Saturday 20 September 2008

MATOKEO KAMILI YA LEO:

SUNDERLAND 2 v MIDDLESBROUGH 0

BLACKBURN 1 v FULHAM 0

LIVERPOOL 0 v STOKE CITY 0

WEST HAM 3 v NEWCASTLE 1

BOLTON 1 v ARSENAL 3

MECHI ZA KESHO:

JUMAPILI, 21 Septemba 2008

[saa 8 mchana bongo taimu]

WEST BROM v ASTON VILLA

[saa 10 jioni bongo taimu]

CHELSEA v MAN U

[saa 11 jioni bongo taimu]

HULL CITY v EVERTON

MAN CITY v PORTSMOUTH

TOTTENHAM v WIGAN

BOLTON 1 ARSENAL 3

Arsenal wakicheza ugenini waliibuka na ushindi wa bao 3 kwa 1 Uwanjani Reebok nyumbani kwa Bolton.
Bolton ndio walioanza kutungua nyavu za Arsenal kwa goli la kichwa la Kevin Davies.
Arsenal wakacharuka na kupiga bao mbili za haraka kupitia Emmanuel Eboue na Nicklas Bendtner.
Hadi mapumziko Bolton 1 Arsenal 2.
Kipindi cha pili Arsenal wakapata bao safi lililofuatia shambulio la haraka kupitia Denilson.

Friday 19 September 2008


LIGI KUU YAPAMBA MOTO:


  • LIVERPOOL WAKWAA KISIKI CHA VIBONDE!!

  • ZOLA AANZA VYEMA: TIMU YAKE WEST HAM YASHINDA!!

  • BLACKBURN 1 FULHAM O

Baada ya kuwafunga Mabingwa wa LIGI KUU Man U wiki iliyopita leo uwanjani kwake Anfield Liverpool walikwama kuifunga timu 'kibonde' Stoke City iliyopanda daraja msimu huu kwa kulazimishwa sare ya 0-0. Liverpool, wakiwa na kikosi kamili wakiwemo Nahodha Steven Gerrard na Mshambuliaji staa Fernando Torres, walilazimisha wimbi baada ya wimbi la mashambulizi lakini Stoke City walisimama imara. Liverpool walipata kona zaidi ya 20 lakini zote hazikufua dafu! Hata pale walipofunga goli ambalo wengi walidhani ni halali kabisa Refa alilikataa.
Gianfranco Zola akishika hatamu kwa mara ya kwanza kama Meneja wa West Ham alishuhudia timu yake ikiifunga timu isiyo na Meneja Newcastle kwa bao 3-1. Newcastle kwa sasa inaongozwa kwa muda na aliekuwa msaidizi Chris Houghton baada ya Kevin Keagan kujiuzulu alipokasirishwa na menejimenti kuuza wachezaji bila kumhusisha. West Ham ilipata goli mbili za kwanza kupitia Mtaliana David de Michele na la tatu alilitengeneza Mtaliana huyo huyo kwa kumpasia Matthew Etherington aliefunga.
Michael Owen aliwafungia Newcastle bao la moja.
Huko Ewood Park nyumbani kwa Blackburn Rovers, Matt Derbyshire alifunga goli moja na la ushindi baada ya Roque Santa Cruz kumpasia kwa kichwa safi cha ujanja kufuatia krosi murua ya Carlos Villanueva na hivyo kuwapiga wageni wao Fulham kwa bao 1-0.
MECHI YA VIGOGO KESHO: vimbwanga vyaanza!!

-FERGUSON: CHELSEA WANATUOGOPA!!

-SCOLARI ACHOCHEA: RONALDO ANAKARIBISHWA CHELSEA!!

-WENGER: BORA DRO KWANI KILA TIMU ITAPOTEZA POINTI!!

