haya CFR Cluj-Napoca iliyofanya maajabu kwenye mechi ya kwanza ilipoifunga timu yenye uzoefu na ngumu Roma ya Italia nyumbani kwake.
Nao Liverpool baada ya kushinda ugenini kwa bao 2-1 zidi ya Marseille sasa itakuwa nyumbani Anfield kupigana kuendeleza wimbi la ushindi watakapocheza na PSV Eindhoven ya Uholanzi iliyofungwa nyumbani na Atletico Madrid.
Jumanne, 30 Septemba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]


KUNDI E

Aalborg v Man U

Villarreal v Celtic

KUNDI F

Bayern Munich v Lyon

Fiorentina v Steau Bucharest

KUNDI G

Arsenal v Porto

Fenrbahce v Dynamo Kiev

KUNDI H

Bate v Juventus

Zenit St Petersburg v Real Madrid

Jumatano, 1 Oktoba 2008 [saa 3 dak 45 usiku saa za bongo]

KUNDI A

CFR Cluj-Napoca v Chelsea

Bordeaux v Roma

KUNDI B

Anorthosis Famagusta v Panathinaikos

Inter Milan v Werder Bremen

KUNDI C

Shakhtar Donetsk v Barcelona

Sporting Lisbon v Basle

KUNDI D

Atletico Madrid v Marseille

Liverpool v PSV

Sunday 28 September 2008



WIGAN 2 MANCHESTER CITY 1

Wakiwa na Wachezaji watatu ambao wamo Timu ya Taifa ya Brazil, Manchester City walijikuta wakibebeshwa bao 2-1 na Wigan katika mechi ya LIGI KUU iliyochezwa nyumbani kwa Wigan JJB Stadium.

Manchester City wakiwa na Wabrazil wao Robinho, Elano na Jo walishindwa kufurukuta kwa timu ya Wigan iliyocheza nguvu kazi tangu dakika ya kwanza hadi mwisho huku Mshambuliaji wao toka Misri Amr Zaki bila shaka ndie Mchezaji Bora wa mechi.

Wigan walitangulia kupata bao la kwanza kupitia kwa Valencia aliefunga kwa shuti murua na Manchester City wakasawazisha kibahati baada ya mpira kumbabatiza beki wao Kompany na kutikisa nyavu kufuatia frikiki.

Lakini Amr Zaki aliwafungia Wigan bao la ushindi kwa penalti baada ya Palacios wa Wigan kuchezewa rafu na Javier Garrido wa Manchester City.

Kipindi cha pili ingawa mechi ilichangamka sana hakuna mabao mengine yaliyopatikana.

Tottenham wazidi kushindiliwa misumari: wapigwa 2-0 na Portsmouth!

Sasa kibarua kinazidi kuwa kigumu kwa Meneja wa Tottenham kutoka Spain Juande Ramos baada ya Tottenham kupata kipigo kingine kwenye LIGI KUU leo walipofungwa 2-0 na Portsmouth kwenye Uwanja wa Portsmouth Fratton Park.

Tottenham ndio wameshika mkia kwenye msimamo wa LIGI KUU wakiwa na pointi mbili tu katika mechi 6 walizocheza.

Mabao yaliyowaua Tottenham yalifungwa na Jermaine Defoe na Peter Crouch. Ingawa Portsmouth walimaliza mechi wakiwa 10 baada ya Kiungo wao Lassana Diara kupata kadi mbili za njano na hivyo kutolewa kwa kadi nyekundu Tottenham walionyesha dhahiri hawana ubavu wowote.

Portsmouth: James, Johnson, Campbell, Distin, Belhadj, Little, Diarra, Hughes, Armand Traore, Crouch, Defoe. AKIBA: Ashdown, Kaboul, Hreidarsson, Pamarot, Utaka, Mvuemba, Kanu.

Tottenham: Gomes, Corluka, Dawson, Woodgate, Assou-Ekotto, Bentley, Jenas, Zokora, O'Hara, Gilberto, Pavlyuchenko. AKIBA: Cesar, Huddlestone, Lennon, Bent, Modric, Gunter, Giovani.

REFA: Mike Dean (Wirral).



MECHI ZA LEO JUMAPILI 28 SEPTEMBA 2008

Portsmouth v Tottenham [saa 9 na nusu mchana];

Wigan v Man City [saa 12 jioni];


LIGI KUU UINGEREZA:
WASEMAYO MAMENEJA WA TIMU VIGOGO BAADA YA MECHI ZA JANA:
-Sir Alex Ferguson wa Mabingwa Man U kuhusu penalti tata iliyowapa bao la kwanza kwenye mechi waliyowafunga Bolton 2-0 alisema kwa mzaha: 'Nilishangaa maana niliona mchezaji wao kacheza mpira! Lakini huyu Refa Rob Styles msimu uliopita alitunyima penalti 4 au 5 za wazi! Naona sasa anatulipa! Sasa tunamdai penalti 4!!'
-Arsene Wenger wa Arsenal baada ya kuadhiriwa uwanjani kwake Emirates na timu 'kibonde' Hull City iliyopanda daraja msimu huu kwa mara ya kwanza tangu ianzishwe kwa kufungwa bao 2-1 tena kwenye siku aliyokuwa akiadhimisha miaka 12 ya kuwa Meneja wa Arsenal. Wenger alihuzunika: 'Tulikuwa si waangalifu pengine moyoni tulijiamini tutashinda kwa vyovyote vile! Hull walijituma na sie tulikosa nafasi nyingi! Hata tungeshinda sina sababu ya kusherehekea miaka 12 hapa!!'
-Luis Felipe Scolari wa Chelsea walipoifunga Stoke City bao 2-0: 'Tunajiamini na timu inacheza vizuri ingawa si soka ya kupendeza!'
-Meneja wa Liverpool Rafael Benitez baada ya kuwafunga watani wa jadi Everton bao 2-0 uwanja wa Everton Goodison Park kwa mabao yaliyofungwa na Fernando Torres: 'Sifa si kwa Torres peke yake ni timu nzima kwani wamecheza vizuri kitimu!'
Powered By Blogger