Meneja Sir Alex Ferguson wa Manchester United amesisitiza kuwa Chelsea wanajua wazi kikosi chake kina uwezo wa kushinda nyumbani kwa Chelsea Uwanja wa Stamford Bridge.
Mpaka sasa Chelsea hawajafungwa katika mechi 84 za ligi walizochezea uwanja wao wa Stamford Bridge na mara ya mwisho kufungwa hapo ilikuwa mwaka 2005.
Mpaka sasa Chelsea imecheza mechi 4 na ina pointi 10 wakati Man U ina pointi 4 kwa mechi 3.
Endapo Chelsea watashinda basi timu ya Luiz Felipe Scolari watakuwa mbele kwa pointi tisa zaidi ya Man U kitu ambacho Sir Alex Ferguson hataki kitokee ingawa timu yake imecheza mechi moja pungufu
Ferguson alisema: "Chelsea wanajua fika Manchester United wanaweza kushinda Jumapili. Wao ni timu nzuri na wameaanza ligi vizuri. Lakini timu yangu ina uwezo. Tuna kazi kubwa lakini wachezaji wangu wana ari kubwa.”
Ferguson akaongeza: “Ronaldo ananikera kila dakika anataka kuanza Jumapili. Amefanya mazoezi mazito na yuko fiti.”
Nae Luiz Felipe Scolari ametia utambi mechi hii kwa kudai atapendelea sana kama Cristiano Ronaldo atakuja kuwa mchezaji wa Chelsea kwani anaamini ni Mchezaji Bora Duniani jambo ambalo bila shaka limelengwa kumuudhi Sir Alex Ferguson.
Scolari aliwahi kumfundisha Ronaldo wakati akiwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Ureno ambayo Ronaldo huchezea.
Nae Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, amesema wao wanaomba timu zote zipoteze pointi kwa kutoka suluhu.
Arsenal leo wanasafiri hadi Bolton kucheza na Bolton mechi itakayoaanza saa 1 na nusu usiku bongo taimu.
CHOPRA AWAINUA SUNDERLAND!
-apachika bao mbili!

Katika mechi ya LIGI KUU UINGEREZA iliyoanza mapema Mshambuliaji wa Sunderland Michael Chopra akitokea benchi na aliingizwa tu baada ya Teemu Tainio kuumia bega alifunga bao 2 na kuwapa Sunderland ushindi kwenye uwanja wake wa nyumbani uitwao Stadium of Light zidi ya Middlesbrough.
Middlesbrough 'walizawadiwa' penalti baada ya Mshambuliaji wao Aliadiere kujiangusha kwenye boksi.
Downing akapaisha penalti hiyo.
FERGUSON NA WENGER: sasa ni marafiki?

Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ilikuwa si kitu cha ajabu kusikia au kuona Mameneja Sir Alex Ferguson wa Manchester United na Arsene Wenger wa Arsenal wakizozona huku timu zao zikipambana vikali uwanjani.
Lakini kwa sasa kuna kila dalili mizozo hiyo imekwisha na Mameneja hao wana msimamo mmoja.
Hali hii ilithibitika siku kadhaa zilizopita walipokuwa wageni rasmi waalikwa kwenye chakula cha usiku cha Chama cha Mameneja wa Ligi huko Uingereza ili kutunisha mfuko wao wa kusaidia jamii.
Katika hafla hiyo, Mameneja wote hao wawili walipata fursa ya kuhutubia na wote walionyesha sasa wana msimamo mmoja. Wote waliwaunga mkono Kevin Keagan aliekuwa Meneja wa Newcastle na Alan Curbishley wa West Ham waliolazimika kujiuzulu kwa sababu ya kuingiliwa kazi zao na wamiliki wa Klabu hizo.
Sir Alex Ferguson alitamka:'Kwa mazingira ya sasa ambayo klabu zinatawaliwa na Wenyeviti vijana matajiri sana, lazima uwe na mafanikio kama Meneja lakini utapataje mafanikio hayo ikiwa Mwenyekiti huyohuyo anawauza Wachezaji wako bora nyuma ya mgongo wako ili azidi kutajirika na vilevile anataka timu ishinde! Bila shaka Keagan na Curbishley wamefanya kitendo cha heshima kujiuzulu ili kutetea msimamo wao!'
Wenger akamuunga mkono Ferguson kwa kusema:'Meneja ni mtu muhimu sana kwenye klabu!! Kama si muhimu kwanini anafukuzwa kazi timu ikifanya vibaya?' Nadhani mimi na Ferguson tuna bahati kwani tuliweza kufanya kazi bila kuingiliwa hivyo tulikuwa huru kujenga timu bora.'
Walipoulizwa kuhusu uhsiano wao binafsi kwa sasa, Wenger alitamka:'Sasa tuna maelewano vizuri sana kati yetu na tunaheshimiana sana.'
Nae Ferguson akaongeza:'Sasa tunakaa na kunywa mvinyo na chakula pamoja! Tushakutana mara nyingi kwenye vikao vya Mameneja hasa kule Geneva. Wote tuna timu changa na bora na tuna ushindani.'

Thursday 18 September 2008

MAPYA:

-ESSIEN AFANYIWA UPASUAJI

Kiungo wa Chelsea Michael Essien leo amepasuliwa goti lake huko Ufaransa baada ya kuumizwa wakati akichezea nchi yake Ghana ilipocheza na Libya mjini Tripoli wiki iliyokwisha kwenye mechi ya kuwania kuingia Fainali Kombe la Dunia Afrika Kusini mwaka 2010.
Inakadiriwa Essien atakuwa nje ya uwanja kwa miezi 6.

-RAY WILKINS ATEULIWA MENEJA MSAIDI CHELSEA

Ray Wilkins aliewahi kuzichezea klabu za Chelsea, Man U, AC Milan, PSG na QPR ameteuliwa kuwa msaidi wa Meneja Luis Felipe Scolari kuchukua nafasi ya Steve Clarke alieacha kazi juzi kwenda kujiunga na Meneja mpya wa West Ham Gianfranco Zola.
Ray Wilkins alishawahi kuwa na nafasi hiyo hapo Chelsea kati ya mwaka 1998 na 2000 wakati Meneja wa Chelsea alikuwa Gianluca Vialli.

-FA KUCHUNGUZA KAULI YA SIR ALEX FERGUSON KUHUSU KUTENGULIWA KADI YA JOHN TERRY

Chama cha Soka Uingereza kimetamka kinachunguza kauli za Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson alipomponda Bosi wa Marefa Keith Hackett kwa kuleta shinikizo ili Nahodha wa Chelsea John Terry afutiwe kadi nyekundu.
Meneja huyo wa Manchester United, Sir Alex Ferguson juzi alibwata: 'Hacket alimlazimisha Refa Mark Halsey aifute kadi nyekundu iwe njano lakini refa alipogoma sasa kashushwa na wikiendi hii hachezeshi mechi za LIGI KUU! Atachezesha mechi ya Daraja la Tatu [inaitwa LEAGUE TWO]! Angekuwa mchezaji wa Man U Hackett asingefanya hili!!!'
Wikiendi hii Refa Mark Halsey kapangiwa kuchezesha mechi ya LEAGUE TWO kati ya Chester na Shrewsbury.

RATIBA YA LIGI KUU UINGEREZA WIKIENDI HII

JUMAMOSI, 20 Septemba 2008

[saa 8 dak 45 mchana bongo taimu]
SUNDERLAND v MIDDLESBROUGH;

[saa 11 jioni bongo taimu]

BLACKBURN v FULHAM;

LIVERPOOL v STOKE CITY;

WEST HAM v NEWCASTLE;

[saa 1 na nusu usiku bongo time]

BOLTON v ARSENAL ;

JUMAPILI, 21 Septemba 2008

[saa 8 mchana bongo taimu]

WEST BROM v ASTON VILLA ;

[saa 10 jioni bongo taimu]

CHELSEA v MAN U;

[saa 11 jioni bongo taimu]

HULL CITY v EVERTON ;

MAN CITY v PORTSMOUTH;

TOTTENHAM v WIGAN

Wednesday 17 September 2008

MABINGWA MAN U WATOKA DRO!
-Arsenal wachomoa dakika za mwisho!

Mabingwa watetezi Man U wamekwama kuwafunga Villarreal katika mechi ambayo washabiki wengi wa Man U watalalamika refa hakutenda haki baada ya kuwanyima penalti mbili za wazi.

Huko Ukraine Arsenal walipigwa bao la penalti yenye utata lakini Nahodha William Gallas akachomoa dakika za mwisho.
MATOKEO KAMILI:

KUNDI E:

MAN U 0 V VILLAREAL 0,

CELTIC 0 V AALBORG O,

KUNDI F:

STEAU BUCHAREST 0 V BAYERN MUNICH 1,

LYON 2 V FIORENTINA 2,

KUNDI G:

PORTO 3 V FENERBAHCE 1,

DYNAMO KIEV 1 V ARSENAL 1,

KUNDI H:

JUVENTUS 1 V ZENIT O,

REAL MADRID 2 V BATE 0,

UTATA WA KUFUTWA KADI NYEKUNDU YA JOHN TERRY: Ferguson aponda uamuzi, Scolari asema hajapata kuona maishani uamuzi wa Refa unafutwa!!

Kufuatia Chelsea kushinda rufaa iliyomfutia Nahodha wake kadi nyekundu aliyopewa Jumamosi iliyokwisha kwenye mechi ambayo Chelsea waliifunga Man City 3-1, kumezuka mzozo mkubwa huko Uingereza kuhusu uhalali wa kuifuta kadi hii.
Refa wa mechi Mark Halsey aliyotoa kadi hiyo nyekundu aliandika kwenye ripoti yake ya mechi kuwa kadi ilitoka kwa sababu ya 'rafu mbaya' na si 'faulo ya kiprofesheni' kama wengi wanavyodai.
Ili mchezaji atolewe nje kwa 'faulo ya kiprofesheni' inabidi awe beki wa mwisho anaemzuia kwa njia isiyo halali mchezaji kwenda kufunga.
Siku hiyo wakati John Terry akitenda kosa hilo nyuma yake alikuwa beki mwenzake Carvalho aliekuwa akija kukaba nyuma na vilevile beki mwingine wa Chelsea Bosingwa alikuwa tayari amefika kumsaidia Terry na Carvalho.
Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, ameuponda uamuzi huu na kuuita upendeleo uliotokana na shinikizo la Bosi wa Marefa Keith Hackett ambae siku za nyuma ashawahi kukwaruzana na Ferguson.
Ferguson alibwata: 'Hacket alimlazimisha Refa Mark Halsey aifute kadi nyekundu iwe njano lakini refa alipogoma sasa kashushwa na wikiendi hii hachezeshi mechi za LIGI KUU! Atachezesha mechi ya Daraja la Tatu [inaitwa LEAGUE TWO]! Angekuwa mchezaji wa Man U Hackett asingefanya hili!!!'
Wikiendi hii Refa Mark Halsey kapangiwa kuchezesha mechi ya LEAGUE TWO kati ya Chester na Shrewsbury.
Nae Meneja wa Chelsea Luis Felipe Scolari ameshangazwa na uamuzi huo wa kufuta kadi na kusema: 'Hii ni mara ya kwanza katika maisha yangu ya ukocha kuona kadi nyekundu inafutwa na uamuzi wa refa unabadilishwa!! Nadhani ni Uingereza tu hili linatokea!! Nchi nyingine refa ni Mungu!!'
Kama kadi nyekundu ya John Terry ingesimama palepale basi asingecheza mechi ya Jumapili ambapo Chelsea inaikaribisha Man U Stamford Bridge.
Kukerwa kwa Ferguson bila shaka kumezidishwa na ukweli kuwa siku hiyohiyo Jumamosi Beki wake wa kutumainiwa Nemanja Vidic alipewa kadi mbili tata za njano hivyo kupata nyekundu na kutolewa nje ya mechi waliyofungwa 2-1 na Liverpool.
Beki huyo ataikosa mechi ya Jumapili na Chelsea.
Hata hivyo Man U hawakukata rufaa.
MAN U KUANZA KUTETEA TAJI LAO LEO!!!

==Arsenal wako Kiev ambako hawajahi kushinda!!!!

Manchester United, Mabingwa wa Ulaya, leo wanaanza utetezi wao wa Kombe la UEFA Champions League kwa kucheza nyumbani kwao Old Trafford na timu ngumu ya Spain Villarreal katika mechi ya KUNDI E na kujaribu kuweka historia ya kuwa Bingwa wa kwanza mtetezi wa Kombe la LIGI ya MABINGWA wa UEFA kumudu kutetea taji lake.
Tangu mfumo wa kutafuta Klabu Bingwa Ulaya ubadilishwe [pamoja na kubadilisha jina la michuano hii] kutoka mtindo wa mtoano na kuja mtindo wa ligi na kutoka jina la Kombe la Ulaya na sasa kuitwa LIGI ya MABINGWA wa UEFA hapo mwaka 1992, hakuna hata timu moja iliyonyakua kombe hili ikafanikiwa kulitetea msimu unaofuata mara baada ya kulinyakua.
Timu pekee iliyokaribia kuweka historia ni Klabu ya Juventus ya Italia ambayo ilinyakua Kombe la LIGI ya MABINGWA wa UEFA mwaka 1997 kwa kuifunga Borrusia Dortmund lakini wakakwama mwaka uliofuata walipopigwa kibao 1-0 na Real Madrid kwenye Fainali ya mwaka 1998.
Mechi nyingine kwenye kundi la Man U ni kati ya Aalborg ya Denmark na Celtic ya Scotland.
Katika kuanza utetezi wa taji lao Man U huenda wakaongezewa nguvu baada ya kujulikana Mchezaji na Mfungaji Bora Ulaya Cristiano Ronaldo amepona. Man U watawakosa Viungo Michael Carricl alievunjika mfupa mguuni siku ya Jumamosi kwenye mechi na Liverpool na Paul Scholes ambae amefungiwa mechi hii baada ya kula kadi nyekundu kwenye mechi ya Super Cup zidi ya Zenit St Petersburg.
Vilevile kuna hatihati ya Mchezaji mpya Dimitar Berbatov kucheza baada ya kupata maumivi ya goti kwenye gemu ya Jumamosi ya Liverpool na Meneja Sir Alex Ferguson amesema kama hachezi nafasi iko wazi kwa Manucho, Fowadi hatari wa Angola, kupewa namba.
TIMU ITATOKA KWA HAWA:
Van der Sar, Kuszczak, Foster, Brown, Neville, R Da Silva, Ferdinand, Vidic, Evans, O'Shea, Evra, F Da Silva, Ronaldo, Nani, Hargreaves, Anderson, Possebon, Fletcher, Park, Giggs, Tevez, Rooney, Berbatov, Manucho, Welbeck.

Nao Arsenal ambao wako KUNDI G wanaanza kampeni yao leo kwa kuwatembelea Dynamo Kiev na historia inaonyesha hawajahi kushinda huko kwenye nchi za umoja wa zamani wa Kirusi hata siku moja!

Mwaka 1998 na 2003 walifungwa huko Kiev na 2006 walipigwa na CSKA Moscow wakati 2001 walibamizwa na Spartak Moscow.

Hata Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri: 'Mechi za huku ni ngumu sana! Tumepata matatizo huku kwani kila mara wanatushangaza kwa jinsi wanavyojitutumua na kujituma. Lakini safari hii tumeshajifunza!'

Mechi nyingine kwenye KUNDI G la Arsenal ni PORTO V FENERBAHCE.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE UWANJANI TENA LEO!!!

==MABINGWA MAN U WAANZA UTETEZI WA TAJI LAO na Mchezaji, Mfungaji Bora Ulaya RONALDO dimbani leo!!!
JUMATANO 17 SEPTEMBA 2008
[mechi saa 3 dak 45 usiku kwa saa za bongo]




KUNDI E:

MAN U V VILLAREAL,

CELTIC V AALBORG,

KUNDI F:

STEAU BUCHAREST V BAYERN MUNICH,

LYON V FIORENTINA,

KUNDI G:

PORTO V FENERBAHCE,

DYNAMO KIEV V ARSENAL,

KUNDI H:

JUVENTUS V ZENIT,

REAL MADRID V BATE,
LIVERPOOL NA CHELSEA WAANZA VYEMA

-AS ROMA WAPIGWA MWELEKA KWAO NA TIMU MPYA!
Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard ameiongoza vyema timu yake na kuifungia mabao mawili na kuwashinda Marseille kwa mabao 2-1 katika mechi ya KUNDI D.
Marseille wakiwa uwanjani kwao Stade Velodrome walitangulia kupata bao dakika ya 23 baada ya Nahodha wao Lorik Cana kuvunja mtego wa kuotea na kutikisa nyavu.
Dakika chache baadae Steven Gerrard akasawazisha kwa bao murua na akafunga la pili kwa penalti baada ya Torres kufanyiwa madhambi.
Katika mechi nyingine ya kundi hili la Liverpool KUNDI D, PSV iliadhiriwa kwa mabao 3-0 na Atletico Madrid.
Nao Chelsea wakichezea Uwanja wao Stamford Bridge waliwabandika Bordeaux ya Ufaransa mabao 4-0 katika mechi ya KUNDI A.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Frank Lampard, Joe Cole, Florent Malouda na Nicolas Anelka.
Katika mechi nyingine ya kundi hili la Chelsea timu iliyotegemewa sana AS Roma ikicheza nyumbani kwake ilipigwa mweleka na timu mpya na isiyojulikana kabisa kwenye michuano hii CFR Cluj kutoka Romania kwa mabao 2-1.
Christian Panucci aliwapa AS Roma bao la kutangulia dakika ya 17 lakini Juan Culio kutoka Argentina aliisawazishia timu yake CFR Cluj kwenye dakika ya 27 na tena kupachika bao la ushindi dakika ya 49.

MATOKEO KAMILI NI:

KUNDI A:
Chelsea 4-0 Bordeaux;
Roma 1-2 CFR Cluj-Napoca;

KUNDI B:
Panathinaikos 0-2 Inter Milan ;
Werder Bremen 0-0 Anorthosis Famagusta;

KUNDI C:
Barcelona 3-1 Sporting;
Basle 1-2 Shakhtar Donetsk;

KUNDI D:
Marseille 1-2 Liverpool;
PSV 0-3 Atletico Madrid;

Tuesday 16 September 2008


LEO USIKU UEFA CHAMPIONS LEAGUE KUTIMUA VUMBI ULAYA!!

Mechi nane zinachezwa miji mbalimbali Ulaya leo usiku saa 3 dakika 45 saa za kibongo na zitakutanisha timu zenye matumaini tofauti.
Kwa sasa ukweli uliopo Ulaya ni kwamba timu za Uingereza ndizo zinazotawala Soka ya Klabu huko Ulaya na hili linadhihirishwa na kuweza kuingiza timu tatu kwenye Nusu Fainali ya michuano hii msimu uliokwisha na hatimaye kuingiza timu zao mbili Fainali huku Manchester United ikiibuka Bingwa.
Vilevile, kwenye tuzo ya Wachezaji Bora, Klabu hizo zilizoa tuzo zote kwani Ronaldo wa Man U aliibuka ndie Mchezaji na Mfungaji Bora, huku tuzo za Kipa, Mlinzi na Kiungo Bora zikienda kwa Wachezaji wa Chelsea ambao ni Petr Cech, John Terry na Frank Lampard.
Katika mechi za leo nane, Klabu za Uingereza zinazocheza ni Chelsea na Liverpool na mechi zao ni: Chelsea v Bordeaux na Marseille v Liverpool.
Timu nyingine Ulaya ambazo ni tishio na ambazo zipo uwanjani leo ni Barcelona, Inter Milan na AS Roma.
Timu ngeni kabisa ambazo zipo dimbani leo ni Anorthosis Famagusta ya Cyprus na timu ya Romanian CFR Cluj.
MECHI KAMILI NA MAKUNDI YA TIMU NI:
KUNDI A

CHELSEA v BORDEAUX

AS ROMA v CFR CLUJ

KUNDI B

PANATHINAIKOS v INTER MILAN

WERDER BREMEN v ANORTHOSIS FAMAGUSTA

KUNDI C

BARCELONA v SPORTING LISBON

BASEL v SHAKHTAR DONETSK

KUNDI D

MARSEILLE v LIVERPOOL

PSV EINDHOVEN v ATLETICO MADRID

CHELSEA WASHINDA RUFAA YA JOHN TERRY!!!

Klabu ya Chelsea imeshinda rufaa waliyokata kwa FA kupinga kadi nyekundu aliyopewa Nahodha wao John Terry kwenye mechi na Manchester City iliyochezwa Uwanja wa City of Manchester ambayo Chelsea walishinda 3-1 wikiendi iliyokwisha.
Hivyo, Terry yuko huru kuikabili Man U watakapocheza Jumapili kwenye mechi ya LIGI KUU uwanjani Stamford Bridge.

MICHAEL CARRICK NJE WIKI SITA!!!

Kiungo wa Mabingwa Man U Michael Carrick atakuwa nje ya uwanja kwa wiki 6 baada ya kuthibitishwa amevunjika mfupa mguuni baada ya kuumizwa na Yossi Benayoun Jumamosi katika mechi ya Liverpool na Man U.
Huu ni mkosi kwa Carrick kwani alikuwa ndio kwanza tu amerudi uwanjani baada ya kuwa nje kwa wiki 3 baada ya kuumia enka.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE:


CHELSEA v BORDEAUX

saa 3 dak 45 usiku [bongo taimu]
Leo timu iliyobwagwa Fainali ya michuano hii msimu uliopita na Mabingwa Man U ikiongozwa na Meneja Mbrazil Luis Felipe Scolari, Chelsea, inashuka uwanjani kwake STAMFORD BRIDGE kupambana na timu ya Ufaransa Bordeaux ambayo inaongozwa na Meneja Laurent Blanc aliekuwa Nahodha wa Timu ya Taifa ya Ufaransa iliyotwaa Kombe la Dunia mwaka 1998 na vilevile tutamkumbuka kuwa aliwahi kuwa Beki wa Mabingwa Man U. [PICHANI NI LAURENT BLANC na SCOLARI wakicheka pamoja].
Mpaka leo Laurent Blanc ndie anaeshikilia rekodi ya kuwa Mchezaji 'mzee' aliefunga bao kwenye michuano hii ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE pale alipofunga goli wakati akichezea Man U kwenye mechi na Olympiakos Oktoba 2002. Alifunga goli hilo akiwa na miaka 36 na siku 339.
Leo Chelsea itamkosa Mfungaji wao stadi Didier Drogba ambae amefungiwa kucheza baada ya kupewa kadi nyekundu kwenye mechi ya Fainali ilipobwagwa na Man U huko Moscow mwezi Mei.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE:

MARSEILLE v LIVERPOOL

saa 3 dak 45 usiku [bongo taimu]

MECHI LAIVU DSTV SS3

Baada ya furaha ya kuishinda Man U Jumamosi kwa mabao 2-1, leo Liverpool wanatua nchini Ufaransa mjini Marseille kwenye uwanja uitwao STADE VELODROME kupambana na Timu ngumu ya Marseille kwenye mechi ya KUNDI D. Msimu ulioisha timu hizi zilikuwa Kundi moja na Marseille walimudu kuwatungua Waingereza hao bao 1-0 Uwanja wa Anfield ingawa nao walitwangwa mabao 4-0 kwenye uwanja huu wao wa nyumbani.
Leo Liverpool wanategemea kuwaanzisha nyota wao Nahodha Steven Gerrard na Mshambuliaji Fernando Torres.
Nao Marseille watakuwa tena na nyota wao ambao walikuwa majeruhi Mathieu Valbuena na Hatem Ben Arfa.
TIMU YA LIVERPOOL INATEGEMEWA KUWA:
Reina, Dossena, Arbeloa, Agger, Skrtel, Carragher, Gerrard, Alonso, Mascherano, Lucas, Benayoun, Babel, Kuyt, Torres, Riera, Keane, Cavalieri, Degen.


MECHI ZA LEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE:

JUMANNE 16 SEPTEMBA 2008

CHELSEA V BORDEAUX,

ROMA V CFR,

PANATHINAIKOS V INTER MILAN,

BREMEN V ANORTHOSIS,

BASEL V SHAKHTAR,

BARCELONA V SPORTING LISBON,

PSV V ATLETICO MADRID,

MARSEILLE V LIVERPOOL
[mechi iko laivu DSTV SS3]

TOTTENHAM 1 ASTON VILLA 2
Timu ya Tottenham ikicheza nyumbani uwanjani kwake White Hart Lane imepigwa bao 2-1 na Aston Villa jana usiku. Mpaka sasa Tottenham wamecheza mechi nne za LIGI KUU UINGEREZA na wameambulia pointi moja tu walipotoka suluhu ya bao 1-1 na Chelsea.
Aston Villa walipata bao la kwanza dakika ya nne tu ya mchezo baada ya krosi ya Gabriel Agbonlahor kumaliziwa kirahisi na Nigel Reo-Cocker. Goli la pili la Villa lilipatikana kwenye dakika ya 54 baada ya shuti dhaifu la Ashley Young kumpita kiajabu Kipa wa Tottenham Heurelho Gomes.
Darren Bent aliwapatia Tottenham kifuta machozi kwenye dakika ya 87.
Tottenham jana waliwachezesha kwa mara ya kwanza Wachezaji wao wapya Mshambuliaji wa Urusi Roman Pavlyuchenko na Beki wa Croatia Vedran Corluka.

Monday 15 September 2008



CHELSEA WAIKATIA RUFAA KADI NYEKUNDU YA NAHODHA JOHN TERRY!!

Klabu ya Chelsea leo imekata rufaa kwa FA kupinga kadi nyekundu aliyopewa Nahodha wao John Terry juzi kwenye mechi na Manchester City iliyochezwa Uwanja wa City of Manchester ambayo Chelsea walishinda 3-1.
Kwa mujibu wa ripoti ya Refa Mark Halsey, John Terry alipewa kadi nyekundu kwa kucheza rafu mbaya na si kwa kumzuia Mshambuliaji wakati akiwa ndio beki wa mwisho ambayo kitaaluma huitwa 'rafu ya kiprofesheni'.
Rufaa hii itasikilizwa kesho.
Endapo rufaa itabwagwa basi Nahodha John Terry atakosa mechi tatu ya kwanza ya Jumapili tarehe 21 Septemba 2008 zidi ya Mabingwa wa LIGI KUU Manchester United, ya pili ni ya Kombe la Carling watakayocheza na Portsmouth Septemba 24 na ya mwisho na Stoke City ambalo ni pambano la LIGI KUU.
RONALDO KUONEKANA UWANJANI JUMATANO!!




Cristiano Ronaldo, Mchezaji Bora na Mfungaji Bora wa LIGI KUU UINGEREZA pamoja na LIGI YA MABINGWA YA ULAYA, atarudi tena uwanjani siku ya Jumatano wakati timu yake ambayo pia ni Mabingwa wa LIGI KUU UINGEREZA pamoja na ULAYA Manchester United itakapocheza na Villareal ya Spain kwenye michuano ya LIGI YA MABINGWA ULAYA Uwanjani Old Trafford.
Ronaldo alifanyiwa operesheni ya enka mwezi Julai na ilitegemewa atakuwa nje ya uwanja hadi mwezi Oktoba lakini sasa amepata nafuu haraka na Meneja Sir Alex Ferguson amethibitisha atacheza mechi hiyo.
Wakati Ronaldo akiwa nje ya uwanja alihusishwa sana na habari kwamba atahamia Real Madrid taarifa ambazo ziliwakera wapenzi wengi wa Man U.
Hata hivyo Ronaldo mwenyewe amesema haogopi jinsi washabiki watakavyompokea siku hiyo kwani yeye siku zote amekuwa akicheza kwa moyo mmoja na nguvu zake zote daima anapovaa jezi ya Man U.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE yaanza kesho!

Ule uhondo wa kuona Klabu kubwa za Ulaya zikichuana kuwania Ubingwa wa Klabu za Ulaya unaanza kesho.

Klabu hizi zimegawanywa kwenye Makundi manane ya timu nne nne na kila Kundi litacheza mtindo wa ligi. Timu mbili za juu za kila kundi ndizo zitakazosonga mbele kwenye raundi inayofuata ambayo itachezwa kwa mtindo wa mtoano
Timu toka Uingereza ni Bingwa mtetezi wa michuano hii Manchester United, mshindi wa pili wa Kombe hili Chelsea, Arsenal na Liverpool.

RATIBA YA MECHI NI IFUATAVYWO [mechi zote zitaanza saa 3 dakika 45 usiku saa za bongo]:

JUMANNE 16 SEPTEMBA 2008

CHELSEA V BORDEAUX

ROMA V CFR

PANATHINAIKOS V INTER MILAN

BREMEN V ANORTHOSIS

BASEL V SHAKHTAR

BARCELONA V SPORTING LISBON

PSV V ATLETICO MADRID

MARSEILLE V LIVERPOOL

JUMATANO 17 SEPTEMBA 2008

MAN U V VILLAREAL

CELTIC V AALBORG

STEAU BUCHAREST V BAYERN MUNICH

LYON V FIORENTINA

PORTO V FENERBAHCE

DYNAMO KIEV V ARSENAL

JUVENTUS V ZENIT

REAL MADRID V BATE
LIGI KUU UINGEREZA:
STOKE CITY 2 EVERTON 3
Everton jana waliwafunga nyumbani kwao Stoke City timu iliyopanda daraja msimu huu mabao 3-2 katika mechi ya vuta ni kuvute.
Everton walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Mnigeria Yakubu dakika ya 41 na kwenye dakika ya 51 Victor Anichebe akafunga la pili kwa Everton.
Stoke City wakajitutumua na kufunga la kwanza kwa bao la Olofinjana dakika ya 55 na kisha mlinzi wa Everton Jagielka akajifunga mwenyewe na kufanya ngoma kuwa 2-2.
Lakini kwenye dakika ya 77 kona iliyopigwa na Arteta ilimaliziwa na Tim Cahill kwa kichwa safi na kuwapa ushindi Everton wa mabao 3-2.
Kwenye mechi hii Meneja wa Everton David Moyes alilambwa kadi nyekundu na Refa Alan Wiley baada ya kulalamika kwa nguvu kwa Refa wa akiba kuhusu timu yake kunyimwa penalti ya dhahiri na hivyo ikabidi aondolewa kwenye benchi la akiba na kwenda kumalizia mechi kwenye jukwaa la watizamaji.
LIGI KUU inaendelea leo usiku saa 4 [bongo time] kwa mechi kati ya Tottenhan na Aston Villa.
Powered By Blogger